Mpaka Kieleweke
JF-Expert Member
- Feb 27, 2007
- 4,132
- 1,571
Nimesoma taarifa ambayo ilitolewa jana na Katibu Mkuu Kiongozi Ndugu Philemon Luhanjo , ambayo inasema kuwa Rais Kikwete ameteua kikosi kazi kwa ajili ya kusimamia kazi ya kurekebisha shirika la Bima la Taifa (NIC).
Kinachonifanya nishindwe kumuelewa ni kitendo cha kumteua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege Nchini (ATCL) ndugu David Mtaka kuwa miongoni mwa wajumbe sita waliopewa jukumu la kusimamia kazi ya kurekebisha shirika la Bima wakati Mattaka ameshindwa kulisimamia shirika lake mwenyewe mpaka linajifia pamoja na serikali kumwaga mabilioni ya shilingi za walipa kodi kila wakati.
Kikubwa zaidi kinachonifanya nishindwe kumwelewa Kikwete ni kazi za kikosi kazi hicho (Task Force) ambazo ni pamoja na kuandaa mpango wa kazi (NIC Bussiness Plan).
Mataka aliyeshindwa kuandaa mpango kazi kwa ajili ya ATCL mpaka ikafilisika hivi ataweza kulinusuru shirika lingine wakati la kwake limemshinda?
Hivi Mattaka , ambaye ameshindwa kabisa kuliokoa shirika lake anaweza kuokoa NIC?
Kikwete na Mattaka wana mahusiano gani mengine tofauti na ya kikazi? kwani nashindwa kuamini kama Kikwete anashindwa kuona kuwa ATCL imeshindwa kufanya kazi na hata waziri wake wa Miundombinu ilimbidi naye akaunda kikosi kazi kwa ajili ya kulinusuru shirika hilo , huku mkurugenzi wake akiwa ameshazidiwa .
Nashindwa kuzielewa akili za Kikwete kwani anachonionyesha hapa ni kuwa yeye hayaoni mapungufu ya Mattaka , na ndio maana anamtaka aende kuunda mpango kazi wa kufufua shirika lingine wakati la kwake linajifia.
Nashindwa kumwelewa Kikwete anataka kulipeleka wapi shirika la NIC , ama anamtafutia Mattaka sababu ya kusema kuwa alikuwa na kazi nyingi na hivyo alishindwa kusimamia fedha zilizotolewa na serikali siku mahesabu yake yatakapokuwa hayako sawa.?
Kinachonifanya nishindwe kumuelewa ni kitendo cha kumteua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege Nchini (ATCL) ndugu David Mtaka kuwa miongoni mwa wajumbe sita waliopewa jukumu la kusimamia kazi ya kurekebisha shirika la Bima wakati Mattaka ameshindwa kulisimamia shirika lake mwenyewe mpaka linajifia pamoja na serikali kumwaga mabilioni ya shilingi za walipa kodi kila wakati.
Kikubwa zaidi kinachonifanya nishindwe kumwelewa Kikwete ni kazi za kikosi kazi hicho (Task Force) ambazo ni pamoja na kuandaa mpango wa kazi (NIC Bussiness Plan).
Mataka aliyeshindwa kuandaa mpango kazi kwa ajili ya ATCL mpaka ikafilisika hivi ataweza kulinusuru shirika lingine wakati la kwake limemshinda?
Hivi Mattaka , ambaye ameshindwa kabisa kuliokoa shirika lake anaweza kuokoa NIC?
Kikwete na Mattaka wana mahusiano gani mengine tofauti na ya kikazi? kwani nashindwa kuamini kama Kikwete anashindwa kuona kuwa ATCL imeshindwa kufanya kazi na hata waziri wake wa Miundombinu ilimbidi naye akaunda kikosi kazi kwa ajili ya kulinusuru shirika hilo , huku mkurugenzi wake akiwa ameshazidiwa .
Nashindwa kuzielewa akili za Kikwete kwani anachonionyesha hapa ni kuwa yeye hayaoni mapungufu ya Mattaka , na ndio maana anamtaka aende kuunda mpango kazi wa kufufua shirika lingine wakati la kwake linajifia.
Nashindwa kumwelewa Kikwete anataka kulipeleka wapi shirika la NIC , ama anamtafutia Mattaka sababu ya kusema kuwa alikuwa na kazi nyingi na hivyo alishindwa kusimamia fedha zilizotolewa na serikali siku mahesabu yake yatakapokuwa hayako sawa.?