Linda Smart phone yako,Flat TV,Home theater,na computer visiungue dhidi ya radi au short ya umeme

Transistor

JF-Expert Member
Aug 8, 2013
970
1,461
Kabla ya kujua ubunifu wa leo unahusu nini;naomba nikuulize maswali yafuatayo.


JE? ulisha wahi kushuhudia:-,

* Flat TV au TV ya kawaida wakati wa kuwasha au wakati unaangalia ghafla inaungua?


*Radio ambazo ni smart mfano Home Theatre ikiungua wakati unaitumia/ikiwa stand-by au wakati wa kuiwasha?


*Simu aina ya Smartphone zikiungua au kilipuka ghafla kama bomu wakati wa kuzi-charge kwa kutumia umeme?




*Computer Desk-top au (Laptop wakati wa kuicharge)zikiungua ghafla wakati zimepachikwa kwenye umeme?


*Baadhi ya taa za umeme katika nyumba yako hazimalizi hata siku mbili zinaungua hovyo?


*Unalipa bili ya umeme kubwa kuliko matumizi yako,japo umejaribu kufatilia wirering ya umeme ya nyumba yako na mambo mengine yote unaona yako sawa lakini bill ya umeme bado iko juu?


Uharibifu huu unasababishwa na mabadiliko ya tabia ya umeme yanayo tokea ndani ya sekunde kadhaa tu;lakini huacha uharibifu mkubwa kwa vifaa vya umeme.


Hali hii kitaalamu inaitwa Voltage surge(kama tatizo limetokana kutokana na voltage) au Current surge(kama tatizo limetokana na Current)


Japo wengi wanaitambua kwa umaarufu wa jina moja tu yaani VOLTAGE SURGE!



Zingatia


SURGE haiwezi kuzuiliwa na na stabilizer ya kawaida, ndio maana unaweza ukawa unatumia stabilizer lakini bado kifaa chako kikaungua, Vifaa vya kuzuia surge ni vifaa maalumu vilivyo tengenezwa kwa ajili ya kazi hiyo tu!


Vifaa vingi vinavyo ungua na surge mfano TV au computer, ukipeleka kwa fundi mara nyingi utaambiwa kuwa POWER SUPPLY ndiyo imeungua!


Lakini simu ikiungua kutokana na voltage surge mara nyingi huwa ni ya kutupa!


*Kwa kuorodhesha tu vyanzo vikubwa vinavyo sababisha kutokee Voltage Surge katika nyumba yako ni:-


1.Radi


2.Mashirika ya usambazaji wa umeme husababisha kutokea kwa voltage surge kwenye makazi ya watu kutokana na kuzima na kuwasha umeme mara kwa mara, pamoja na mifumo mibovu ya usafirishaji wa umeme kutoka katika transformer hadi kwa wateja kama vile loose connection n.k


3.Fridge au Freezer


4.Wirering Mbovu


5.Air Conditioners


6.Motor(za visima vya maji, kufungua mageti, na lift n.k)


7.Photocopy machines



Ni takribani mwaka mmoja na miezi kadhaa toka nilipo leta mada yangu hapa jamvini yenye kichwa cha habari "VOLTAGE SURGE"ni hatari ambayo wegi wanaishi ndani yake.


Kifaa hiki kina-suppress vitu vikubwa viwili ambavyo ni hatari kwa vifaa vyetu majumbani ambavyo ni Voltage surge pamoja na Current surge, hivyo kifaa hiki sio voltage surge protector tena bali ni Voltage and Current Surge Protector(VCSP) .ambacho ni hiki hapa chini









Kabla sijaanza kuelezea kitaalamu jinsi kifaa hiki kilivyo tengenezwa,ningependa nisiwachoshe wale wasiopenda kusoma maelezo marefu kwa kueleza kwa kifupi tu kifaa hiki kinavyo fanya kazi.

