Kwanini watanzania ( hasa wanafunzi) wanakataa kuchukua fursa hizi?

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
May 30, 2008
5,457
956
Nimekuwa nikijiuliza kila mara, kwenye nchi za wenzetu ni kawaida sana kukutana na wahudumu ( waiters/waitresses) ambao ni wanafunzi hasa wa vyuo vikuu wakifanya kazi kwenye mahoteli au migahawa kama namna ya kuongeza kipato kwa njia ya halali. Siyo huko tu, hata kwenye maktaba, maduka ya nguo, vyakula, nk. Hii ni kwa uchache tu.Tanzania sijabahatika kuona hili... hapo hapo unaona wanafunzi waki struggle sana kupata pesa au kulalamika kuwa pesa wanayoipata haiwatoshi. Siyo ajabu kusikia wanafunzi hasa wa kike wakisemwa kuwa wanafanya vitendo visivyo sawa kujipatia pesa.

Ni kwanini watanzania hatujaona hizi fursa za kupata pesa ya halali na hapohapo kujitengenezea CV ili pale mtu utakapotafuta kazi " experience" isiwe ni tatizo tena maana moja ya sababu zinazowakosesha kazi vijana wengi ni kukosa uzoefu.

Naweza nikawa nakosea , labda tayari wapo wenye kufanya hizi part time, lakini nadhani wengi bado wanasubiri kuja kuanza kazi wamalizapo vyuo au kufanya "tempo" wawapo likizo...
Hebu tubadilishane uzoefu kama namna ya kusaidiana kutatua matatizo ya kijamii..
 
Ni mtazamo wa kazi yenyewe kwenye jamii yetu huku kwetu bar maid anaoneka ana multiple task/double role ya kuhudumia vinywaji pamoja na kuhudumia wateja wa kiiume kimwili/kujiuza. Kwa mantiki hiyo kuwa bar maid kwa bongo ni uhuni/umalaya.

Vilevile wengi wa ma bar maid bongo wanajiuza tena very cheap wengine kwa hata bia moja tu, hali kama hio inachangia sana kudhoofisha hio career. Pia ukieenda na mkeo bar hawakuudumii vizuri unaweza kaa hata dakika 20 no service, wanachukia wanaona soko limekufa.

Kwa wahudumiwaji wanaume nao wana matatizo pia bia 1 tu bar maid anageuka wife/anamuuona mzuri kila bia inavyopanda kichwani then wanashikashika hovyo hadharani. Nahisi wengi hichi kitendo hawakipendi ila wafanyeje sasa ndio kazi yenyewe kususa hawawezi na muda unaavyooenda wanazoea kushikwashikwa hadharani.

Kazi yenyewe hailipi kwa nje wanalipwa kwa masaa 100$ + hapa kwetu kwa mwezi TZS 30.

Hivi sheria sheria inasemaje kuhusu kuwalinda dada zetu.
 
Ngoja niangalie ilani ya chama inasemaje kwa hili.
Maana lazima misingi ijengwe mapemaa
 
Ni mtazamo wa kazi yenyewe kwenye jamii yetu huku kwetu bar maid anaoneka ana multiple task/double role ya kuhudumia vinywaji pamoja na kuhudumia wateja wa kiiume kimwili/kujiuza. Kwa mantiki hiyo kuwa bar maid kwa bongo ni uhuni/umalaya.

Vilevile wengi wa ma bar maid bongo wanajiuza tena very cheap wengine kwa hata bia moja tu, hali kama hio inachangia sana kudhoofisha hio career. Pia ukieenda na mkeo bar hawakuudumii vizuri unaweza kaa hata dakika 20 no service, wanachukia wanaona soko limekufa.

Kwa wahudumiwaji wanaume nao wana matatizo pia bia 1 tu bar maid anageuka wife/anamuuona mzuri kila bia inavyopanda kichwani then wanashikashika hovyo hadharani. Nahisi wengi hichi kitendo hawakipendi ila wafanyeje sasa ndio kazi yenyewe kususa hawawezi na muda unaavyooenda wanazoea kushikwashikwa hadharani.

Kazi yenyewe hailipi kwa nje wanalipwa kwa masaa 100$ + hapa kwetu kwa mwezi TZS 30.

Hivi sheria sheria inasemaje kuhusu kuwalinda dada zetu.

Asante kwa mchango wako ndugu yangu. Ukiachilia mbali bar.. ambapo nilitoa kama mfano tu. Inaweza kuwa mgahawa pia ambao hauuzi pombe na bado hutaona watu wakijishughulisha na part time.Hata vijana wa kiume pia hawajishughulishi.

