LIVE UPADTES: M4C DAR - Lengo ni Kukusanya Bilioni 5 CHANGIA MABADILIKO

Wadau tufahamishane ni kiasi gani kimepatikana kwenye harambee ya Jana!
 
Imebaki kiasi gani kupata chopa?Tofautisha michango ya wananchi na Mafisadi hiyo 5 bilion si anatoa nani pekee yake?then kesho watanzania tunamlipa na faida juu!

Chopa moja ni $300,000 zaidi ya milioni 400 piga hesabu wewe imebaki kiasi gani.
 
Salaam wakuu!
Naomba kumshauri mwenyekiti wa M4C bwana Godbless Lema kuwa ubabe hauna tija kwa CDM. Kauli kwamba "makampuni ya simu wakidhubutu kutuhujumu tutapita mtaani na kukusanya card zao na kuzitumbukiza chooni"!! Huu ni ujuaji. Cdm ni chama makini kinachochipukia kinatakiwa ustaarabu na maadili kukijenga chama na kukifikisha kule watanzania wanakotaka. Kutumia lugha na kauli za kujikweza kabla hata ya kukamata dola inanipa mashaka sana kama mwanachama. Ikiwa kama hawa ndio mawaziri tunaowategemea, mbona hawatakuwa na tofauti na hawa wa CCM tulionao!!

Nawatakia kila la heri.
Mungu ibariki Chadema, Mungu ibariki Tanzania.

Maneno ya busara sana haya nimeyapenda mkuu, kauli zina matter sana kwenye communications kama hizi. ahadi za visasi hazijengi CDM kinatakiwa kuonesha unyenyekevu wa hali ya juu kwa wananchi, na sio tu kuonesha bali ku practise.
 
Katika hali iliyotarajiwa na wengi michango hiyo imeonekana ni mradi wa viongozi wa Chadema, ebu waambieni wananchi taingia muanze kuwachangisha watanzania mmeishawapa mchanganunuo wa matumizi yenu kuna mfuasi wa Chadema yeyote anajua matumizi ya ruzuku ya Chadema.

Lema anasimama anasema nataka bilioni tano nikanunue Chopa mbili na magari 100 unataka ukanune Chopa wakati ofisi mmepanga vyumba vitatu pale Kindondoni mtaa Ufipa.

Lema, Mbowe, Slaa, tuone michanganuo ya michango mnayowachangisha wananchi wambieni michango imefanya a.b.c siyo kukaa kimya
 
Lema amezoea kuongea na machalii, pia ana hasira ya hukumu dhidi ya ubunge wake. Ni vizuri kukaonekana kwamba walioandaa shuhuli walijipanga ikiwa ni pamoja na kupanga nani aongee na aongee nini. Ilikuwa wazi kwamba mtu pekee aliyejiandaa atasema nini na kwa malengo gani ni Mbowe

Nitafurahi kama next event itaonekana kuna order fulani ambayo waandaaji walijipanga na kukubaliana. Ikiwezekana Lema akae mezani tu aache walioandaliwa kuongea na kuendesha shuhuli.

Endeleeni kuchangia, kwa SMS tuma neno Chadema kwenda 15710. Kwa benki CRDB akaunti namba 01j1080100600
 
Tatizo la CDM kwa sasa ni kuset priorities. Huwezi kuniambia kama kweli ni akili kwa chama kununua magari ya 5bn wakati bado kina mambo mengi ya msingi ya kufanya. Kumbuka mpaka sasa CDM hakiwezi kujiendesha chenyewe, kinategemea sana donations. Wangeangalia kwanza njia mbadala za kukuza kipato. Nimewadharau sana kwa kitendo cha kuwa na mpango wa kununua magari ya 5bn!!! Tena Lema anasema kabisa zikipatikana zaidi wananua na helkopta, na tayari ameshaichagua hiyo helkopta.

Kuna njia nyingi sana za kuwafikia wananchi, siyo lazima kwa magari, helkopta na pikipiki. Serikali yetu imejitahidi sana kukuza mawasiliano. Wangeitumia vizuri hii advantage ya improvement ya communication sector ambayo ni cost effective kuliko kutegemea njia za kizamani kuwafikia wanachi.