-Kifaa hiki kina Circuit muhimu MBILI

1.Delay and control circuit




Hii ni saketi ambayo inasaidia kuchelewesha kifaa chako cha umeme ulicho kipachika kwenye VCSP, kupokea umeme pale unavyo washa switch au umeme unapo rudi baada ya kukatika.

Kifaa hiki huzuia umeme huo kwa sekunde kadhaa ili kusubili umeme huo utulie kabisa ndipo kifaa hiki kita uruhusu umeme kuingia kwenye kifaa chako iwe simu,TV n.k.


Hivyo kamakuna surge yeyote ilikua imeambatana wakati umeme unarudi au wakati unawasha switch surge hiyo haita pata nafasi ya kukidhuru kifaa chako.

Saketi hii ina indicators ambazo zianaonyesha delaying process wakati umeme umeingia kwenye VCSP kabla ya kuingia kwenye kifaa chako Saketi yenyewe hii hapa!







Saketi ya pili ndiyo saketi muhimu zaidi na ndiyo inayo beba jukumu kuu la kulinda vifaa vyako


2.Surge suppresser circuit




(a)Kazi ya Varistor(Metal oxide varistor (MOV) katika saketi hii


MOVs kazi yake ni kuondoa kiwango cha umeme ambacho kinazidi kiwango cha kawaida katika mfumo wa umeme.


Kama ikitokea umeme ukazidi kiwango cha kawaida MOVs huanza kutengeneza ukinzani ambao utaondoa excess voltage katika line ya umeme.


Kwakuwa Voltage surge ni kitendo cha kuongezeka kwa kiwango cha umeme


ghafla kunako sababishwa na kitu kama vile radi au loose connection na ambacho hutokea kwa sekunde kadhaa tu,MOVS kazi yake ni kuondoa ongezeko hilo la umeme kwenye line ili isifike kwenye kifaa chako na kuleta madhara.


(b)Kazi ya Themistor katika saketi hii


Thermistor;ni kifaa maalumu ambacho kazi yake ni kuzuia inrush currents mara tu umeme unavyo rudi au switch inapo washwa.


Tambua kuwa kila kifaa cha umeme kina mahitaji yake ya kiwango cha current,hivyo kuruhusu kiwango chote cha current kuingia katika kifaa husika mara nyingine huleta madhara ya kifaa hicho kuungua;ndio maana vifaa vingi vya umeme huungua wakati wa kuwashwa;hii inasababishwa na inrush currents.




Kuondoa tatizo hilo thermistor hutumika ambapo umeme huanza kuingia katika thermister ndipo huingia katika kifaa cha umeme.


Baadaya ya umeme kuwaka thermister huwa na ukinzani mkubwa sana hivyo kuzuia kiwango cha current kisiingie moja kwa moja katika kifaa chako,baada ya hapo kwa kuwa kifaa husika kitakua kinahitaji kiwango fulani cha current ili kifanye kazi,kitavuta kiasi cha current ambacho chenyewe kinahitaji;kwa kuwa thermistor imezuia current hizo kuvutwa kwa current na kifaa chako cha


umeme kutasababisha thermistor ipate moto;thermistor ikipata moto ukinzani wake hupungua hivyo kuruhusu kile kiwango tu cha current ambacho kimehitajika na kifaa ulicho kipachika wakati huo!


Hivyo kwa kutumia thermister kifaa kitapewa current kutokana na mahitaji yake bila kuzidishiwa!


Hivyo tatizo la current surge linakuwa limeondoka!


(c) Kazi ya Ceramic Capacitor Y Capacitors-DIP katika saketi hii


Hii ni capacitor maalumu kwa ajili ya kuondoa Cheche zinazo tokea kwenye line ambazo zinaweza kupelekea surge(spaks killer)


Tambua kuwa unapowasha switch kuna cheche ambazo hutokea kutokana na kuungana kwa terminal mbili,au wakati mwingine kama line husika ina loose connection hupelekea kutokea kwa cheche,ambazo huweza kuleta surge;hivyo kuhakikisha tunaendelea kuwa salama dhidi ya surge tunalazimika kuondoa sparks za aina yeyote kwenye line yetu ndo mana Ceramic Y Capacitor-DIP ikatumika.


