Kwakweli kauli hii imetoka mdomoni kwa mtu makini anayeelewa ni nini anafanya kwa maslahi ya taifa. Kauli ya Lipumba inaashiria kwamba endapo Dr. Slaa angetangaza nia mapema, basi yeye Lipumba angeweza kujitoa ili kumpisha Slaa. Natamani akina MS KN na Tumain waseme lolote kuhusu hili.
Upo sahihi kabisa Lumbe. Natamani Lipumba angekuwa anaweza kusoma hoja yako hii. Mimi pia nafikiri kwamba kwa kuwa Lipumba anajua wazi kwamba hawezi kushinda, na anajua wazi kwamba Dr Slaa yupo fit, ampe support ili wachukue nchi halafu wakubaliane terms za kugawana madaraka. Kuna kila sababu ya Lipumba kufanya hilo.hajachelewa anaweza akaiunga mkono CHADEMA - Lipumba ameshajaribiwa mara nyingi. Amsapoti mwenzake ili waitoe ccm na wakubaliane hata kupeana madaraka kuboresha maisha ya watz. na kuachiana kimajimbo ubunge na udiwani.