Leo nimenusurika kutapeliwa na madalali wawili tofauti, kuweni makini!

Precious Diamond

JF-Expert Member
Jun 9, 2023
397
993
Wakuu salama, niwape story kwa yaliyonikuta leo inaweza kumsaidia mtu.

Katika harakati za kutafuta nyumba maeneo ya Mbezi Beach nikakutana na madalali wawili kwa nyakati tofauti maeneo ya Makonde. Dalali mmoja akawa amenionesha nyumba stand alone ya vyumba 3 kwa kodi ya 500k kwa mwezi upande wa juu. Nikaenda kuiona nyumba fresh, changamoto ilikuwa imepakana na Kanisa, nikawa nahofia makelele.

Wakati nafikiria kufanya maamuzi dalali wapili akaniambia kuna nyumba hapa Makonde upande wa chini ambayo ni apartment ya watu 2, kule kodi ilikuwa 500k pia ila baada ya kupewa discount ikawa 450, hii ilikuwa ni ya vyumba vitatu pia, lakini ilikuwa mtaa mzuri na pametulia kuliko kule kwenye kanisa nilikokuwa na mashaka, nilipokwenda kuiona tulifunguliwa nyumba na jamaa aliyedai ni mtoto wa mwenye nyumba. nikauliza mwenye nyumba anaitwa nani, wakanitajia jina lake.

Basi nikamwambia dalali wapili hii nimeilewa naomba mawasiliano na mwenye nyumba tumalizane. Kwa dalali wa kwanza nikamwambia nimepata kwengine. Basi nikapewa mawasiliano ya mwenye nyumba tukaongea freshi, akatuma mkataba kwa soft copy nikaupitia nikampasia na ndugu yangu mwanasheria aangalie kama kila kitu sawa, akasema upo vizuri hamna shida.

Basi tukakubaliana niende leo kwenye nyumba hiyo wanipe mkataba ili tumalizane. Katika pita pita insta kwa page za madalali (nikiangalia labda naweza ona something better) nikakutana na ile nyumba ya pili lakini kodi ilikuwa 650k. Nikamtafuta dalali ambae amekuwa akinitafutia nyumba (nimekuwa nikitafuta nyumba kwa miezi sasa hola) nikamwambia naona mambo yenu ya kuongeza kodi, wakati mwenye nyumba kakubali kupangisha kwa 450, jamaa akasema mhh kwa bei hiyo ngoja niulize.

Kuuliza akarudi na majibu nyumba inapangishwa kwa 650k na ilikuwa 700k hapo ameshusha kidogo. Nikauliza mara mbili mbili, tunaongelea nyumba hii hii au nyingine? Embu niulizie mwenye nyumba anaitwa nani, nikaambiwa mwenye nyumba ni mwanamke na likatajwa jina lingine. Hapo siamini naona wanazingua tu. Nikasema fresh kesho si tunaenda kuonana kitajulikana.

Kesho (leo hii sasa) ikafika, mimi nikashindwa kwenda eneo la tukio, nikamwambia dalali atakuja dogo kwenye nyumba mumpe mkataba akimaliza mimi ntaweka pesa benki. Huku nyuma nikampanga dogo na yule dalali namekuwa akinitafutia nyumba warudi tena kwenye nyumba ile, wafike kwenye nyumba ile mapema zaidi na kuhakiki details za benki nilizopewa pamoja na majina ya mwenye nyumba, kama wasipokuta mtu waende kwa mjumbe.

Mwenye nyumba huku akanipigia simu, akasema dalali kaniambia utatuma mtu aje kukamilisha malipo, lakini mimi nimepata dharura, nimeenda mjini kufatilia kazi zangu na muda huo sitakuwepo. Cha kufanya wewe weka hela tu benki ubaki na slip, halafu jioni au kesho ntakupa mkataba.

Hapa nikaanza kuamini, hawa kweli watakuwa wapigaji. Nikawambia sawa hamna tatizo ntafanya malipo kwenye saa tano. Basi dogo akaenda na dalali yule anayenitafutia nyumba, kufika wakagonga wakafunguliwa mlango na kijana anaelinda hapo (nilipofika jana kijana hakuwepo niliambiwa katoka, na apartment nyingine mpangaji alikuwa ametoka pia), wakamwambia ndugu yangu anataka kupanga hapa sasa tumekuja kuhakiki kama taarifa hizi za benki alizopewa ni sahihi.

