Chromium
JF-Expert Member
- Apr 17, 2008
- 589
- 185
Nilisikitishwa na kitendo cha Lipumba kumponda Dr. Slaa kwa kisingizio cha kujibu swali kwamba anamwuunga nani kati ya Dr. Slaa na Bw.Kikwete ambao ndio wanaoonekana kuwa washindani wa kweli. Kwa nini kama kweli ni mpinzani wa kweli, asingetumia fursa hiyo kumponda Kikwete? Kulikuwa na ulzama gani wa yeye kumponda vile Dr. Slaa? Hata mshiriki mmoja alimwomshangaa kwa kumponda mpambanaji mwenzie, bado aliendelea kumponda?! Yaani adui wa adui yako anakuwa rafiki yako?!
Kubwa zaidi, alihitimisha kwa kumwita Bw. Kikwete mtani (swahiba) wake.
Siku moja baadae, vipinzani vingine vinajitokeza eti vinamwunga mkono Kikwete baada ya Mtengeneza silaha kujitoa! halafu Mbatia naye ametangaza bifu na CHADEMA.
My take: CHADEMA wanapambana na maadui wengi wa ndani ya upinzani wenyewe wanaotumiwa na CCM. Wengi wanaojiita wapiznani si lolote ni majizi tu yanayotaka kuharibu mapambano yaliyofikia kilele chake hivi sasa.
Ushauri: CHADEMA wasifanye kosa kumwamini yeyote (hawa wapinzani) baada ya kushinda uchaguzi.
Ukweli CHADEMA kama CHADEMA haihitaji kushirikiana na yeyote. Uamuzi mlioufanya awali ulikuwa sahihi.
Tujiandae kuona mabadiliko kesho.
Kubwa zaidi, alihitimisha kwa kumwita Bw. Kikwete mtani (swahiba) wake.
Siku moja baadae, vipinzani vingine vinajitokeza eti vinamwunga mkono Kikwete baada ya Mtengeneza silaha kujitoa! halafu Mbatia naye ametangaza bifu na CHADEMA.
My take: CHADEMA wanapambana na maadui wengi wa ndani ya upinzani wenyewe wanaotumiwa na CCM. Wengi wanaojiita wapiznani si lolote ni majizi tu yanayotaka kuharibu mapambano yaliyofikia kilele chake hivi sasa.
Ushauri: CHADEMA wasifanye kosa kumwamini yeyote (hawa wapinzani) baada ya kushinda uchaguzi.
Ukweli CHADEMA kama CHADEMA haihitaji kushirikiana na yeyote. Uamuzi mlioufanya awali ulikuwa sahihi.
Tujiandae kuona mabadiliko kesho.