Lijuakali aagiza polisi wamkamate Godbless Lema kwa uchochezi

DC kabla ya suspect kuwa arrested ni LAZIMA awe na docket police, DC nenda kwanza kafungue kesi police ili uchunguzi ufanyike, kama kuna kesi ya kujibu then ukamataji ndio utafanyika,upumbavu wa DC
 
Mpina alieagiza Mwigulu Mbarawa na Bossi wa Yepi Merkezi wakamatwe mbona amepuuzwa halafu mnakomaa na Nabii Lema?
 
DC kabla ya suspect kuwa arrested ni LAZIMA awe na docket police, DC nenda kwanza kafungue kesi police ili uchunguzi ufanyike, kama kuna kesi ya kujibu then ukamataji ndio utafanyika,upumbavu wa DC
Hahaha dc wa mchongo
 
Hahaha kwanini asimfungulie mashitaka kwanza kama kuna kosa akalitenda? kisha mahakama itampa taarifa ikiona anakosa la kujibu.
Kila mtu ana mamlaka ya kutuma polisi kukamata watu nchi hii.
 
DC wa Nkasi ameagiza vyombo kumsaka na kimtia nguvuni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chadema Godbless Lema Kwa kufanya Uchochezi akiwa kwenye mikutano ya Hadhara Wilayani Nkasi.

Naunga mkono wito Kwa sababu badala ya kufanya siasa wao wanafanya Uchochezi wa kuvunja amani ya Nchi.Na wale ambao wataendelea kufanya Uchochezi wapigwe marufuku kupanda majukwaani as specific individuals.


View: https://twitter.com/swahilitimes/status/1721953359471534242?t=cja3FsCVqhEU4Y2d-5s2bw&s=19
 
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Peter Lijualikali ameagiza Jeshi la Polisi kumsaka popote alipo na kumkamata Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema, ili ahojiwe kwa alichoeleza "kutoa kauli za uchochezi" kwenye mkutano wa hadhara Oktoba 24, 2023.

Katika video ambayo inasambaa kwenye mitandao ya kijamii, Lema anahamasisha wanaume wa Kijiji cha Korongwe Asilia, wamuue Mtendaji wa kijiji chao kwa madai ya kuwasumbua wananchi.

Hata hivyo Lema amezungumzia video hiyo kuwa, hakuhamasisha kitu kama hicho na asingeweza kutoa kauli kama hiyo badala yale aliwaambia wanaume wamuoe mtendaji huyo ili asiwasumbue jambo ambalo amejitetea kwa kusema "lugha za kisiasa."

Kwenye video hiyo, Lema akiwa na baadhi ya viongozi, wanachama na wafuasi wa Chadema katika Vitongoji vya Forodhani na Fipa, Kata ya Korongwe, anaonekana kutamka neno

ambalo limetafsiriwa na Mkuu wa

Wilaya kuwa ni kutaka wanaume wamuue mtendaji anayewasumbua.

Lijualikali amesema haiwezekani kiongozi mwenye ushawishi mkubwa wa watu aachiewe kutamba kwa kauli hiyo ambayo imesababisha taharuki kwa wananchi na Mtendaji huo ambaye kwa sasa maisha yake yako shakani, huku kiwango cha utendaji kikishuka.

"Namuagiza OCD wa Nkasi, kuchukua hatua za kisheria mara moja kumuita kokote aliko Godbles Lema ili afike Nkasi akafanyiwe mahojiano kuhusu kauli yake ya kichochezi ya kuhatarisha hali ya usalama wa mtendaji huyo katika eneo letu na kukwaza juhudi za wananchi kufanya shughuli za maendeleo," amesema Lijualikali.

Akijibu swali ni kwa nini jambo hilo lilitokea muda mrefu lakini wamechelewa kutoa taarifa, Mkuu wa Wilaya amesema walianza kwa uchunguzi kuhusu kauli hiyo ilikuwa na maana gani na ililenga nini kitokee na kwamba wamejiridhisha haikuwa kauli nzuri.
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Peter Lijualikali ameagiza Jeshi la Polisi kumsaka popote alipo na kumkamata Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kaskazini Godbless Lema ili ahojiwe kwa kauli za uchochezi alizozitoa kwenye mkutano wa hadhara Oktoba 24,2023.

Kwenye Mkutano huo ambao ulifanyika katika kata ya Korongwe jimbo la Nkasi Kaskazini ambako anaelezwa kuwa alitamka kuwa wanaume wa Kijiji Korongwe asilia wamuue Mtendaji wa Kijiji hicho Daud Ismail.

Hata hivyo Lema amekanusha madai ya uchochezi huo akisema alitamka kuwa wanaume ‘wamuoe’ mtendaji huyo akidai ni lugha za kisiasa na wala hakuna madhara yoyote kuhusiana na utendaji wake.

Imedaiwa Lema akiwa na baadhi ya viongozi, wanachama na wafuasi wa Chadema kwenye mkutano huo katika Vitongoji vya Forodhani na Fipa, Kata ya Korongwe, kwa makusudi alitoa kauli ya vitisho kwa mtumishi huo baada ya wananchi kulalamika kwenye mkutano huo kuwa wanasumbuliwa na Mtendaji huyo.

DC Lijualikali alisema haiwezekani kiongozi mwenye ushawishi kuachiwa atambe kwenye kauli hiyo ambayo imepeleka taharuki kubwa kwa wananchi na Mtendaji huo ambaye kwa sasa maisha yake yako hatarini.
Na ashughulikiwe barabara akitibitika na uovu huo....
Aman na utulivu ni jambo la msingi sana kuamua vitu kwa njia ya ubabe ni sawa na kuvuta fegi sheli
 

Attachments

  • haki na aman.jpg
    haki na aman.jpg
    122.3 KB · Views: 2
Back
Top Bottom