Mlinzi kupewa jina akasema mwenye nyumba sio huyo, wakatajiwa jina walilotaja madalali na kwamba mwenye nyumba ni mwanamke, na nyumba hiyo imeshalipiwa toka jana! Nikachoka! Nikamtafuta dalali, nikamwambia nimetuma dogo kucheki taarifa kama ni sahihi lakini kaishia kupewa jina la mtu mwingine. Dalali akasema aah kweli, basi nakuja hapo, nipo Bunju naomba mnisubiri, baada ya hapo akawa hapokei simu😂😂.

Baada ya hapo ikapita muda kidogo, akasema unajua hao madalali wengine wanataka kuniharibia ila mimi nimesamehe. Nikamwambia kama uongo kwanini umegoma kuja? Jamaa akasema mimi siwezi kupoteza muda wangu kuja huko, nimesamehe tu nyumba ziko nyingi, mwenye nyumba amekasirika sana biashara imekufa😂. Nikamwambia aliyetoa taarifa si dalali, ni kijana anaelinda hapa, we njoo hapa mi ntaingia gharama za kulipia usafiri wako uje uthibitishe wewe sio tapeli, akagoma. Kwahiyo ikaisha hivyo kwa huyu mpuuzi.

Baada ya kuona nimekosa hapa nikasema ngoja nirudi kwa dalali wa kwanza, huenda kelele si mbaya sana, nikamtuma dogo akaulize majirani kuhusu kelele za kanisa na nyumba za karibu. Dogo akaenda freshi na kunijulisha kelele si sana panakalika. Basi nikamtafuta mwenye nyumba, nikamwabia kama bado hujapangisha naomba naomba tuendelee tulipoishia.

Mzee akaijibu sawa, ila uwahi kulipia maana kesho kuna mtu anakuja kulipia, nikamwambia fresh, naomba account namba na jina la account, nikisubiri nae anipe details dogo akahakikishe kama alivyofanya kwenye ya kwanza. Picha likaanza jina la account likawa tofauti na jina la mwenye nyumba😂. Nikamwambia dogo mtindo ni ule ule, nenda kwenye nyumba ile kaulize, ukikosa mtu nenda kwa mjumbe.

Basi dogo akaenda, mbele ya nyumba hilo kuna duka la bidhaa za reja reja, kufika pale akamuuliza yule dada mwenye nyumba hapa anaitwa nani, ndio yule dada kusema nyumba ni ya kaka yake, na imeshapata mpangaji na kulipiwa, na kwamba kodi yake ilikuwa 800K (huku dalali alisema 500) nikachoka zaidi. Nikamwambia dogo ondoka hapo, hamna kitu.

Hivyo ndio ilvyokuwa, nikanusurika kupigwa mara mbili leo. Muwe makini katika kutafuta nyumba, aisee wapigaji ni wengi, na wanayokupanga yaani ni vigumu kushtukia.

Poleni kwa kuwachosha na gazeti, ikimsaidia hata mtu mmoja kuepuka kupigwa basi ni jambo jema. Kwa mliokuna na scam za aina nyingine wekeni hapa msaidie watu wasikutane na majanga kama haya.
 
Wakuu salama, niwape story kwa yaliyonikuta leo inaweza kumsaidia mtu.

Katika harakati za kutafuta nyumba maeneo ya Mbezi Beach nikakutana na madalali wawili kwa nyakati tofauti maeneo ya Makonde. Dalali mmoja akawa amenionesha nyumba stand alone ya vyumba 3 kwa kodi ya 500k kwa mwezi upande wa juu. Nikaenda kuiona nyumba fresh, changamoto ilikuwa imepakana na Kanisa, nikawa nahofia makelele.

Wakati nafikiria kufanya maamuzi dalali wapili akaniambia kuna nyumba hapa Makonde upande wa chini ambayo ni apartment ya watu 2, kule kodi ilikuwa 500k pia ila baada ya kupewa discount ikawa 450, hii ilikuwa ni ya vyumba vitatu pia, lakini ilikuwa mtaa mzuri na pametulia kuliko kule kwenye kanisa nilikokuwa na mashaka, nilipokwenda kuiona tulifunguliwa nyumba na jamaa aliyedai ni mtoto wa mwenye nyumba. nikauliza mwenye nyumba anaitwa nani, wakanitajia jina lake.

