Elections 2010 Lipumba Amfagilia Dr. Slaa

Slaa na Lipumba wapi kwa wapi ,embu fanyeni uchambuzi wa kina juu ya mikoa yote na kura ambazo walipata vyama hivyo,inatakiwa mfahamu tu kura za wapiga kura wa vyama hivyo bado zipo na ni hazina ya vyama ,hakuna ithibati yeyote ile kuwa wanachama wa CUF wapatao laki moja wamerudisha kadi au kuacha chama na kujiunga na chama kingine.
 
Ninaomba majina ya wote wanaosema Lipumba muongo,mnafiki,mjinga.. mkiweza kutoa majina yenu tutaamini mnayoongea..

Naweza kuthubutu kusema kwa kinywa kipana kuwa hakuna kiongozi thabiti na mkweli ktk nchi hii kama Pr Lipumba.. alifikia mpaka kuvunjwa mkono kwa kuwatumikia wananchi,uhuru wa siasa za Tz umeanza kupatikana kupitia mgongo Pr Lipumba,maandamano yote alikuwa akiongoza yeye mwenyewe.. Namuamini Pr wa duniani.. Slaa ni makini lkn bado ni mchanga kwa Lipumba,slaa aliwajibika aongee na Lipumba waunde timu moja ambayo ingeongozwa na Lipumba,ungeona moto wake... lkn tatizo letu wapinzani wote kwa jumla kila mmoja anataka awepo juu ya mwenzake.. haya hapo ndipo ccm inapochekelea..
 
Kwakweli kauli hii imetoka mdomoni kwa mtu makini anayeelewa ni nini anafanya kwa maslahi ya taifa. Kauli ya Lipumba inaashiria kwamba endapo Dr. Slaa angetangaza nia mapema, basi yeye Lipumba angeweza kujitoa ili kumpisha Slaa. Natamani akina MS KN na Tumain waseme lolote kuhusu hili.

hajachelewa anaweza akaiunga mkono CHADEMA - Lipumba ameshajaribiwa mara nyingi. Amsapoti mwenzake ili waitoe ccm na wakubaliane hata kupeana madaraka kuboresha maisha ya watz. na kuachiana kimajimbo ubunge na udiwani.
 
hajachelewa anaweza akaiunga mkono CHADEMA - Lipumba ameshajaribiwa mara nyingi. Amsapoti mwenzake ili waitoe ccm na wakubaliane hata kupeana madaraka kuboresha maisha ya watz. na kuachiana kimajimbo ubunge na udiwani.
Upo sahihi kabisa Lumbe. Natamani Lipumba angekuwa anaweza kusoma hoja yako hii. Mimi pia nafikiri kwamba kwa kuwa Lipumba anajua wazi kwamba hawezi kushinda, na anajua wazi kwamba Dr Slaa yupo fit, ampe support ili wachukue nchi halafu wakubaliane terms za kugawana madaraka. Kuna kila sababu ya Lipumba kufanya hilo.
 
Back
Top Bottom