Kweli Yanga mnamuacha Kiiza?

Yes mkuu.
Yanga wamemuwekea mezani $35,000 yeye kachomoa anataka $50,000!!!!!
Ngasa kalamba $30,000 tuu,sasa yeye na Ngassa nani jembe?
Kiiza ni zaidi ya jembe....physique yake ni ya-kisoka; akipata kocha mzuri akampika kisawasawa anaweza kutisha; naomba sana atue Msimbazi mje muone soka itakayo kuwa inatandazwa.
 
Kiiza ni zaidi ya jembe....physique yake ni ya-kisoka; akipata kocha mzuri akampika kisawasawa anaweza kutisha; naomba sana atue Msimbazi mje muone soka itakayo kuwa inatandazwa.
Sasa si bora aende KILUVYA UTD?
 
Kiiza aachwe, siyo tishio kama ilivyokuwa kwa Okwi. Mimi Yanga damu nikisikia Okwi yumo nilikuwa nakosa amani, tangu aondoke ni raha tupu. Hebu tuwe wakweli ni Wanasimba wangapi wanakumbwa na hofu wakimwona Kiiza yuko uwanjani? Hana hadhi ya kuichezea Yanga, kiwango kimeshuka, ni heri ya Ssentongo kuliko Kiiza.
Mimi si mwanaYanga lakini kwa washambuliaji mlionao sasa Kiiza ni bora kuliko hao wengine, labda kama mtasajili lakini mkibaki na hao kina Tegete, Bahanuzi na Kavumbagu ni mara kumi aondoke yeyote ili Kiiza abaki.
 
Mkuu Ulimakafu unamkumbuka Said Swed Scud wewe?Scud yule wa enzi za Abas Gulamali?unakumbuka alivyokua anaifunga Simba anavyotaka?unakumbuka ndio mchezaji wa kwanza wa ligi ya ndani kumiliki gari dogo la kuendea mazoezini?unakumbuka Gulamal aliwahi kutoa chozi kutokana na burudani ya mshikaji uwanjani?lakini kilichofatia ni kuiringia Yanga?akisema mazoezi hayana hadhi na sasa yeye na mazoezi sasa basi isipokua atakua anacheza mechi tuu?unakumbuka nini kilifuatia baada ya hapo?alifukuzwa jangwani zikiwa zimebaki dk chache kuumana na Simba na Yanga akaua mtu,baada ya kutimliwa akarudi zake Mirambo FC na mpira ukafa.

Kiiza anajiona star na hadhi yake sii ya $35,000 ambazo Yanga walikua tayari kumpa na ambazo wachezaji karibu wote wa Yanga wamepewa.Lakini pia kwa ushauri wa coach kasema kwamba kama hataki kusaini kwa pesa hiyo wamwache maana kuna Ngasa,Nizar,Kabange na Msuva wanaoweza kucheza vizuri zaidi.

Hapa Yanga wanabaki kwenye falsafa yao kwamba hawana desturi ya kumbembeleza mchezaji!!

Kweli, lakini tofauti na SCUD ambaye alikuwa anaifunga Simba tu,huyu ni proven striker anayefunga timu yoyote,wangekaa nae tu waelewane,akienda Msimbazi tumeumia.
 
Yes mkuu.
Yanga wamemuwekea mezani $35,000 yeye kachomoa anataka $50,000!!!!!
Ngasa kalamba $30,000 tuu,sasa yeye na Ngassa nani jembe?
Ngassa ana akili za maiti..hajitambui..yule hata bure angesajili Yanga.


Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
kuna tetesi kuwa niyonzima kapewa $50,000 ndo maana kiiza naye anatikisa kiberiti kutaka kiasi hicho!

hata mimi nina mtizamo kama wako mkuu, hizo $35,000 alizotengewa bado ni nyingi mno, angepewa tu 25,000, akikataa waachane naye. akikaa kule ngasa na huku msuva then katikati tegete na bahanuzi huku wakilishwa na niyonzima mbona fowadi nzuri tu hiyo
Mpaka hao akina Bahanuzi na Tegete wafanye kazi ya ziadi pale mbele wajifue.
 
Hili ni wazo makini, mi pia nina mtizamo kama wako. Yanga wakipata fowadi (scorer) angalau mmoja mwenye nguvu itakuwa tishio, wangeachana na the likes of kiiza, kabange sijui beko halafu hizo hela wakainvest kumpata mshambuliaji wa maana!

Spot on mate,that is the thing..proven goal scorer,period...
 
Kiiza limebakia jina tu, si mchezaji wa kutisha kama ambavyo jina lake lavuma...Hata akiondoka leo sidhani kama safu ya mbele ya Yanga itatetereka maana naamini wapo wengi tu wenye kaliba kama yake...
 
Kiiza limebakia jina tu, si mchezaji wa kutisha kama ambavyo jina lake lavuma...Hata akiondoka leo sidhani kama safu ya mbele ya Yanga itatetereka maana naamini wapo wengi tu wenye kaliba kama yake...

Huyo ni mcheza mkuu,amini haya niyasemayo.......
 
Huyo ni mcheza mkuu,amini haya niyasemayo.......
Miaka yote Yanga huwa wanatumia wings kujenga mashambulizi, tena hutumia wingers wenye mbio, chenga na kupiga krosi...mfano wa o kwa uchache ni Lunyamila, Said Maulid, Kipese, Ngassa n.kSasa kwa formation ya 4-3-3 ambayo Yanga wamekuwa wakiitumia kwa muda sasa, unaona kabisa Kiiza anavyokosa ile composure na kuweza kukikimbiza mabeki wa kushoto au ku-cut inside...Kwangu bado namuona ni mchezaji wa kawaida sana tu...
 
Hiyo timu ni ya daraja la ngapi mkuu.
Mkuu hiyo 'KILUVYA UTD'ni timu ya wauza 'NAZI' ipo kibaha maili moja na inashiriki ligi ya wilaya kibaha!

Cc Masau Bwile -msemaji wa chama cha soka kibaha-pwani.
 
Last edited by a moderator:
Miaka yote Yanga huwa wanatumia wings kujenga mashambulizi, tena hutumia wingers wenye mbio, chenga na kupiga krosi...mfano wa o kwa uchache ni Lunyamila, Said Maulid, Kipese, Ngassa n.kSasa kwa formation ya 4-3-3 ambayo Yanga wamekuwa wakiitumia kwa muda sasa, unaona kabisa Kiiza anavyokosa ile composure na kuweza kukikimbiza mabeki wa kushoto au ku-cut inside...Kwangu bado namuona ni mchezaji wa kawaida sana tu...
Mimi bado namkubali sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom