Land Cruiser Prado - msaada

Jafar

JF-Expert Member
Nov 3, 2006
1,136
52
Naomba kuuliza.
Kuna Land Cruiser Prado mbili zote za 2001, zote ni automatic, 90 series, rangi tofauti (nyeupe na silver), kilometer moja ni 65,000 na nyingine 88,000, lakini moja ni Petrol Engine 2.7 L na nyingine ni Diesel Engine 3.0 L. Kitaalamu ipi ni gari nzuri ya kununua? Petrol au Diesel katika hizo mbili? Ukizingatia kwamba matumizi yake ni bongoland.
 
Mkuu
Mimi binafisi ningekushauri ununue ile inayotumuia petrol,kutokana na general service za mara kwa mara.
Mafundi watakuwa wanafahamu, services za gari aina ya petrol si sawa na gari aina ya diesel ukiingia kiundani kwenye combusition chamber inayotoa energy na kugenerate motion kwa upande wa petrol na diesel nitofauti.
Nunua petrol, ninauzoefu ninamiliki gari 2 za petrol, sipati tabu ya kubadilisha sijui plugs sijui pumps sijaona.
Soma haraka hii habari, hawa jamaa wa jamii forum maoni yangu huwa wanayatoa haraka, ingawa sijajua kwanini.
 
vizuri ukapata ushauri wa kitaalamu mi natumia ya diesel si mbaya coz naenda nayo vizuri kwa mwaka wa pili sasa na wataalam wananisaidia sana pale DIZOTECH PG RD labda ujaribu kucheki nao wanaweza kushauri nini kinakufaa zaidi.
 
Naomba kuuliza.
Kuna Land Cruiser Prado mbili zote za 2001, zote ni automatic, 90 series, rangi tofauti (nyeupe na silver), kilometer moja ni 65,000 na nyingine 88,000, lakini moja ni Petrol Engine 2.7 L na nyingine ni Diesel Engine 3.0 L. Kitaalamu ipi ni gari nzuri ya kununua? Petrol au Diesel katika hizo mbili? Ukizingatia kwamba matumizi yake ni bongoland.
Well,

Make ni moja lakini moja ni gasoline na nyingine Diesel.

Kabla mimi sijaenda mbali, hizo readings za Odometer hujatufahamisha ya 65k ni ya la Diesel au Gasoline.
 
Sure, nunua ya Petrol service zake ni cheaper than that of diesel.

Bajameni,

Mbona tunamshauri mwenzetu kwa upande wa service tu hatuangalii consumption ya mafuta kwani nafahamu petrol inatumika haraka zaidi ya diesel? Na mafuta kama anatumia kila siku hilo gari, basi ndio itakuwa gharama yake kubwa zaidi ya service ambayo inafanyika labda kila baada ya gari kutembea kilometer kadhaa.

Mshaurini kwa kuangalia pande zote mbili za shillingi.

Tiba
 
Mkuu pia hujatuambia indicative prices zake zikoje, ili pia tuziweke kwenye equation?
 
Naomba kuuliza.
Kuna Land Cruiser Prado mbili zote za 2001, zote ni automatic, 90 series, rangi tofauti (nyeupe na silver), kilometer moja ni 65,000 na nyingine 88,000, lakini moja ni Petrol Engine 2.7 L na nyingine ni Diesel Engine 3.0 L. Kitaalamu ipi ni gari nzuri ya kununua? Petrol au Diesel katika hizo mbili? Ukizingatia kwamba matumizi yake ni bongoland.


Ok, mimi nakushauri kitaalam na kiuzoefu. Nimeshazitumia zote mbili diesel na petrol. Najua umetoa tukushauri kwa kuangalia utaalam zaidi na siyo bei kwani hujatueleza bei gani yanauzwa, Lakini kwa uzoefu wangu najua kununua hiyo ya petrol ni cheap kuliko hiyo ya diesel hapo huwezi kubisha.

