Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Gazeti la Mtanzania likidhani ndiyo linamjenga JK kumbe la hasha limemnukuu Bw. Lowasa akimnadi mgombea wa CCM wa Uraisi JK kwenye kichwa cha khabari kisemacho.........."JK hana mpinzani na zamu hii atashinda kwa kishindo kikubwa zaidi....."
Tatizo hapa ni kuwa kama mwaka 2005 JK alipata asilimia 80 inamaanisha ya kuwa Lowasa anatarajia JK kuvuka hicho kiwango jambo ambalo haliwezekani hata kidogo......
Hivyo Lowasa amenithibitishia ya kuwa ameshindwa kuzisoma alama za wakati hata chembe na ni vyema akajikita kutetea kiti chake cha ubunge ambacho kipo kwenye hati hati ya kuporwa na mgombea ubunge wa Chadema ambaye yaelekea ndiyo chaguo la wengi hapo Monduli hata kumlazimu Bw. Lowasa kuigiza kampeni za JK za kuitumia familia yake kwa minajili ya kulinda ulaji wake hapo bungeni............
Tatizo hapa ni kuwa kama mwaka 2005 JK alipata asilimia 80 inamaanisha ya kuwa Lowasa anatarajia JK kuvuka hicho kiwango jambo ambalo haliwezekani hata kidogo......
Hivyo Lowasa amenithibitishia ya kuwa ameshindwa kuzisoma alama za wakati hata chembe na ni vyema akajikita kutetea kiti chake cha ubunge ambacho kipo kwenye hati hati ya kuporwa na mgombea ubunge wa Chadema ambaye yaelekea ndiyo chaguo la wengi hapo Monduli hata kumlazimu Bw. Lowasa kuigiza kampeni za JK za kuitumia familia yake kwa minajili ya kulinda ulaji wake hapo bungeni............