Basi nikamwambia dalali wapili hii nimeilewa naomba mawasiliano na mwenye nyumba tumalizane. Kwa dalali wa kwanza nikamwambia nimepata kwengine. Basi nikapewa mawasiliano ya mwenye nyumba tukaongea freshi, akatuma mkataba kwa soft copy nikaupitia nikampasia na ndugu yangu mwanasheria aangalie kama kila kitu sawa, akasema upo vizuri hamna shida.

Basi tukakubaliana niende leo kwenye nyumba hiyo wanipe mkataba ili tumalizane. Katika pita pita insta kwa page za madalali (nikiangalia labda naweza ona something better) nikakutana na ile nyumba ya pili lakini kodi ilikuwa 650k. Nikamtafuta dalali ambae amekuwa akinitafutia nyumba (nimekuwa nikitafuta nyumba kwa miezi sasa hola) nikamwambia naona mambo yenu ya kuongeza kodi, wakati mwenye nyumba kakubali kupangisha kwa 450, jamaa akasema mhh kwa bei hiyo ngoja niulize.

Kuuliza akarudi na majibu nyumba inapangishwa kwa 650k na ilikuwa 700k hapo ameshusha kidogo. Nikauliza mara mbili mbili, tunaongelea nyumba hii hii au nyingine? Embu niulizie mwenye nyumba anaitwa nani, nikaambiwa mwenye nyumba ni mwanamke na likatajwa jina lingine. Hapo siamini naona wanazingua tu. Nikasema fresh kesho si tunaenda kuonana kitajulikana.

Kesho (leo hii sasa) ikafika, mimi nikashindwa kwenda eneo la tukio, nikamwambia dalali atakuja dogo kwenye nyumba mumpe mkataba akimaliza mimi ntaweka pesa benki. Huku nyuma nikampanga dogo na yule dalali namekuwa akinitafutia nyumba warudi tena kwenye nyumba ile, wafike kwenye nyumba ile mapema zaidi na kuhakiki details za benki nilizopewa pamoja na majina ya mwenye nyumba, kama wasipokuta mtu waende kwa mjumbe.

Mwenye nyumba huku akanipigia simu, akasema dalali kaniambia utatuma mtu aje kukamilisha malipo, lakini mimi nimepata dharura, nimeenda mjini kufatilia kazi zangu na muda huo sitakuwepo. Cha kufanya wewe weka hela tu benki ubaki na slip, halafu jioni au kesho ntakupa mkataba.

Hapa nikaanza kuamini, hawa kweli watakuwa wapigaji. Nikawambia sawa hamna tatizo ntafanya malipo kwenye saa tano. Basi dogo akaenda na dalali yule anayenitafutia nyumba, kufika wakagonga wakafunguliwa mlango na kijana anaelinda hapo (nilipofika jana kijana hakuwepo niliambiwa katoka, na apartment nyingine mpangaji alikuwa ametoka pia), wakamwambia ndugu yangu anataka kupanga hapa sasa tumekuja kuhakiki kama taarifa hizi za benki alizopewa ni sahihi.

Mlinzi kupewa jina akasema mwenye nyumba sio huyo, wakatajiwa jina walilotaja madalali na kwamba mwenye nyumba ni mwanamke, na nyumba hiyo imeshalipiwa toka jana! Nikachoka! Nikamtafuta dalali, nikamwambia nimetuma dogo kucheki taarifa kama ni sahihi lakini kaishia kupewa jina la mtu mwingine. Dalali akasema aah kweli, basi nakuja hapo, nipo Bunju naomba mnisubiri, baada ya hapo akawa hapokei simu😂😂.

Bada ya hapo akasema unajua hao madalali wengine wanataka kuniharibia ila mimi nimesamehe. Nikamwambia kama uongo kwanini umegoma kuja? Jamaa akasema mimi siwezi kupoteza muda wangu kuja huko, nimesamehe tu nyumba ziko nyingi, mwenye nyumba amekasirika sana biashara imekufa😂. Nikamwambia aliyetoa taarifa si dalali, ni kijana anaelinda hapa, we njoo hapa mi ntaingia gharama za kulipia usafiri wako uje uthibitishe wewe sio tapeli, akagoma. Kwahiyo ikaisha hivyo kwa huyu mpuuzi.

