Lol, wanajikausha hapa kukwepa kukujibu.
Nina theories 2
1- kuna genetic disorder inaharibu gene pool
2- maisha yamekuwa magumu sana, kuna scarce resource na matumizi ya wanawake wa siku hizi yamezidi. So wanaume wa siku hizi hawawezi kuendelea kujilea na kulea familia zao. Zamani mwanaume akileta kitenge cha morogoro tu na chachacha na shanti mama anakenua. Siku hizi lace wig, mkorogo, gari, nyumba, jenereta, sijui maskuli bus! Baba wa watu awezee wapi jamani?
Note: kumnunulia mpenzio vitu na kumpa treat sio kumlea. Wanawake tuna silika ya uchoyo na kujihesabia haki ya kutunzwa kila wakati bila kusoma alama za nyakati.
Majibu pls.
Mmmh.. Hata mie nilishakutana na mmoja wa hawa wanaume wenye kupenda kulelewa.. Utasikia Baby nimesahau ATM Card yangu lipia tuu wewe hii bill.. Sasa sio mara moja, leo atakwambia kasahau wallet kesho amesahau ATM card..! Mara siku nyingine anaomba umkopeshe pesa.. Duuh, ukimkopesha ndio imetoka..! Lol..! Aaah... Hayo mapenzi yalinishinda..!
Sasa hayo yote mbona ni maisha tuu.......hakina jema alowahi kukufanya......sorry kukufanyia
Aaaah... Tunaongelea baadhi ya wanaume kupenda kulelewa... Kama suala ni kunifanyia jema hata mie mema mengi nilimfanyia...! Ila suala la kunigeuza mie ATM machine kila siku lilinishinda..!