Leo nimekutana na Waziri wa fedha Saada Mkuya Salum

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,932
31,178
Heshima sana wanajamvi,

Leo muda wa saa saba na nusu mchana nimekutana na waziri wa fedha Bi Saada Mkuya Salum hapa mjini Arusha.Najua wengi mtakata kwakuwa mnamwona kwenye luninga zetu akibwabwaja huko Idodomya katika lile jumba lililoja kila aina ya vituko.

Ni hivi wakati najiandaa kupata chakula cha mchana ghafla wanaingia vijana wanne wa TRA wakiongozana na askari polisi mwenye v mbili nje ya ofisi yangu kuna CCCTV nawaona askari wengine wawili wenye silaha wakijiweka tayari kwa lolote.Nawapokea bila ajizi nawauliza kulikoni kijana mmoja ananiwahi kwa kuniomba Z report nampatia anaikagua kama dakika 5 ananirejeshea baada ya kuirekodi katika daftari lake na kuondoka ?.

Nabaki nikijiuliza maswali mawili matatu hivi Z report siku hizi inakaguliwa na bunduki ?.Kuna mfanyabiashara aliyesajili VRN atakayekaidi kutoa Z report ili iweje ?.Nadhani matumizi ya askari wetu yafaa yaangaliwe upya.Wakati bado najiuliza maswali mengi naikumbuka hotuba ya waziri wa fedha wakati akiijibu michango ya waheshimiwa wabunge.

Nawasilisha.
 
Mkuu Victor wa happy haujaelewa nini ?.Ngoja nikutafunie zaidi na zaidi ni hivi waziri wetu wa fedha wakati akihitimisha mjadala wa bajeti yake alikuwa mkali sana hawa kwa wafanyabiashara wasiopenda kulipa kodi na kaenda mbali kwa kuahidi kupambana nao.Leo nimeona utekelezaji wa hotuba yake,kasi ya vijana wa TRA wakisaidiana na polisi kufuatilia matumizi ya EFD na ukaguzi wa Z report sijawahi kuhushuhudia hata siku moja nadhani huu ni mwanzo mzuri.

Tulipe kodi kwa maendeleo ya taifa letu ingawa matumizi ya kodi zetu ni kitendawili kingine.

Sijaelewa
 
Last edited by a moderator:
Nimekupata sasa mkuu

Wafanyabiashara safari hii mtauza na TRA wakiwa pembeni
 
mbona hueleweki umekutana na saada salum arusha ,mara tena polisi wameingia sijakuelewa mkuu. ukipewa mtihani utafeli una mbwembwe sana
 
Mkuu Saada Mkuya kaanza kuonekana hata kabla mwaka mpya wa bajeti haujaanza?
 
Hata mimi ni div, 5. sijakuelewa kabisa.

Hivi Waziri ni jukumu lake kuja dukani kwako kukukagua kama unalipa kodi au lah, maana kama hadi yeye anafikia hatua ya kuja kwako, na yule aliyestahili kuja kwako kwa kazi hiyo anafanya nini, na kama hajaja kachukuliwa hatua gani, huyo Waziri atatembea katika maduka mangapi nchi nzima, mbona mimi nipo hapa Nyarugusi lakini simuoni Waziri kuja kunikagua.

Ushauri wa bure, ili nami Division 5 nielewe na pia kumpongeza, ajitahidi kufanya system ifanye kazi, na sio yeye kuzunguka katikz maduka
 
Mkuu Saada Mkuya kaanza kuonekana hata kabla mwaka mpya wa bajeti haujaanza?
Ukiona hivyo ujue serikali haina pesa, na bunge la katiba karibia litaanza...watakomaje? Na sisi magari tunapaki sijui watamkamata nani tena?
 
Back
Top Bottom