Kwann TBC haikulipa kipaumbele tukio la uvamizi Mkuranga

Mkuu, TBC wanaamini kwamba wao pekee ndiyo wenye uwezo na nguvu ya kufika maeneo ya vijijini na hivyo kukaa kwao kimya katika matukio kama haya kunawafanya wananchi waliopo vijijini au pembezoni wasipate
habari zenye kushitua kama hizi
na kuwafanya wawe na maswali au mashaka na utendaji na umakini wa serikali yao. Rejea mkasa wa meli kule Nungwi TBC walikuwa wanapiga taarabu huku habari ikisambaa
kama moto hadi vijijini. Binafsi tukio la kuuwawa kwa askari huko Mkuranga nimelisikia kwa mara ya kwanza kutoka kwa ndg yangu aliyeko Nanyumbu tena kijijini kabisa.

Hivyo wamepoteza sifa ya kuitwa televisheni ya Taifa wanashindwa hata na vituo binafsi kuonyesha matukio kadhaa kwanza hata wakionyesha picha zinakua mnato mara sauti inawahi kuliko msemaji wa tukio, wakati mwingine picha giza tupu
 
Hivyo wamepoteza sifa ya kuitwa televisheni ya Taifa wanashindwa hata na vituo binafsi kuonyesha matukio kadhaa kwanza hata wakionyesha picha zinakua mnato mara sauti inawahi kuliko msemaji wa tukio, wakati mwingine picha giza tupu
TBC haina mvuto hata kwa muonekano wake. Imepauka rangi. watangazaji hawana mvuto, japo si wote.
 
Hili tukio halipo kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM, kumbuka huu ni wakati wa kutekeleza ilani
 
sasa we umeiona hiyo njaa uchwara ya tundu lissu.
au gharama chakula tu iko juu?
Ukiona kilo 25 za unga bei yake imefikia zaidi ya elfu 40 halafu ukaendelea kushangilia wewe ni zoba na zuzu.
Wewe unadhani gharama zimeongezeka kwa sababu wananchi wamekuwa matajiri ghafla au kwa kuwa bidhaa hizo zimekuwa haba?
 
Hili tukio halipo kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM, kumbuka huu ni wakati wa kutekeleza ilani
Kwa kweli. Nadhani mkulu hakuahidi kutoa taarifa za namna hii wakati wa kampeni zake.
 
Wana jamvi

Kituo cha Taifa cha televisheni yaani TBC haikuitendea haki taarifa yenye majonzi kwa uvamizi na kuuawa kwa askari wa jeshi la polisi Mkuranga, hili ni tukio lenye sura ya kitaifa kwa maana ya kupoteza askari wetu, lakini kituo cha tbc tunachokitegemea sana kutuhabarisha kimelipa kisogo tukio hilo lilnalopingwa na kulaaniwa na wadau wote wa amani nchini, TBC walichotakiwa kufanya ni kuwatafuta wasemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani na vyombo husika ili tujuzwe hali ilivyo, hii ni tofauti kwa vyombo vya habari vya nchi za Ulaya na Marekani vituo vyote vya ulaya na Marekani vinaweka vipaumbele vya matukio hatari kama hayo kwa kuandika "Breaking news" za mara kwa mara kuhusu matukio yenye sura za kivamizi na mauaji
Ukisikia UMBEA NDIO HUU.
 
Mkulu aliwagombesha ITV kwa kutangaza habari za mapigano ya wakulima na wafugaji badala ya kutangaza habari za maendeleo
 
Back
Top Bottom