Infinite_Kiumeni
JF-Expert Member
- Jan 23, 2023
- 382
- 661
Wanawake ni viumbe wanaopenda kufanya udadisi hasa linapokuja suala la mahusiano. Hii ni kwasasabu wanawake hawaridhiki mpaka wapate kile wanachokitaka, kabla hawajakipata hicho kitu mawazo yao na hisia zao muda mwingi zinakua juu ya hicho kitu. Kumfanya mwanamke awe mtafiti kwako ni moja ya changamoto mwanamke anazohitaji ili aendelee kuwa nawe kimapenzi.
Akikutambua 100%, atakua hana cha kufanyia utafiti, hana cha kumpa mawazo, hana cha kumfanya ajisikie hisia za kuna kitu hakijui kuhusu wewe, hana cha kumpa changamoto, inabidi akuache ili atafute sehemu nyingine ya kumpa hulka ya utafiti na akibaki utajikuta upo kwenye mazoea na mwanamke, jambo ambalo sio zuri kimapenzi, mnaishia kufanya mapenzi kutimiza wajibu tu.
Hii ndio sababu wanaume wanaowadanganya wanawake wanaendelea kupendwa na kuishi nao, sababu mwanamke anakua hana jibu sahihi na ataendelea kuwa naye mpaka aone ukweli ni upoje. Unakuta mwanamke anayedanganywa ataolewa kila mwaka anaendelea kuwa na huyo mwanaume na kujipa moyo lakini anamkataa mwanaume anayemuweka wazi kwamba anataka amuoe na kila kitu kipo tayari, alafu anashangaa kwanini amekataliwa.
Ukisema udanganye, uongo una madhara yake, utaishia kutengeneza mahusiano yenye sumu, na penye uongo hakuna maendeleo. Ukisema ufiche kila kitu utaonekana huna upendo pia hakutakua na maendeleo ya muda mrefu kifamilia.
Njia ipi ni sahihi sasa?
Mpatie mwanamke majibu taratibu. Utatengeneza mazingira rahisi ya kuchombezana na furaha (chombezo na furaha huimarisha mahusiano) kwa kuwa atakua anakuchombeza na kukubembeleza umpatie majibu. Pia na wewe unamchombeza na kumpatia jibu moja moja, alafu rudisha mada kwake kwa kumuuliza swali ajielezee.
Mfano, anakuuliza “unafanya kazi gani” na wewe unamjibu kiujumla, mfano we ni fundi wa kuweka vigae, unamjibu “nafanya kazi ya kupendezesha nyumba za watu” huku ukiwa na tabasamu sababu unafurahia kazi yako.
Kwa mwanamke ambaye anataka kukujua ni lazima atakuuliza maswali zaidi, wewe utaamua uendelee kumpa majibu taratibu au ubadili mada muda wowote ili abaki na maswali zaidi juu yako na kujitengezea picha nzuri/ ya kimapenzi kuhusu wewe yeye mwenyewe. Jambo litakalomfanya aendeleze utafiti juu yako.
Lakini ni muhimu ujue maswali ya kutoa jibu lote, na ni muda gani unatakiwa utoe majibu taratibu ili kumfanya mwanamke awe mdadisi zaidi juu yako, na kuendelea kukupa mawazo na hisia zake. Ukichanganya hayo utaonekana muongo au unataka sifa au mtu usiye makini na atakuchukulia kama mtu wa michezo tu na hutotengeza mahusiano matamu.
Ndio maana kuna kundi maalumu la wanaume (Whatsapp), kila siku utajifunza kuboresha mahusiano yako kwa njia zilizothibitishwa kumvutia na kumtunza mwanamke unayehitaji kujenga naye maisha.
Akikutambua 100%, atakua hana cha kufanyia utafiti, hana cha kumpa mawazo, hana cha kumfanya ajisikie hisia za kuna kitu hakijui kuhusu wewe, hana cha kumpa changamoto, inabidi akuache ili atafute sehemu nyingine ya kumpa hulka ya utafiti na akibaki utajikuta upo kwenye mazoea na mwanamke, jambo ambalo sio zuri kimapenzi, mnaishia kufanya mapenzi kutimiza wajibu tu.
Hii ndio sababu wanaume wanaowadanganya wanawake wanaendelea kupendwa na kuishi nao, sababu mwanamke anakua hana jibu sahihi na ataendelea kuwa naye mpaka aone ukweli ni upoje. Unakuta mwanamke anayedanganywa ataolewa kila mwaka anaendelea kuwa na huyo mwanaume na kujipa moyo lakini anamkataa mwanaume anayemuweka wazi kwamba anataka amuoe na kila kitu kipo tayari, alafu anashangaa kwanini amekataliwa.
Ukisema udanganye, uongo una madhara yake, utaishia kutengeneza mahusiano yenye sumu, na penye uongo hakuna maendeleo. Ukisema ufiche kila kitu utaonekana huna upendo pia hakutakua na maendeleo ya muda mrefu kifamilia.
Njia ipi ni sahihi sasa?
Mpatie mwanamke majibu taratibu. Utatengeneza mazingira rahisi ya kuchombezana na furaha (chombezo na furaha huimarisha mahusiano) kwa kuwa atakua anakuchombeza na kukubembeleza umpatie majibu. Pia na wewe unamchombeza na kumpatia jibu moja moja, alafu rudisha mada kwake kwa kumuuliza swali ajielezee.
Mfano, anakuuliza “unafanya kazi gani” na wewe unamjibu kiujumla, mfano we ni fundi wa kuweka vigae, unamjibu “nafanya kazi ya kupendezesha nyumba za watu” huku ukiwa na tabasamu sababu unafurahia kazi yako.
Kwa mwanamke ambaye anataka kukujua ni lazima atakuuliza maswali zaidi, wewe utaamua uendelee kumpa majibu taratibu au ubadili mada muda wowote ili abaki na maswali zaidi juu yako na kujitengezea picha nzuri/ ya kimapenzi kuhusu wewe yeye mwenyewe. Jambo litakalomfanya aendeleze utafiti juu yako.
Lakini ni muhimu ujue maswali ya kutoa jibu lote, na ni muda gani unatakiwa utoe majibu taratibu ili kumfanya mwanamke awe mdadisi zaidi juu yako, na kuendelea kukupa mawazo na hisia zake. Ukichanganya hayo utaonekana muongo au unataka sifa au mtu usiye makini na atakuchukulia kama mtu wa michezo tu na hutotengeza mahusiano matamu.
Ndio maana kuna kundi maalumu la wanaume (Whatsapp), kila siku utajifunza kuboresha mahusiano yako kwa njia zilizothibitishwa kumvutia na kumtunza mwanamke unayehitaji kujenga naye maisha.