Kwanini Nyota wa Soka wa Amerika Kusini wanachukiana Ulaya?!

Gang Chomba

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
20,301
4,681
Kwa wageni wa Soka na watoto waliouvamia mchezo huu kwa kusukumwa na shetani la kamari ndio wanaweza kushangazwa na umwamba wanao wekeana nyota wa klabu ya PSG Edinson Cavani raia wa Uruguay na Neymar jr raia wa Brazil.

Lakini kwa wenyeji wa mchezo huu, ambao tulianza kuufuatilia mchezo wa soka yapata miongo miwili na miaka ipatayo nusu ya mwongo mmoja, waala hatujashtushwa na ubabe wa kila mmoja kati ya wawili hao.

Kule bara la Amerika ya Kusini kila nchi ni temi. Japo wengi huhisi kuwa watemi wa bara lile ni Brazil na Argentina.
Umwamba wa wachezaji wa bara lile, tena wenyewe kwa wenyewe haukuanza jana wala juzi…

Hivi mnakumbuka sakata la Ronaldo de Lima raia wa Brazil na Ivan Zamorano raia wa Chile, pale walipogombea jezi nambari 9 mgongoni kiasi kwamba uhasama ulipelekea kuigawa klabu ya Inter Milan kwani washabiki walisimama upande wa Zamorano ambae ndie alikuwa na jezi hio, lakini uongozi wa klabu ukiongozwa na milionea wa visima vya mafuta ambae ndie alikuwa mmiliki klabuni hapo Masimo Moratti ulitaka jezi hio apewe mchezaji ghali alienunuliwa kwa dau la kuvunja rekodi ya Dunia karne iliopita?

Nani ambae hakuwahi kuona jezi ikiwa na namba ya tofauti ambayo Zamorano aliamua kuivaa ili kumuachia De Lima namba 9?

Hivi ni nani asiekumbuka aina ya ushangiliaji alioitumia Ivan Zamorano baada ya kufunga goli huku akiwa kavaa jezi namba 1+8 ambayo ilikuwa na jawabu la 9?

Je ilimaanisha Inter walikuwa na jezi mbili zenye nambari 9 mgongoni?

Je nani kasahau ugomvi wa De Lima na Alvaro Recoba wa kugombea mipira mfu iliopatikana katika mechi za klabu hio?

Kuna sababu ya matukio haya kutokea.

Kwa sasa endelea kunywa Mtori, Nyama utazikuta chini…

Nitarudi…

IMG_7105.jpeg
 
Kwa wageni wa Soka na watoto waliouvamia mchezo huu kwa kusukumwa na shetani la kamari ndio wanaweza kushangazwa na umwamba wanao wekeana nyota wa klabu ya PSG Edinson Cavani raia wa Uruguay na Neymar jr raia wa Brazil.

Lakini kwa wenyeji wa mchezo huu, ambao tulianza kuufuatilia mchezo wa soka yapata miongo miwili na miaka ipatayo nusu ya mwongo mmoja, waala hatujashtushwa na ubabe wa kila mmoja kati ya wawili hao.

Kule bara la Amerika ya Kusini kila nchi ni temi. Japo wengi huhisi kuwa watemi wa bara lile ni Brazil na Argentina.
Umwamba wa wachezaji wa bara lile, tena wenyewe kwa wenyewe haukuanza jana wala juzi…

Hivi mnakumbuka sakata la Ronaldo de Lima raia wa Brazil na Ivan Zamorano raia wa Chile, pale walipogombea jezi nambari 9 mgongoni kiasi kwamba uhasama ulipelekea kuigawa klabu ya Inter Milan kwani washabiki walisimama upande wa Zamorano ambae ndie alikuwa na jezi hio, lakini uongozi wa klabu ukiongozwa na milionea wa visima vya mafuta ambae ndie alikuwa mmiliki klabuni hapo Masimo Moratti ulitaka jezi hio apewe mchezaji ghali alienunuliwa kwa dau la kuvunja rekodi ya Dunia karne iliopita?

Nani ambae hakuwahi kuona jezi ikiwa na namba ya tofauti ambayo Zamorano aliamua kuivaa ili kumuachia De Lima namba 9?

Hivi ni nani asiekumbuka aina ya ushangiliaji alioitumia Ivan Zamorano baada ya kufunga goli huku akiwa kavaa jezi namba 1+8 ambayo ilikuwa na jawabu la 9?

Je ilimaanisha Inter walikuwa na jezi mbili zenye nambari 9 mgongoni?

Je nani kasahau ugomvi wa De Lima na Alvaro Recoba wa kugombea mipira mfu iliopatikana katika mechi za klabu hio?

Kuna sababu ya matukio haya kutokea.

Kwa sasa endelea kunywa Mtori, Nyama utazikuta chini…

Nitarudi…

View attachment 2801325
hizi habari ulizo ziandika hapa , mwanaspoti kaziandika sana mkuu.

but issue za bifu kwa wachezaji zinatengenezwa na conflict of intetest miongoni mwa wachezaji na sio utaifa,ukanda ama utaifa.

mfano :van nesterlooy vs Ronaldo (man united)

Ronaldo vs Raul gonzalez
William gallas vs kolo toure
 
Umeandika vizuri ila napingana nawewe Zamorano na Ronaldo hawakuwa na bifu mkuu hizo namba yalikua mambo ya kibiashara niliangalia world cup 1998 baada ya mechi Brazil vs Chile Zamorano na Ronaldo walikua wanapiga story na walikua wamekumbatiana
 
Umeandika vizuri ila napingana nawewe Zamorano na Ronaldo hawakuwa na bifu mkuu hizo namba yalikua mambo ya kibiashara niliangalia world cup 1998 baada ya mechi Brazil vs Chile Zamorano na Ronaldo walikua wanapiga story na walikua wamekumbatiana

Hivi unajuwa hata Picha ya pamoja ya klabu ilichelewa kupigwa baada ya pande zote mbili kutokukubaliana kuhusiana na hio jezi?!
 
Navyojua hao vijana wa Amerika kusini kma wana visasi sana wao kwa wao, angalia tu ndani ya Argentina mechi ya River plate vs Bocca junior..Wakikutana ni vurugu mwanzo mwisho.
 
Sasa sisi vijana wa leo tumeingiaje kwenge masimango ya namna hiyo??

Wewe kuzaliwa mapema ndo ubatunanga tuliozaliwa baada yako!!
Anatusimanga kama tuliamua au kupanga wenyewe vile hayo mambo ya kuzaliwa,,kuzaa,,na kuzaliana!!Mleta thridi mafii Yakee
 
😂🤣😂🤣 dah naona mmekuja wengi kunipinga badala ya kusoma mada na kusubiri muendelezo
Hao ndio wale hata ukiwauliza Abajalo wanaijuwa watakwambia IPO Nigeria, ni wa kuwaangalia tu.

Mkuu usipotee sana, jukwaa limepoteza muelekeo wake hili.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom