geraldkowero1
JF-Expert Member
- Jul 5, 2014
- 1,838
- 644
shida ya lowasa ni kupata urais kwa njia yoyote , usibishe mkuu , ichukue kama tetesi , kwa mujibu wa gazeti la Tanzania daima lowasa ni mfadhili wa ACT , hii habari si ya leo wala jana .
Chochote chaweza tokea ingawa katu siamini kama kweli Lowasa anaweza kuhamia ACT au hata chama kingine cha upinzani. Endapo ikatokea kuwa amehama ccm kwenda ACT basi huo utaeleweka ulikuwa ni mkakati wa m-badala wa ccm kuunda ACT na baada ya ushindi wa uraisi ambae atakuwa Lowasa ACT itajiunga na ccm na jina la chama kufutika na kubaki CCM na wanachama wote wa ACT kupewe kqdi mpya za ccm. Hayo watakuwa walishakubaliana na kiongozi mkuu wa ACT. Chama kingine cha upinzani Lowasa hawezi kujiunga nacho kwani anaelewa ccm watashinda na utakuwa ndio mwisho wake na mali zake.