Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Liyumba aendeleza mapambano
Friday, 24 December 2010 20:27
James Magai na Tausi Ally
KIGOGO wa zamani katika Benki Kuu ya Tanzania, Amatus Liyumba, ameamua kuendelea kupinga adhabu ya kifungo cha miaka miwili anayoendelea kuitumikia.
Hatua hiyo imekuja baada ya kugonga ukuta katika rufaa yake ya kwanza ya kupinga hukumu hiyo iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Mei 24 mwaka huu.
Katika hukumu hiyo ya rufaa hiyo iliyosomwa Jumanne wiki hii,Jaji Emilian Mushi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, alitupilia mbali rufaa hiyo na kwamba hukumu na adhabu ya Mahakama ya Kisutu ni sahihi.
Uamuzi umemfanya Liyumba kuzidi kusota gerezani akitumikia adhabu hiyo.
Hata hivyo tayari Liyumba kupitia kwa jopo la mawakili wake, linaloongwa na Majura Magafu akisadina na Jaji mstaafu Hilary Mkate, Hudson Ndusyepo na Onesmo Kyauke wameshawasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa katika Mahakama ya Rufani.
Wakili Magafu alilithibitishia Mwananchi jana kuwa waliwasilisha taarifa hiyo Jumatano ya wiki hii.
Liyumba aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Benki Kuu (BoT) alihukumiwa kifungo hicho baada ya kupatikana na hatia ya matumizi mabaya ya Ofisi za umma.
Lakini Mei 28 mwaka huu, Liyumba kupitia kwa jopo la mawakili wake, alipinga adhabu hiyo huku akitoa sababu 12 za kufanya hivyo.
Sababu hizo ni pamoja na madai kuwa Mahakama ya Kisutu ilikosea kisheria na kiukweli katika kutathmini ushahidi na utetezi na kwamba ilkiuka kanuni zilizowekwa na mahakama za juu katika kutoa adhabu.
Lakini katika hukumu ya rufaa hiyo Jaji Mushi alitupilia mbali utetezi wa Liyumba na mawakili wake, na kuunga mkono hoja za upande wa mashtaka na hukumu ya Mahakama ya Kisutu.
Katika hukumu hiyo yenye kurasa 60 aliyoisoma kwa muda wa saa mbili dakika na nne, Jaji Mushi alisema hukumu na adhabu hiyo ilikuwa ni sahihi.
Friday, 24 December 2010 20:27
James Magai na Tausi Ally
KIGOGO wa zamani katika Benki Kuu ya Tanzania, Amatus Liyumba, ameamua kuendelea kupinga adhabu ya kifungo cha miaka miwili anayoendelea kuitumikia.
Hatua hiyo imekuja baada ya kugonga ukuta katika rufaa yake ya kwanza ya kupinga hukumu hiyo iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Mei 24 mwaka huu.
Katika hukumu hiyo ya rufaa hiyo iliyosomwa Jumanne wiki hii,Jaji Emilian Mushi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, alitupilia mbali rufaa hiyo na kwamba hukumu na adhabu ya Mahakama ya Kisutu ni sahihi.
Uamuzi umemfanya Liyumba kuzidi kusota gerezani akitumikia adhabu hiyo.
Hata hivyo tayari Liyumba kupitia kwa jopo la mawakili wake, linaloongwa na Majura Magafu akisadina na Jaji mstaafu Hilary Mkate, Hudson Ndusyepo na Onesmo Kyauke wameshawasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa katika Mahakama ya Rufani.
Wakili Magafu alilithibitishia Mwananchi jana kuwa waliwasilisha taarifa hiyo Jumatano ya wiki hii.
Liyumba aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Benki Kuu (BoT) alihukumiwa kifungo hicho baada ya kupatikana na hatia ya matumizi mabaya ya Ofisi za umma.
Lakini Mei 28 mwaka huu, Liyumba kupitia kwa jopo la mawakili wake, alipinga adhabu hiyo huku akitoa sababu 12 za kufanya hivyo.
Sababu hizo ni pamoja na madai kuwa Mahakama ya Kisutu ilikosea kisheria na kiukweli katika kutathmini ushahidi na utetezi na kwamba ilkiuka kanuni zilizowekwa na mahakama za juu katika kutoa adhabu.
Lakini katika hukumu ya rufaa hiyo Jaji Mushi alitupilia mbali utetezi wa Liyumba na mawakili wake, na kuunga mkono hoja za upande wa mashtaka na hukumu ya Mahakama ya Kisutu.
Katika hukumu hiyo yenye kurasa 60 aliyoisoma kwa muda wa saa mbili dakika na nne, Jaji Mushi alisema hukumu na adhabu hiyo ilikuwa ni sahihi.