(d)Kazi ya Filter capacitor katika saketi hii

Kazi ya capacitors hizi kubwa mbili ni ku-smooth umeme unaoingia katika kifaa chako kuhakikisha hakuna mawimbi yasio hitajika yanajipenyeza katika kifaa chako cha umeme ambayo yanaweza kuleta madhara.


Pia kapacitor hizi zinasaidia kuhakikisha VCSP haizalishi mawimbi yatakayo ingiliana na mifumo mingine kama vile mawimbi ya radio,TV n.k


(e)Kazi ya Choke ferrite transformer katika saketi hii.

Kazi ya choke hii ni kuwa na sifa ya ku-Absorb excess voltage kwa kugeuza nguvu hiyo ya umeme iliyo zidi kuwa sumaku(electromagnetism).


Hivyo cke pia ni kifaa kingine muhimu katika kukabiliana na surge.


(f)Kazi ya Fuse katika saketi hii

Kwa kifaa ambacho kinatimia MOVs,ni lazima kifaa hicho kiwe na fuse,kutokana na ufanyaji kazi wa MOVs.


Kama Voltage surge itakuwa kubwa sana kuishina MOVs,kwa kawaida MOVs huzuia umeme kuingia kabisa katika saketi kwa kutengeneza short circuit ili fuse ikate.


Hivyo matumizi ya Fuse sehemu ambapo MOVs zimetumika hayakwepeki.


Hivyo ni vifaa vikubwa sita pamoja na mfumo wa delay ambavyo kila kimoja kila kinafanya kazi yake katika kuhakikisha umeme utakao kuwa unatoka katika output ya VCSP unakuwa Clean and safe kwa vifaa vyako vya umeme dhidi ya vyanzo vyote vya surge kama vile radi n.k


Saketi nzima ya kifaa hiki inaonekana hivi:-






Kwa upande wa nje features za kifaa hiki ni kama zinavyo enekana hapa chini;-






Tambua-Indicator nyekundu itakuwa ikiwaka kuonyesha umeme ni salama kwa matumizi na pia kuonyesha kuwa Thermistor na Varistor zinafanya kazi vizuri!


-Kwa usalama wa vifaa vyako nyumbani,nakushauri utumie kifaa hiki kuvirinda kwani hasara utakayo ipata baada ya simu yako au tv yako au home theater yako kuungua ni kubwa zaidi kuliko kununua kifaa hiki.


Vifaa ambavyo vipo kwenye hatari kubwa ya kuungua na voltage surge ni Flat TVs,Smart phones na Home theaters,kwani zinatumia soft technologies ambayo ipo vulnerable tu surge


Tuangalie youtube kifaa hiki kinavyo fanya kazi


 

Attachments

  • IMG_20141230_092725.jpg
    IMG_20141230_092725.jpg
    183.5 KB · Views: 998
  • IMG_20141230_092617.jpg
    IMG_20141230_092617.jpg
    122.2 KB · Views: 979
  • IMG_20141229_190905.jpg
    IMG_20141229_190905.jpg
    285.9 KB · Views: 998
  • IMG_20141229_185114.jpg
    IMG_20141229_185114.jpg
    52.4 KB · Views: 960
  • IMG_20141229_190922.jpg
    IMG_20141229_190922.jpg
    53 KB · Views: 891
  • e.jpg
    e.jpg
    361.6 KB · Views: 919
  • IMG_20150102_135243.jpg
    IMG_20150102_135243.jpg
    620.2 KB · Views: 882
  • iiiiiiiiiiiiiii.jpg
    iiiiiiiiiiiiiii.jpg
    783.8 KB · Views: 874
  • IMG_20150102_135351.jpg
    IMG_20150102_135351.jpg
    860.6 KB · Views: 863
Ndugu hichi kifaa kinapatikana Tanzania? kama kipo ni shillingi ngapi na wapi? na pia je hicho kifaa kinatofauti yoyote na stabilizer za kawaida?
 
