Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,174
Kweli aliniapia ya kuwa yeye sasa basi imetosha kabisa!
Kweli aliniapia ya kuwa yeye sasa hataki tena hata iweje!
Kweli aliniapia ya kuwa yeye sasa siyo teja wa asali tena!
Kweli aliniapia ya kuwa yeye sasa siyo mshupaliaji wake!
Lakini hii TRUVADA sasa yamtia kiwewe na kumletea kifaduro.
Yawaje kweli yote aliyoniapia kuyaona kazi bure?
Yawaje kweli yote aliyoniapia aone ulikuwa ni utani tu?
Yawaje kweli hata soo asinionee pale anafarijiwa na TRUVADA?
Yawaje kweli muarobaini huo sasa aone ndiyo jibu la tamaa zake?
Lakini hii TRUVADA sasa yamtia kiwewe na kumletea kifaduro.
Ngonjera anazonipa kweli kichwani haziingii hata chembe.
Ngonjera anazotamba nazo bado kwangu ni upuuzi mtupu.
Ngonjera anazojivunia bado hazina uthibitisho hata chembe.
Ngonjera zake zadai eti amechoka kuwakiana nao tamaa kila kuchako.
Lakini hii TRUVADA sasa yamtia kiwewe na kumletea kifaduro.
TRUVADA kwani ni kitu gani kama siyo kinga ya nusunusu?
TRUVADA ni nini kama bado haiko majaribioni tu nawe ni jaribio tu?
TRUVADA ni nini kama siyo chambo ya kukutia majaribuni nawe unaswe?
TRUVADA ni nini kama haiwezi kukulinda kwa asilimia zote kabisa?
Lakini hii TRUVADA sasa yamtia kiwewe na kumletea kifaduro.