Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wadau:
Kufuatana yanayoendelea kujitokeza katika CUF, sasa naanza kupata mwanga kwa nini Prof. Lipumba alionekana kutetea ufisadi na mafisadi. Aliwahi kujitokeza hadharani kabisa kuhusu vitu viwili:
1. Aliwahi kutetea ununuzi wa mitambo chakavu ya Dowans, bila kujali ufisadi ulioikumba mitambo hiyo tangu Richmond.
2. Baada tu ya Mzee Mengi kuwataja mafisadi papa - akiwemo Rostam, Profesa aliitisha mkutano wa waandishi na kumpinga Mengi kuhusu hatua yake dhidi ya mafisadi.
Sasa kwa kuwa tumesikia kwamba Rostam na Jussa ni maswahiba wakubwa sana kibiashara kiasi cha Hamad Rashid kumuomba Jussa amuombee mkopo wa Sh bil moja toka kwa Rostam, basi ni dhahiri Rostam amekuwa akikifadhili CUF au viongozi wake na pengine Profesa kufaidika kwa namna fulani hapo.
Mie nadhani Lwakatare na Pro Safari wanajua mengi kuhusu Rostam na CUF, na hasa Lwakatare kwani kulikuwapo andiko moja, yaani barua aliyomwandikia Prof Lipumba wakati anaki9hama chama. Alitaja kitu kimoja alichokuwa anakipinga, kwamba Baraza Kuu la chama hicho huwa hakilazimiki kutoa vyanzo vya mapato mengine ya chama hicho mabli na ruzuku kutoka serikali.
Kufuatana yanayoendelea kujitokeza katika CUF, sasa naanza kupata mwanga kwa nini Prof. Lipumba alionekana kutetea ufisadi na mafisadi. Aliwahi kujitokeza hadharani kabisa kuhusu vitu viwili:
1. Aliwahi kutetea ununuzi wa mitambo chakavu ya Dowans, bila kujali ufisadi ulioikumba mitambo hiyo tangu Richmond.
2. Baada tu ya Mzee Mengi kuwataja mafisadi papa - akiwemo Rostam, Profesa aliitisha mkutano wa waandishi na kumpinga Mengi kuhusu hatua yake dhidi ya mafisadi.
Sasa kwa kuwa tumesikia kwamba Rostam na Jussa ni maswahiba wakubwa sana kibiashara kiasi cha Hamad Rashid kumuomba Jussa amuombee mkopo wa Sh bil moja toka kwa Rostam, basi ni dhahiri Rostam amekuwa akikifadhili CUF au viongozi wake na pengine Profesa kufaidika kwa namna fulani hapo.
Mie nadhani Lwakatare na Pro Safari wanajua mengi kuhusu Rostam na CUF, na hasa Lwakatare kwani kulikuwapo andiko moja, yaani barua aliyomwandikia Prof Lipumba wakati anaki9hama chama. Alitaja kitu kimoja alichokuwa anakipinga, kwamba Baraza Kuu la chama hicho huwa hakilazimiki kutoa vyanzo vya mapato mengine ya chama hicho mabli na ruzuku kutoka serikali.