Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Mpaka leo bado ninajiuliza kwa nini kwenye uchaguzi wa mwaka 2010 Kikwete alikacha mdahalo, kwanini CCM iliwazuia wagombea wake kushiriki midahalo na kwa vipi hali hii iliweza kukubalika ndani ya jamii iliyostaarabika.
Tume ye Uchaguzi ikiongozwa na Jaji Mstaafu ilikaa kimya, Ofisi ya Msajili wa vyama ikisimamiwa na Jaji mstaafu ilikaa kimya na taasisi mbali mbali zinazotetea utawala wa kidemokrasia nchini zilikaa kimya.
Lakini kubwa zaidi ni vipi mtu ambaye hakukubali kuhojiwa na waajiri wake (wananchi) kujua kama ana sifa, sababu na uwezo aliweza kupata hiyo ajira. Wana jamvi, naomba hili swali tulijadili bila jazba, kwa nini midahalo inayowapa wananchi fursa ya kuwasikiliza wagombea na kuwauliza maswali, hasa katika hadhi kama ya Uraisi, haikufanyika mwaka 2010?
Kwanini chama tawala kilihakikisha midahalo haifanyiki?
Tume ye Uchaguzi ikiongozwa na Jaji Mstaafu ilikaa kimya, Ofisi ya Msajili wa vyama ikisimamiwa na Jaji mstaafu ilikaa kimya na taasisi mbali mbali zinazotetea utawala wa kidemokrasia nchini zilikaa kimya.
Lakini kubwa zaidi ni vipi mtu ambaye hakukubali kuhojiwa na waajiri wake (wananchi) kujua kama ana sifa, sababu na uwezo aliweza kupata hiyo ajira. Wana jamvi, naomba hili swali tulijadili bila jazba, kwa nini midahalo inayowapa wananchi fursa ya kuwasikiliza wagombea na kuwauliza maswali, hasa katika hadhi kama ya Uraisi, haikufanyika mwaka 2010?
Kwanini chama tawala kilihakikisha midahalo haifanyiki?