Naamini kama ni badiliko yanaletwa na wananchi wenyewe wa eneo husika, sidhani kama ni lazima mchaga atoke moshi na Arusha aje kunishawishi mimi mmakonde nibadilike. Hii movement yao naona ni njia tu ya loserz kama Dr Slaa na Lema ya kujiongezea kipato!!

Eti Rejao anaishauri CDM,tsk! stk! tk!! for whose interests? wonders will never end!!
 
Katika hali iliyotarajiwa na wengi michango hiyo imeonekana ni mradi wa viongozi wa Chadema, ebu waambieni wananchi taingia muanze kuwachangisha watanzania mmeishawapa mchanganunuo wa matumizi yenu kuna mfuasi wa Chadema yeyote anajua matumizi ya ruzuku ya Chadema.

Lema anasimama anasema nataka bilioni tano nikanunue Chopa mbili na magari 100 unataka ukanune Chopa wakati ofisi mmepanga vyumba vitatu pale Kindondoni mtaa Ufipa.

Lema, Mbowe, Slaa, tuone michanganuo ya michango mnayowachangisha wananchi wambieni michango imefanya a.b.c siyo kukaa kimya

USIWE JUHA!!

Kwani Nyerere alivyoenda UNO kudai uhuru aliporudi watanganyika waliomchangia nauli waliuliza mchanganuo wa matumizi yake?

Siku zote UHURU huja kwa kujitolea!!
 
tayari new ufisadilism on the work mnazoibia mashirika ya umma pamoja na wabunge wenu kushindwa kuwatosha na kugundulika, meanzish harakati za mabadiliko kta wizi wa fedha, mmegundua watanzania wajinga na malimbukeni wa mitandao hivyo kwakushirikiana na media wizi wenu utafanikiwa. Hongereni kwa kuamua kuanzisha Mabadiliko Fisadilism Changamkieni.Mabadiliko Filisi Chako.
 
Nimefurahi mmejua umuhimu kuwa na pesa ili kuimarisha chama,tunatkiwa kufika mpaka vjijini,hvyo gari,pikipiki,baiskeli nk vinahitajika pamoja na gharama za kuviendesha!huwezi kufungua ofisi sehemu bila kukujua ndo maana tunakwenda kwanza tunawaelewesha nia yetu kwanza alafu mambo ya ofisi yanafuata,si unajua kile chama cha majambazi kilivyowalaza watz wengi usingizi,lkn watatoka usingizini hakuna kulala mpk kieleweke.watz ukombozi umekuja changamkeni,nyie ndo wakombozi wa nchi yenu,mia,mia mbili,mia tano,elfu moja,elfu tano na elfu kumi yako inahitajika lakini wewe ni muhimu sana ktk kuikomboa nchi hii.ALUTA CONTINUA
 
Katika hali iliyotarajiwa na wengi michango hiyo imeonekana ni mradi wa viongozi wa Chadema, ebu waambieni wananchi taingia muanze kuwachangisha watanzania mmeishawapa mchanganunuo wa matumizi yenu kuna mfuasi wa Chadema yeyote anajua matumizi ya ruzuku ya Chadema.

Lema anasimama anasema nataka bilioni tano nikanunue Chopa mbili na magari 100 unataka ukanune Chopa wakati ofisi mmepanga vyumba vitatu pale Kindondoni mtaa Ufipa.

Lema, Mbowe, Slaa, tuone michanganuo ya michango mnayowachangisha wananchi wambieni michango imefanya a.b.c siyo kukaa kimya

Pilipili ipo mikononi mwako endelea kusambaza maeneo mengine ya mwili......
Wapeni wananchi Michanganuo wa Chenji za EPA na Rada. Vipi kuhusu malipo ya Dowans na mauzo ya Kiwira,Loliondo,Twiga waliosafirishwa wakiwa hai.....shame on u
 
kwani hayo makampuni ya simu si ndio itakuwa kiama chao,wajaribu waone kwani hao ccm wangapi si wanahesabika yaani wepesi kuliko karatasi
 
Back
Top Bottom