Nadhani ni utamaduni tu uliojengeka wa kutokutaka kujishughulisha nje ya kile mtu alicho focus on. Mtu akiwa mwanafunzi hataki kujishughulisha na kingine.
 
Asante kwa mchango wako ndugu yangu. Ukiachilia mbali bar.. ambapo nilitoa kama mfano tu. Inaweza kuwa mgahawa pia ambao hauuzi pombe na bado hutaona watu wakijishughulisha na part time.Hata vijana wa kiume pia hawajishughulishi.

Nadhani ni utamaduni tu uliojengeka wa kutokutaka kujishughulisha nje ya kile mtu alicho focus on. Mtu akiwa mwanafunzi hataki kujishughulisha na kingine.

Mwalimu shuleni anatumia lugha gani kufundisha? Nakumbuka mwalimu wetu alikuwa anasema,soma vizuri ili utakapomaliza masomo yako upate kazi nzuri. Kwa hiyo tunasubiri mpaka tumalize masomo yetu ndio tuanze kazi.:love:
 
WOS hiyo ni changamoto kwa wanafunzi

Mfano mzuri ni nilishuhudia Kampala na Nairobi, kwenye mahotel na baa maarufu wanafunzi waliopo vyuo vyuoni kweli wanafanya kazi kama part time kwenye hiyo miji japo hawapo wengi saana.Kwa Tanzania sijawahi ona kabisa,, kwa mawazo yangu naona labda ni uchache wa mahotel na mabaa, pili ni ile kasumba kwamba mwanafunzi wa chuo kikuu hawezi fanya kazi kama hizo, Tatu mahoteli mengi yanapenda kuwachukua wanafunzi kutoka vyuo vilivyosajiliwa na VETA na kwingineno na kuwapatia ajira japo wanawalipa mshahara kidogo saana.Na la mwisho mfumo na kasumba tuliowajengea watoto wetu ndo chanzo kikubwa kwa hawa wanafunzi kutojishughulisha. mwanafunzi anajua nikishiwa kama sio baba au mama atanipa pesa, ntamwomba mjomba au shangazi, kaka au dada ua hata na ma BF na ma GF ni chanzo kikubwa cha kipato kwa wanafunzi wetu wa vyuo vikuu..
 
Asante kwa mchango wako ndugu yangu. Ukiachilia mbali bar.. ambapo nilitoa kama mfano tu. Inaweza kuwa mgahawa pia ambao hauuzi pombe na bado hutaona watu wakijishughulisha na part time.Hata vijana wa kiume pia hawajishughulishi.

Nadhani ni utamaduni tu uliojengeka wa kutokutaka kujishughulisha nje ya kile mtu alicho focus on. Mtu akiwa mwanafunzi hataki kujishughulisha na kingine.

Tunarudi pale pale huko migahawa iko mingapi hapa dar?TZ na inauwezo wa kuwalipa hata kiasi? je umewahi kufanya ka utafiti kadogo kuhusu payment?

Na nilisema hapo juu kuwa kwa bongo hakuna pati taimu wanapendelea full time kwa mwezi hyuo mwanafunzi atasoma saa ngapi? kwa bar lazma wafike kuanzia saa 7 mchana.
 
Nahisi wengi hichi kitendo hawakipendi ila wafanyeje sasa ndio kazi yenyewe kususa hawawezi na muda unaavyooenda wanazoea kushikwashikwa hadharani.

Kazi yenyewe hailipi kwa nje wanalipwa kwa masaa 100$ + hapa kwetu kwa mwezi TZS 30.

Hivi sheria sheria inasemaje kuhusu kuwalinda dada zetu.

Naamini mwajiri akikusudia anaweza kubadili hii mitazamo na namna watu wanawachukulia wafanyakazi wa maeneo haya. na hata hili la maslahi pia siamini kama linashindikana. Utalipwa vizuri kutokana na kazi nzuri unayoifanya.Huko nje kama wanalipwa 100$ kwa saa ni kwa vile wanazalisha zaidi ya hicho wanacholipwa kwa muda ule wanapokuwa kazini. Ni discipline ya kazi. Ikiwa mteja atahudumiwa vizuri kwa haraka for sure ataspend pesa yake kuliko ukimpa service za kipuuzi zinazotolewa hapa, wateja watakuwa wengi na bei pia itaendana na wahudumu.
 
kujitengenezea CV ili pale mtu utakapotafuta kazi "experience" isiwe ni tatizo tena maana moja ya sababu zinazowakosesha kazi vijana wengi ni kukosa uzoefu
u baa meidi utanisaidiaje kwenye resume ya kuombea kazi ya utafiti wa cardiovascular diseases
 
Tunarudi pale pale huko migahawa iko mingapi hapa dar?TZ na inauwezo wa kuwalipa hata kiasi? je umewahi kufanya ka utafiti kadogo kuhusu payment?

