SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,244
- 4,258
Enyi vijana wangu wa BAVICHA!
Poleni sana na hongereni kwa kazi nzuri mlofanya kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.
Mlidharauliwa sana na kubezwa kwa kuitwa kwamba nyie ni wanywa viroba msiojua mbele, nyuma au pembeni. Hasa hapa JF ikiletwa thread yenye kukosoa upande wa pili wachangiaji wanaokunywa maji ya kijani huchangia kwa kusema "mawazo ya kibavicha hayo" au "viroba vya bavicha hivyo"
Lakini hao wanywa maji ya kijani, kwa kupoteza ufahamu wao kama ilivyo kawaida yao hawakufahamu hata kidogo kwamba ninyi ni jeshi kubwa la wapiga kura lenye uwezo wa kubadili serikali ya nchi hii.Wao wamebaki kusema wanywa viroba hao.Lililotokea kwenye chaguzi za serikali za mitaa limewapa kizunguzungu kiasi hawalikumbuki neno 'viroba' tena.
Wanalolifahamu ni 'tutaangalia tulipojikwaa ili tujisahihishe' Hawajui kuwa walianza kujikwaa tangu hilo kundi lilipozaliwa 1977.
Sasa vijana wangu wapendwa nawaomba hivi:msisahau kujiandikisha kwenye uboreshaji wa daftari la wapiga kura katika sehemu unayoishi, ili mwakani 2015 uwe na kibali cha kuwachinjia mbali hii mijitu inayoita wenzao 'wanywa viroba'
Ni hayo tu kwa leo vijana wangu, sina mengi.
Poleni sana na hongereni kwa kazi nzuri mlofanya kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.
Mlidharauliwa sana na kubezwa kwa kuitwa kwamba nyie ni wanywa viroba msiojua mbele, nyuma au pembeni. Hasa hapa JF ikiletwa thread yenye kukosoa upande wa pili wachangiaji wanaokunywa maji ya kijani huchangia kwa kusema "mawazo ya kibavicha hayo" au "viroba vya bavicha hivyo"
Lakini hao wanywa maji ya kijani, kwa kupoteza ufahamu wao kama ilivyo kawaida yao hawakufahamu hata kidogo kwamba ninyi ni jeshi kubwa la wapiga kura lenye uwezo wa kubadili serikali ya nchi hii.Wao wamebaki kusema wanywa viroba hao.Lililotokea kwenye chaguzi za serikali za mitaa limewapa kizunguzungu kiasi hawalikumbuki neno 'viroba' tena.
Wanalolifahamu ni 'tutaangalia tulipojikwaa ili tujisahihishe' Hawajui kuwa walianza kujikwaa tangu hilo kundi lilipozaliwa 1977.
Sasa vijana wangu wapendwa nawaomba hivi:msisahau kujiandikisha kwenye uboreshaji wa daftari la wapiga kura katika sehemu unayoishi, ili mwakani 2015 uwe na kibali cha kuwachinjia mbali hii mijitu inayoita wenzao 'wanywa viroba'
Ni hayo tu kwa leo vijana wangu, sina mengi.