God bell
JF-Expert Member
- May 13, 2011
- 590
- 210
Hodi wanaJF mimi ni mgeni humu jukwaani nikiwakwaza mnisamehe. Mada yangu ni kwamba wanawake wengi sana ndo huwa wanawafanya waume zao mazezeta kwa kuwaendea kwa waganga ili waweze kuwapooza wapate nafasi ya kufanya mambo yao wanayotaka wenyewe.Nimetoa hii mada maksudi kwa sababu: Nina rafiki yangu nafanya nae kazi na pia tunaishi mtaa mmoja alipata matatizo km haya. Mke alikuwa anatoka nje ya ndoa jamaa akamfumania live ukawa ugomvi mkubwa sana na jamaa akawatangazia ndugu wa mke na mjirani kila kitu jinsi alivyomfumania na hamtaki tena wa kwanza akiwa mimi kuambiwa. Wakiwa kwenye ugomvi ndani ya cku 2 mke akaondoka asubuh akaenda kuckojulikana. Aliporudi kesho yake akamkuta mzee nyumban yuko kama mbogo aliyefukuzwa na simba, akampikia chakula. Mzee alipokula tu hasira zote zikaisha akasahau kila kitu. Cha kushangaza ni kwamba mke ndo amekolea kutembea nje ya ndo na si mwanaume mmoja. Na sasa hv jamaa anajua kila kitu lakini amepoa kama maji kwene mtungi. Kuna cku alipigiwa cm kuhusu mke wake akajibu 'nyie ndo mnanigombanisha na mke wangu' na jamaa ninavyomuona yuko km amechanganyikiwa. Jamani huyu jamaa c ameshafanywa zezeta tayari? Kwani hata shuguli za mendeleo amesitisha na mke nde mwenye kupokea hela na kujivinjari na mabwana zake wa nje.