Baada ya kuona nimekosa hapa nikasema ngoja nirudi kwa dalali wa kwanza, huenda kelele si mbaya sana, nikamtuma dogo akaulize majirani kuhusu kelele za kanisa na nyumba za karibu. Dogo akaenda freshi na kunijulisha kelele si sana panakalika. Basi nikamtafuta mwenye nyumba, nikamwabia kama bado hujapangisha naomba naomba tuendelee tulipoishia.

Mzee akaijibu sawa, ila uwahi kulipia maana kesho kuna mtu anakuja kulipia, nikamwambia fresh, naomba account namba na jina la account, nikisubiri nae anipe details dogo akahakikishe kama alivyofanya kwenye ya kwanza. Picha likaanza jina la account likawa tofauti na jina la mwenye nyumba😂. Nikamwambia dogo mtindo ni ule ule, nenda kwenye nyumba ile kaulize, ukikosa mtu nenda kwa mjumbe.

Basi dogo akaenda, mbele ya nyumba hilo kuna duka la bidhaa za reja reja, kufika pale akamuuliza yule dada mwenye nyumba hapa anaitwa nani, ndio yule dada kusema nyumba ni ya kaka yake, na imeshapata mpangaji na kulipiwa, na kwamba kodi yake ilikuwa 800K (huku dalali alisema 500) nikachoka zaidi. Nikamwambia dogo ondoka hapo, hamna kitu.

Hivyo ndio ilvyokuwa, nikanusurika kupigwa mara mbili leo. Muwe makini katika kutafuta nyumba, aisee wapigaji ni wengi, na wanayokupanga yaani ni vigumu kushtukia.

Poleni kwa kuwachosha na gazeti, ikimsaidia hata mtu mmoja kuepuka kupigwa basi ni jambo jema. Kwa mliokuna na scam za aina nyingine wekeni hapa msaidie watu wasikutane na majanga kama haya.
JF kisima cha hekima. Hakika wezi wamezidi
 
Wakuu salama, niwape story kwa yaliyonikuta leo inaweza kumsaidia mtu.

Katika harakati za kutafuta nyumba maeneo ya Mbezi Beach nikakutana na madalali wawili kwa nyakati tofauti maeneo ya Makonde. Dalali mmoja akawa amenionesha nyumba stand alone ya vyumba 3 kwa kodi ya 500k kwa mwezi upande wa juu. Nikaenda kuiona nyumba fresh, changamoto ilikuwa imepakana na Kanisa, nikawa nahofia makelele.

Wakati nafikiria kufanya maamuzi dalali wapili akaniambia kuna nyumba hapa Makonde upande wa chini ambayo ni apartment ya watu 2, kule kodi ilikuwa 500k pia ila baada ya kupewa discount ikawa 450, hii ilikuwa ni ya vyumba vitatu pia, lakini ilikuwa mtaa mzuri na pametulia kuliko kule kwenye kanisa nilikokuwa na mashaka, nilipokwenda kuiona tulifunguliwa nyumba na jamaa aliyedai ni mtoto wa mwenye nyumba. nikauliza mwenye nyumba anaitwa nani, wakanitajia jina lake.

Basi nikamwambia dalali wapili hii nimeilewa naomba mawasiliano na mwenye nyumba tumalizane. Kwa dalali wa kwanza nikamwambia nimepata kwengine. Basi nikapewa mawasiliano ya mwenye nyumba tukaongea freshi, akatuma mkataba kwa soft copy nikaupitia nikampasia na ndugu yangu mwanasheria aangalie kama kila kitu sawa, akasema upo vizuri hamna shida.

Basi tukakubaliana niende leo kwenye nyumba hiyo wanipe mkataba ili tumalizane. Katika pita pita insta kwa page za madalali (nikiangalia labda naweza ona something better) nikakutana na ile nyumba ya pili lakini kodi ilikuwa 650k. Nikamtafuta dalali ambae amekuwa akinitafutia nyumba (nimekuwa nikitafuta nyumba kwa miezi sasa hola) nikamwambia naona mambo yenu ya kuongeza kodi, wakati mwenye nyumba kakubali kupangisha kwa 450, jamaa akasema mhh kwa bei hiyo ngoja niulize.

