Elections 2010 Lipumba na wapinzani wengine wamejidhalilisha

Chromium

JF-Expert Member
Apr 17, 2008
589
185
Nilisikitishwa na kitendo cha Lipumba kumponda Dr. Slaa kwa kisingizio cha kujibu swali kwamba anamwuunga nani kati ya Dr. Slaa na Bw.Kikwete ambao ndio wanaoonekana kuwa washindani wa kweli. Kwa nini kama kweli ni mpinzani wa kweli, asingetumia fursa hiyo kumponda Kikwete? Kulikuwa na ulzama gani wa yeye kumponda vile Dr. Slaa? Hata mshiriki mmoja alimwomshangaa kwa kumponda mpambanaji mwenzie, bado aliendelea kumponda?! Yaani adui wa adui yako anakuwa rafiki yako?!

Kubwa zaidi, alihitimisha kwa kumwita Bw. Kikwete mtani (swahiba) wake.

Siku moja baadae, vipinzani vingine vinajitokeza eti vinamwunga mkono Kikwete baada ya Mtengeneza silaha kujitoa! halafu Mbatia naye ametangaza bifu na CHADEMA.

My take: CHADEMA wanapambana na maadui wengi wa ndani ya upinzani wenyewe wanaotumiwa na CCM. Wengi wanaojiita wapiznani si lolote ni majizi tu yanayotaka kuharibu mapambano yaliyofikia kilele chake hivi sasa.

Ushauri: CHADEMA wasifanye kosa kumwamini yeyote (hawa wapinzani) baada ya kushinda uchaguzi.

Ukweli CHADEMA kama CHADEMA haihitaji kushirikiana na yeyote. Uamuzi mlioufanya awali ulikuwa sahihi.

Tujiandae kuona mabadiliko kesho.
 
Mkuu wahanya
uchambuzi wako ni yakinifu, wengi wanajipambanua kama wapinzani, ukweli ni mapandikizi ya chama cha kigaidi
 
Nyerere alishatabiri kuwa vyama vya siasa visizuiliwe, bala nitakufa kifo cha kwaida. Uchaguzi wa mwaka huu tunaona tuna vyama vinne CCM, CUF, Chadem na NCCR Mageuzi. Muda si mrefu, historia itaamua na tutakuwa na vyama viwili kama marekani yaani CCM ya wenye kitu na Chadema cha walalahoi.
 
Chadema huu ndio mwisho wao amini usiamini ,na hata nyota zimejipanga kuonyesha kuwa chama cha udini ukabila kinafikia mwisho wake. Jamani tusiandikie tuwache huu muda wa masaa kumi na mbili yaani hadi kesho wakati kama huu tutakuwa na dakika chache kuelewa bichi na bivu.
 
Back
Top Bottom