Petrol gari service zake ni rahisi siyo gharama sana ukilinganisha na diesel, Kwa mfano Gari ya Diesel Utatakiwa ubadilishe Diesel Filter, Oil Filter na kumwaga oil na Oil filter ya hiyo Prado kama engine ni 1KZ original inauzwa 50,000/= Tsh pale Dar kwenye maduka maalum, lakini zipo fake zinauzwa 5,000/=Tsh na ukizubaa unabambikwa ya 5,000/= kwa 50,000/= , Diesel filter ni 30,000/= original

Upande wa petrol service yake ni kubadilisha Oil filter na kumwaga
oil basi. Na Oil filter ya petrol ni 15,000/= only

Lkini service zisikupe maamuzi maana tunafanya service kila baada ya 5000km, kama umeweka original parts ambayo kama si mtembezi sana unaweza ukafanya service mara mbili kwa mwaka.

Fuel consumption: Hapa ndipo uwe makini, Petrol tena hiyo ya cc 2700 inakamua kishenzi, Unaweza ukajikuta unatembea 5Km per Lit., lakini hiyo ya Disel cc 3000 najua ni turbo charger, ukiwa masafa marefu huwa haili kabisa mafuta, kwani ukitembea kuanzia Km 70 - 100 kwa Saa turbo inafunguka then inatumia zaidi air than fuel.

Diesel engine pia ina nguvu zaidi hata kwenye milima inapanda kama unalia, na kwenye matope ni bora sana.

Ushauri wangu nunua ya diesel hata kama inauzwa gharama, na ndiyo maana utaona diesel gari zinauzwa gharama zaidi.

Ni hayo tu mzeeeeeee maamuzi uanyo wewe.
 
nakushukuru sana Mpenda nchi, kwa ushauri wako, huo ushauri na sisi umetusaidia kwa kiwango kikubwa tu.
 
Mkuu Gari Petroli ni nzuri zaidi kwa gari ndogo ambayo injini yake isizidi cc 2000,but for 4x4 with cc 2700 itakuua kwenye kuliendesha,ni kweli service za Diesel ziko juu zaidi ya gari ya petrol,but service huwa inafanyika mara chache zaidi kuliko kujaza mafuta kwenye tank,mie nakushauri chukua hiyo ya diesel,nawakilisha!!!!
 
Mkuu Gari Petroli ni nzuri zaidi kwa gari ndogo ambayo injini yake isizidi cc 2000,but for 4x4 with cc 2700 itakuua kwenye kuliendesha,ni kweli service za Diesel ziko juu zaidi ya gari ya petrol,but service huwa inafanyika mara chache zaidi kuliko kujaza mafuta kwenye tank,mie nakushauri chukua hiyo ya diesel,nawakilisha!!!!


Kwa huku ughaibuni gari ya dieseli ni ghali kwani walipia mazingira na dseli ni ghali pia alafu diesel zao zimeoshwa mara bili na hazitoi moshi kama mafuta ya diseli zetu za bongo. service ya disel injini (full service) badilisha mpaka piston ring,cons, na kuchonga pengine, au vyombo vyote ubadilishe siyo chini ya shs milion tano hadi sita ya bongo and it will last eight to ten years. zingatia disel yetu ni gredi ambayo ni haribifu then service yake lazima iwe ya kibabe.

Petrol ina nguvu sana na ni nyepesi kwa hiyo speed ni haraka mno service yake kama unavyofanya ya disel in 15 years guarantee. Kwa gari zote kama hazifanyi kazi nzito sana na inategemea kama umenunua mpya kila gari muda wa huduma zake ni jinsi nilivyoeleza hapo juu.

Recommendation petroli man.
 
Bei sio tatizo na ndio maana sikuitaja. Lakini Prado ya Diesel ni more expensive. Prado ya petroli ni US$ 22,000 na ya Diesel ni US$30,000.
 
Thanks for all who contributed/responded to my request. I have leanrt a lot through your experiences and knowledge.

Through, this I have changed my earlier thinking and decided to take a Diesel one.
Thanks guys for your time.
 
Thanks for all who contributed/responded to my request. I have leanrt a lot through your experiences and knowledge.

Through, this I have changed my earlier thinking and decided to take a Diesel one.
Thanks guys for your time.



Poa mkuu, lakini pia isiste kuja kutupa updates za jinsi hiyo ya Diesel inavoendelea, labda wengine Mungu akijaalia tutafika kununua...
 
Back
Top Bottom