Kuuliza akarudi na majibu nyumba inapangishwa kwa 650k na ilikuwa 700k hapo ameshusha kidogo. Nikauliza mara mbili mbili, tunaongelea nyumba hii hii au nyingine? Embu niulizie mwenye nyumba anaitwa nani, nikaambiwa mwenye nyumba ni mwanamke na likatajwa jina lingine. Hapo siamini naona wanazingua tu. Nikasema fresh kesho si tunaenda kuonana kitajulikana.

Kesho (leo hii sasa) ikafika, mimi nikashindwa kwenda eneo la tukio, nikamwambia dalali atakuja dogo kwenye nyumba mumpe mkataba akimaliza mimi ntaweka pesa benki. Huku nyuma nikampanga dogo na yule dalali namekuwa akinitafutia nyumba warudi tena kwenye nyumba ile, wafike kwenye nyumba ile mapema zaidi na kuhakiki details za benki nilizopewa pamoja na majina ya mwenye nyumba, kama wasipokuta mtu waende kwa mjumbe.

Mwenye nyumba huku akanipigia simu, akasema dalali kaniambia utatuma mtu aje kukamilisha malipo, lakini mimi nimepata dharura, nimeenda mjini kufatilia kazi zangu na muda huo sitakuwepo. Cha kufanya wewe weka hela tu benki ubaki na slip, halafu jioni au kesho ntakupa mkataba.

Hapa nikaanza kuamini, hawa kweli watakuwa wapigaji. Nikawambia sawa hamna tatizo ntafanya malipo kwenye saa tano. Basi dogo akaenda na dalali yule anayenitafutia nyumba, kufika wakagonga wakafunguliwa mlango na kijana anaelinda hapo (nilipofika jana kijana hakuwepo niliambiwa katoka, na apartment nyingine mpangaji alikuwa ametoka pia), wakamwambia ndugu yangu anataka kupanga hapa sasa tumekuja kuhakiki kama taarifa hizi za benki alizopewa ni sahihi.

Mlinzi kupewa jina akasema mwenye nyumba sio huyo, wakatajiwa jina walilotaja madalali na kwamba mwenye nyumba ni mwanamke, na nyumba hiyo imeshalipiwa toka jana! Nikachoka! Nikamtafuta dalali, nikamwambia nimetuma dogo kucheki taarifa kama ni sahihi lakini kaishia kupewa jina la mtu mwingine. Dalali akasema aah kweli, basi nakuja hapo, nipo Bunju naomba mnisubiri, baada ya hapo akawa hapokei simu.

Baada ya hapo ikapita muda kidogo, akasema unajua hao madalali wengine wanataka kuniharibia ila mimi nimesamehe. Nikamwambia kama uongo kwanini umegoma kuja? Jamaa akasema mimi siwezi kupoteza muda wangu kuja huko, nimesamehe tu nyumba ziko nyingi, mwenye nyumba amekasirika sana biashara imekufa. Nikamwambia aliyetoa taarifa si dalali, ni kijana anaelinda hapa, we njoo hapa mi ntaingia gharama za kulipia usafiri wako uje uthibitishe wewe sio tapeli, akagoma. Kwahiyo ikaisha hivyo kwa huyu mpuuzi.

Baada ya kuona nimekosa hapa nikasema ngoja nirudi kwa dalali wa kwanza, huenda kelele si mbaya sana, nikamtuma dogo akaulize majirani kuhusu kelele za kanisa na nyumba za karibu. Dogo akaenda freshi na kunijulisha kelele si sana panakalika. Basi nikamtafuta mwenye nyumba, nikamwabia kama bado hujapangisha naomba naomba tuendelee tulipoishia.

Mzee akaijibu sawa, ila uwahi kulipia maana kesho kuna mtu anakuja kulipia, nikamwambia fresh, naomba account namba na jina la account, nikisubiri nae anipe details dogo akahakikishe kama alivyofanya kwenye ya kwanza. Picha likaanza jina la account likawa tofauti na jina la mwenye nyumba. Nikamwambia dogo mtindo ni ule ule, nenda kwenye nyumba ile kaulize, ukikosa mtu nenda kwa mjumbe.

Basi dogo akaenda, mbele ya nyumba hilo kuna duka la bidhaa za reja reja, kufika pale akamuuliza yule dada mwenye nyumba hapa anaitwa nani, ndio yule dada kusema nyumba ni ya kaka yake, na imeshapata mpangaji na kulipiwa, na kwamba kodi yake ilikuwa 800K (huku dalali alisema 500) nikachoka zaidi. Nikamwambia dogo ondoka hapo, hamna kitu.