Na nilisema hapo juu kuwa kwa bongo hakuna pati taimu wanapendelea full time kwa mwezi hyuo mwanafunzi atasoma saa ngapi? kwa bar lazma wafike kuanzia saa 7 mchana.

Hii yote ni mipangilio kati ya mwajiri na mwajiriwa...hata huko nje hawa wanafunzi si kwamba wanaajiriwa full time, wanaingia kwa shift kulingana na nafasi zao. By the way kwa hali kama hii ya kazi za kuanzia saa saba mwajiri anataka mtu wa full time wa nini? Ni makubaliano na discipline. Ila kwa vile waajiri wanapenda cheap labour ndio maana hata kila kitu kinakuwa cheap! Unaenda somewhere for a drink wahudumu wanaendelea na maongezi yao kwa kelele kama hakuna wateja, hakuna wa kukuhudumia mpaka uite, kulipa mpaka uwaombe naomba sasa niwalipe! Taabu kweli kweli
 
Hii yote ni mipangilio kati ya mwajiri na mwajiriwa...hata huko nje hawa wanafunzi si kwamba wanaajiriwa full time, wanaingia kwa shift kulingana na nafasi zao. By the way kwa hali kama hii ya kazi za kuanzia saa saba mwajiri anataka mtu wa full time wa nini? Ni makubaliano na discipline. Ila kwa vile waajiri wanapenda cheap labour ndio maana hata kila kitu kinakuwa cheap! Unaenda somewhere for a drink wahudumu wanaendelea na maongezi yao kwa kelele kama hakuna wateja, hakuna wa kukuhudumia mpaka uite, kulipa mpaka uwaombe naomba sasa niwalipe! Taabu kweli kweli

Lack of motivation
 
u baa meidi utanisaidiaje kwenye resume ya kuombea kazi ya utafiti wa cardiovascular diseases

Hili ndio tatizo! Na hapo ndipo unaona jinsi watu wanavyoshindwa kuhusisha kazi zao na maisha yao ya kila siku. Uhudumu unaweza kukusaidia katika kujifunza kuweza kufanya kazi jirani na watu wa aina tofauti, kuhimili challenges hizo zote ni life skills. kama wewe ni medical doctor si utakutana na watu kwenye kazi yako? Wakija wengine toka nje tunashangaa wnapewaje kazi za miradi ooooh kule kwao hajasoma kabisa! Anasimamiaje mradi huu mkubwa hivi na mimi nimesoma sanaaaaa natumwa tumwa nae! mmmmmh huna some other necessary attributes. Hili halimaanishi uhudumu kwenye bar ndio utakupa yote na ndio uende huko zipo kazi ndogo ndogo nyingine huwa tunazidharau
 
Thanks WOS;

I think its another missed opportunity by many Tanzania youths, mimi ni memba mzuri wa Bar na ukijaribu kufuatilia kwenye busy bars mjini, apart from tips, wale wahudumu huwa wanatoka hadi na over 50,000 TZS kwa siku hasa wikendi na kama wadogo zetu wangeweza kuchukua hizi nafasi wangekua mbali, haya ya kusema kazi imekosa maadili nadhani yanategemea mtu mwenyewe

kuna hadi wake za watu wanafanya zile kazi na wanafanikiwa, similarly there are opportunity kwenye kuuza maduka, migahawa, car wash [although we dont have good car wash i hope its a next booming business baada ya male salons]

Its a good idea indeed
 
Kazi si lazima bar tu mtu anaweza kuwa hata babysitter kwa yule anayesoma masomo ya jioni. hata kuwa mfanya usafi wa ofisi fulani inakuongezea kipato. Nakumbuka nilivyokuwa nasoma chuo nchi moja ya jirani kuna semester moja nilikuwa nafanya kazi ya usafi wa ofisi ya traveling agency mara tatu kwa wiki. issue kama za kufanya usafi hizo ni za jioni hata wale wanaosoma day programmes wanaweza kuzifanya.