Ndugu hichi kifaa kinapatikana Tanzania? kama kipo ni shillingi ngapi na wapi? na pia je hicho kifaa kinatofauti yoyote na stabilizer za kawaida?

Kifaa hiki ni tofauti na stabilizer,kama nilivyo eleza hapo juu,Stabilizer ina-deal na mabadiliko ya kupanda na kushuka kwa umeme katika speed ndogo zaidi tofauti na kifaa hiki ambacho kinatumia electronics parts maalumu kwa ajiri ya ku-track mabadiliko ya umeme kwa speed kali zaidi.

Na ndo maana unaweza ukawa unatumia stabilizer lakini bado vifaa vyako vikaungua!

Ku-deal na surge unatakiwa kutumia kifaa maalumu(Surge protector) na siyo stabilizer.

Kwa sababu voltage surge inatokea within nanoseconds!

Kifaa hiki kinaundwa Tanzania na mimi hapa!
Dukani vipo japo Surge nyingi za dukani zinatumia MOVs na choke pekee ili wasiuze gharama!
 
Bei gani mkuu na vinapatikana wapi?
Kifaa hiki ni tofauti na stabilizer,kama nilivyo eleza hapo juu,Stabilizer ina-deal na mabadiliko ya kupanda na kushuka kwa umeme katika speed ndogo zaidi tofauti na kifaa hiki ambacho kinatumia electronics parts maalumu kwa ajiri ya ku-track mabadiliko ya umeme kwa speed kali zaidi.

Na ndo maana unaweza ukawa unatumia stabilizer lakini bado vifaa vyako vikaungua!

Ku-deal na surge unatakiwa kutumia kifaa maalumu(Surge protector) na siyo stabilizer.

Kwa sababu voltage surge inatokea within nanoseconds!

Kifaa hiki kinaundwa Tanzania na mimi hapa!
Dukani vipo japo Surge nyingi za dukani zinatumia MOVs na choke pekee ili wasiuze gharama!
 
Mmh very exhaustive..hongera sana tutapataje na sisi wa Sumbawanga. Ebu ni whatssup nahitaji hicho kitu +61424679013 ASAP
 
Hebu tuambie. Umetaja vifaa viwili ambavyo ni rahisi sana kutaja bei. Umetaja maelezo mengi sidhani kama utashindwa kutaja bei kwa uwazi. Asante mkuu kwa kuwaelewa wateja wa JF wanaopenda uwazi na ukweli
 
Hiki kifaa kina tofauti gani na AVS?

AVS ni Voltage delay + Voltage Surge protector +High and Low voltage Ignore switching device!(imetaengenezwa maalumu kwa ajiri ya vitu kama vile Fridge+Freezer and Air Conditioners ili kuziepusha compressor zizifanye kazi kipindi cha low voltage,ili zisiungue(kinatumika kwa ajiri ya vifaa vya PIN tatu Live Neutral and Earth

VCSP ni Voltage delay+Voltage Surge protector+Current Surge protector+Voltage Filter device+Lightnning brocker device
Maalumu kwa ajiri ya vifaa vya electronics kam vile TV,Simu,Radio na computer(Inatumika kwa ajiri ya Vifaa vya PIN mbili LIVE and Neutral
 
Hebu tuambie. Umetaja vifaa viwili ambavyo ni rahisi sana kutaja bei. Umetaja maelezo mengi sidhani kama utashindwa kutaja bei kwa uwazi. Asante mkuu kwa kuwaelewa wateja wa JF wanaopenda uwazi na ukweli

Cheki bei kwenye inbox
 
Back
Top Bottom