Hivyo ndio ilvyokuwa, nikanusurika kupigwa mara mbili leo. Muwe makini katika kutafuta nyumba, aisee wapigaji ni wengi, na wanayokupanga yaani ni vigumu kushtukia.

Poleni kwa kuwachosha na gazeti, ikimsaidia hata mtu mmoja kuepuka kupigwa basi ni jambo jema. Kwa mliokuna na scam za aina nyingine wekeni hapa msaidie watu wasikutane na majanga kama haya.
Issue za madalali mizinguo mingi ndio maana kuna watu awahitaji kabisa mambo ya udalali kwenye nyumba au vitu vyao

wengi matapeli hapa mwanza usagara wameuza nyumba wakamtapeli mzee mwenye nyumba yake hela hakupata ata senti shoo yake sasa waliipata sawa sawa walikuwa wanne waliisha mmoja mmoja


wote chini kila mmoja kwa muda wake . Wakuu hadi ikafika mahara madalali wakaiogopa kazi yao mtu unamjuwa kabisa ni dalali ukimfata anakwambia mi sio dalali
 
Wakuu salama, niwape story kwa yaliyonikuta leo inaweza kumsaidia mtu.

Katika harakati za kutafuta nyumba maeneo ya Mbezi Beach nikakutana na madalali wawili kwa nyakati tofauti maeneo ya Makonde. Dalali mmoja akawa amenionesha nyumba stand alone ya vyumba 3 kwa kodi ya 500k kwa mwezi upande wa juu. Nikaenda kuiona nyumba fresh, changamoto ilikuwa imepakana na Kanisa, nikawa nahofia makelele.

Wakati nafikiria kufanya maamuzi dalali wapili akaniambia kuna nyumba hapa Makonde upande wa chini ambayo ni apartment ya watu 2, kule kodi ilikuwa 500k pia ila baada ya kupewa discount ikawa 450, hii ilikuwa ni ya vyumba vitatu pia, lakini ilikuwa mtaa mzuri na pametulia kuliko kule kwenye kanisa nilikokuwa na mashaka, nilipokwenda kuiona tulifunguliwa nyumba na jamaa aliyedai ni mtoto wa mwenye nyumba. nikauliza mwenye nyumba anaitwa nani, wakanitajia jina lake.

Basi nikamwambia dalali wapili hii nimeilewa naomba mawasiliano na mwenye nyumba tumalizane. Kwa dalali wa kwanza nikamwambia nimepata kwengine. Basi nikapewa mawasiliano ya mwenye nyumba tukaongea freshi, akatuma mkataba kwa soft copy nikaupitia nikampasia na ndugu yangu mwanasheria aangalie kama kila kitu sawa, akasema upo vizuri hamna shida.

Basi tukakubaliana niende leo kwenye nyumba hiyo wanipe mkataba ili tumalizane. Katika pita pita insta kwa page za madalali (nikiangalia labda naweza ona something better) nikakutana na ile nyumba ya pili lakini kodi ilikuwa 650k. Nikamtafuta dalali ambae amekuwa akinitafutia nyumba (nimekuwa nikitafuta nyumba kwa miezi sasa hola) nikamwambia naona mambo yenu ya kuongeza kodi, wakati mwenye nyumba kakubali kupangisha kwa 450, jamaa akasema mhh kwa bei hiyo ngoja niulize.

Kuuliza akarudi na majibu nyumba inapangishwa kwa 650k na ilikuwa 700k hapo ameshusha kidogo. Nikauliza mara mbili mbili, tunaongelea nyumba hii hii au nyingine? Embu niulizie mwenye nyumba anaitwa nani, nikaambiwa mwenye nyumba ni mwanamke na likatajwa jina lingine. Hapo siamini naona wanazingua tu. Nikasema fresh kesho si tunaenda kuonana kitajulikana.

Kesho (leo hii sasa) ikafika, mimi nikashindwa kwenda eneo la tukio, nikamwambia dalali atakuja dogo kwenye nyumba mumpe mkataba akimaliza mimi ntaweka pesa benki. Huku nyuma nikampanga dogo na yule dalali namekuwa akinitafutia nyumba warudi tena kwenye nyumba ile, wafike kwenye nyumba ile mapema zaidi na kuhakiki details za benki nilizopewa pamoja na majina ya mwenye nyumba, kama wasipokuta mtu waende kwa mjumbe.

