Leo ni siku ya mwisho kurejesha fomu za national id

Gama

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
13,266
4,716
Wana JF, leo ni siku ya mwisho kwa watumishi wa serikali na taasisi zake kurudisha fomu za kuomba vitambulisho vya uraia, leo maofisa wengi wa serikali wako katika misururu mirefu ya kurudisha fomu hizo.
 
Watanzania kwa kupenda kuwa wa mwisho acha kabisa tangia wapewe walikuwa wapi?
 
Mbona mikoani hatujapewa hizo fomu, au ni kwa ajili ya watumishi wanaoishi DAR tu!?
 
Wana JF, leo ni siku ya mwisho kwa watumishi wa serikali na taasisi zake kurudisha fomu za kuomba vitambulisho vya uraia, leo maofisa wengi wa serikali wako katika misururu mirefu ya kurudisha fomu hizo.
Na sisi tusio watumishi wa Serikali,hatustahili kupata hivyo vitambulisho?
 
Mbona mikoani hatujapewa hizo fomu, au ni kwa ajili ya watumishi wanaoishi DAR tu!?
Si ndo hapo,nashangaa au watumishi wa serikali wapo dar tu,maana kila dar dar,utafikiri dar ndo tanzania pekee,nchi kubwaa hii jamaani,na idadi ya watu waliopo ni hata theluthi haifiki
 
Je mtu asiporudisha itakuwaje? hakutakuwa na nafasi nyingine? au ndiyo atakuwa siyo raia?
 
wewe unajisemea tuu ungejua watumishi wenyewe tunavyotaabika kupata cheti cha kuzaliwa ungetulia tu. Mtumishi amezaliwa miaka ya 50 na ushee kabla ya uhuru na alizaliwa kwa mkunga wa jadi kusikokuwa na hati ya kizazi.

Hata hviyo mtumishi huyu ana PASI YA KUSAFIRIA KAMA RAIA WA TANZANIA lakini anaambiwa atoe elfu 20 apewe cheti cha kuzaliwa ili apate National ID.

Yaani hata sielewi hii PASI iliyotolewa na JAMHURI YA MUUNGANO WA TZ inasaidia nini ikiwa haitambuliki kama utambulisho wa MTZ.haitoshi kumpa mtu national ID? Hizi elfu 20 za cheti cha kuzaliwa ni za nini?

Ahaa anyway WATZ tumezoea kuburuzwa na huwa tunakubali tuu bila kuhoji.
 
Sio watumishi wote wa UMMA mkuu. Kwa wamikoani ni jumatatu. Form sio ngumu hivyo, tunapenda kucomplicate mambo.Wewe mpaka leo huna cheti cha kuzaliwa, nashangaa sanaa
 
Na sisi wafanya biashara zamu yetu lini? au cc hatutambuliwi? Kwanza hii issue ya vitamburisho ikoje wajameni??
 
Hizi taasisi unadhani zitajiendeshaje kama wewe unaona unaonewa kuchanhia Tshs 20,000?
wewe unajisemea tuu ungejua watumishi wenyewe tunavyotaabika kupata cheti cha kuzaliwa ungetulia tu. Mtumishi amezaliwa miaka ya 50 na ushee kabla ya uhuru na alizaliwa kwa mkunga wa jadi kusikokuwa na hati ya kizazi.

Hata hviyo mtumishi huyu ana PASI YA KUSAFIRIA KAMA RAIA WA TANZANIA lakini anaambiwa atoe elfu 20 apewe cheti cha kuzaliwa ili apate National ID.

Yaani hata sielewi hii PASI iliyotolewa na JAMHURI YA MUUNGANO WA TZ inasaidia nini ikiwa haitambuliki kama utambulisho wa MTZ.haitoshi kumpa mtu national ID? Hizi elfu 20 za cheti cha kuzaliwa ni za nini?

Ahaa anyway WATZ tumezoea kuburuzwa na huwa tunakubali tuu bila kuhoji.
 
Si kosa lao tatizo unakuta form zimeandikwa kiingereza wakati lugha yetu ni kiswahili
 
Back
Top Bottom