LowasaSupporter
Member
- Dec 3, 2011
- 5
- 0
Nadhani watu tunajua ya kuwa ni ushabiki na chuki binafsi za akina Sita, Ninauye, Membe, Kikwete, Nyalandu na wengine wengi ambao wamezijenga kwa Lowassa. Na pia tukubali ya kuwa uwezo wa Lowassa kikazi unawapa taabu hawa jamaa. Yupi kati ya hawa ni msafi? Membe ambaye amechukua pesa kutoka kwa Quaddafi ili kujikuza kisiasa hapa Tanzania, Sitta ambaye anasafarisha magogo nje ya Tanzania, Kikwete ambaye anachakachua nchi kupitia kijana wake Ridhwani? Nyalandu ambaye amejenga jumba kwenye kiwanja kichotengwa kwa ajili ya ujenzi wa dispensari? Yupi anaweza kumtupia mawe akisema mikono yake ni ya haki? Nadhani baadhi ya watanzania tumekuwa wanafiki sana, chuki hii kwa Lowassa imeanza kufifia na hakuna mwaka mmoja zaidi wimbo huu wa kumchafua Lowassa utakuwa unakubalika tena na watanzania. Yaliyopagwa na mungu binadamu hawezi kutegua, kama Mungu anataka Lowasa kuwa rais wa nchi hii atakuwa, wala siyo hao wenye kuvaa ngozi ya kondoo wakipita wakisema huyu hafai, huyu hivi, yule vile, kama ni fisadi toeni ushahidi. Msije mkakuta mnatoa hukumu pasipo haki....Msihukumu msije mkahukumiwa kwa kukosa kiongozi thabiti...Msidanganyike na hawa wenye hila binafsi akina Sitta, Membe na kundi lake?Atakuwa anakata tawi alilokalia...hana ubavu!