Mwenye nyumba huku akanipigia simu, akasema dalali kaniambia utatuma mtu aje kukamilisha malipo, lakini mimi nimepata dharura, nimeenda mjini kufatilia kazi zangu na muda huo sitakuwepo. Cha kufanya wewe weka hela tu benki ubaki na slip, halafu jioni au kesho ntakupa mkataba.

Hapa nikaanza kuamini, hawa kweli watakuwa wapigaji. Nikawambia sawa hamna tatizo ntafanya malipo kwenye saa tano. Basi dogo akaenda na dalali yule anayenitafutia nyumba, kufika wakagonga wakafunguliwa mlango na kijana anaelinda hapo (nilipofika jana kijana hakuwepo niliambiwa katoka, na apartment nyingine mpangaji alikuwa ametoka pia), wakamwambia ndugu yangu anataka kupanga hapa sasa tumekuja kuhakiki kama taarifa hizi za benki alizopewa ni sahihi.

Mlinzi kupewa jina akasema mwenye nyumba sio huyo, wakatajiwa jina walilotaja madalali na kwamba mwenye nyumba ni mwanamke, na nyumba hiyo imeshalipiwa toka jana! Nikachoka! Nikamtafuta dalali, nikamwambia nimetuma dogo kucheki taarifa kama ni sahihi lakini kaishia kupewa jina la mtu mwingine. Dalali akasema aah kweli, basi nakuja hapo, nipo Bunju naomba mnisubiri, baada ya hapo akawa hapokei simu.

Baada ya hapo ikapita muda kidogo, akasema unajua hao madalali wengine wanataka kuniharibia ila mimi nimesamehe. Nikamwambia kama uongo kwanini umegoma kuja? Jamaa akasema mimi siwezi kupoteza muda wangu kuja huko, nimesamehe tu nyumba ziko nyingi, mwenye nyumba amekasirika sana biashara imekufa. Nikamwambia aliyetoa taarifa si dalali, ni kijana anaelinda hapa, we njoo hapa mi ntaingia gharama za kulipia usafiri wako uje uthibitishe wewe sio tapeli, akagoma. Kwahiyo ikaisha hivyo kwa huyu mpuuzi.

Baada ya kuona nimekosa hapa nikasema ngoja nirudi kwa dalali wa kwanza, huenda kelele si mbaya sana, nikamtuma dogo akaulize majirani kuhusu kelele za kanisa na nyumba za karibu. Dogo akaenda freshi na kunijulisha kelele si sana panakalika. Basi nikamtafuta mwenye nyumba, nikamwabia kama bado hujapangisha naomba naomba tuendelee tulipoishia.

Mzee akaijibu sawa, ila uwahi kulipia maana kesho kuna mtu anakuja kulipia, nikamwambia fresh, naomba account namba na jina la account, nikisubiri nae anipe details dogo akahakikishe kama alivyofanya kwenye ya kwanza. Picha likaanza jina la account likawa tofauti na jina la mwenye nyumba. Nikamwambia dogo mtindo ni ule ule, nenda kwenye nyumba ile kaulize, ukikosa mtu nenda kwa mjumbe.

Basi dogo akaenda, mbele ya nyumba hilo kuna duka la bidhaa za reja reja, kufika pale akamuuliza yule dada mwenye nyumba hapa anaitwa nani, ndio yule dada kusema nyumba ni ya kaka yake, na imeshapata mpangaji na kulipiwa, na kwamba kodi yake ilikuwa 800K (huku dalali alisema 500) nikachoka zaidi. Nikamwambia dogo ondoka hapo, hamna kitu.

Hivyo ndio ilvyokuwa, nikanusurika kupigwa mara mbili leo. Muwe makini katika kutafuta nyumba, aisee wapigaji ni wengi, na wanayokupanga yaani ni vigumu kushtukia.

Poleni kwa kuwachosha na gazeti, ikimsaidia hata mtu mmoja kuepuka kupigwa basi ni jambo jema. Kwa mliokuna na scam za aina nyingine wekeni hapa msaidie watu wasikutane na majanga kama haya.
Pole San mkuu
 
Back
Top Bottom