Kuhusu kujenga resume yako hapo inabidi ukomae na kazi zinazoeleweka kama ni reception au secretary au hata messenger.
 
Soko la Tanzania liko tayari kuajiri part timers?

Na hao wanafunzi wa chuo kikuu wako tayari kuajiriwa kwa thamani ya mtu asiyeenda shule au kamaliza la saba? Manake nakumbuka Nilipomaliza form 4 kwa kipindi cha kusubiri kuingia form 5 niliajiriwa kwetu kwa mama yangu Kama mfanyakazi wa ndani na mwisho wa mwezi nikilipwa Kama ambayo angelipwa mfanyakazi lkn rafiki zangu wote walinicheka na kughiari kukaa tu nyumbani bila kazi kuliko ' kazi Kama hiyo'

kuna haja ya kuwaelimisha wanafunzi na waajiri kuwa wanafunzi wa chuo kikuu watakuwa na ufanisi zaidi ya waajiriwa wasiokuwa na elimu ya juu.....
 
Simple sana waiter/waitress nchi za nje wanachukua pesa nzuri sana hasa ukizingatia tips na mazingira ya kazi nayo ni mazuri. Bongo kuwa waitress ni mateso tu! Minimum wage una bahati ukiipata, na tips bongo hakuna plus sexual harassment is part of the job, sasa kwa mtu mwenye elimu ya nini hayo?
 
Nimependa michango yenu wote hapo juu na ninashindwa hata ku quote! Fantastic!
1. Part time jobs Tanzania kwa sasa zipo nyingi na wapo waajiri wangependa sana kuwaajiri ila tatizo ni kama alivyoonyesha mchangiaji mmoja hapo juu kuwa " mimi ninasomea kozi xyz, haihusiani na kazi abc! Hapa inaonyesha moja kwa moja kuwa Watanzania wengi wamefunnga akili zao na hawafikirii outside the box! Kama ni experience, mtu anashindwa kuona kuwa pamoja na kuwa u waiter/waitress hauhusiani na taaluma yako, bado kuna kitu utapata - mfano kuwa a Team player which is very important katika kazi yoyote hata kama wewe ni daktari.Pili, unajifunza people skills maana utakutana na watu wa kila aina na utajifunza na problem solving! Hakuna chuo/shule ambayo utaenda kozi kama hizi ispokuwa practically!

2. Watu wana kasumba bado kuwa kuna kazi za kisomi na zile zisizo za kisomi! Watu wanadharau kazi kama za huduma - wanasubiri wahitimu kisha wakatafute kazi za professions zao. Kujituma na kuwa tayari kwa kazi yoyote ni kipimo cha mchapa kazi. Unapokuwa na kiburi cha kuchagua kazi inaonyesha wazi kuwa utakuja kuwa tatizo kwenye ajira. Mimi kama mwajiri watu kama hawa nikiona applications zao naziweka kando wala sizisomi!
 
Thanks WOS;

I think its another missed opportunity by many Tanzania youths, mimi ni memba mzuri wa Bar na ukijaribu kufuatilia kwenye busy bars mjini, apart from tips, wale wahudumu huwa wanatoka hadi na over 50,000 TZS kwa siku hasa wikendi na kama wadogo zetu wangeweza kuchukua hizi nafasi wangekua mbali, haya ya kusema kazi imekosa maadili nadhani yanategemea mtu mwenyewe

kuna hadi wake za watu wanafanya zile kazi na wanafanikiwa, similarly there are opportunity kwenye kuuza maduka, migahawa, car wash [although we dont have good car wash i hope its a next booming business baada ya male salons]

Its a good idea indeed

Asante ndugu yangu maana naona umefaulu the ACID TEST!
 
kuajiriwa kwa part time bongo haiko kabisa,kuazia maduka,migahawa nk
full manyanyaso pia yani sheria za ajira hazipo sijui au hatuzijua au hazifatiliwi
mpaka umalize shule ndo waweza pata angalao part-time
me nilipokuwa chuo nilipata NGO moja km part-time,nafundisha elimu rika nk na walipwa ka masaa na nilifanya kwa moyo kwakwel nikawa hadi wananitafuta mara nyingi tu naenda ilintoa sana iyo shughuli ,adi ss nna kazi yangu bt likizo namalizia partly hapo na sehemu zingine nikiweza (sijawai omba pesa ya baba/mama wala shugamamy au BF)...
ni moyo tu wa kazi vijana hawana na kujitolea pia
 
Back
Top Bottom