Yofav
JF-Expert Member
- Mar 12, 2021
- 3,967
- 6,907
Habari wana Jf,
Hapa ninapoishi ni mimi pekee ambae sina mke na nilishawahi kuleta uzi hapa ➡️ Thread 'Ninapoishi ni mimi pekee ambae sijaoa' Ninapoishi ni mimi pekee ambae sijaoa
Sasa imekuwa kawaida mwenye nyumba kunitania kila siku kwamba nioe (mwenye nyumba wangu ni mtani wangu kikabila). Maneno haya yamekuwa yakirudia kila wakti jambo ambalo linaanza kunifanya nione au ni kweli sasa napaswa kuoa.
Tuachane na hilo kuna mpangaji mwenzangu leo kanikuta nafanya zangu viusafi akanimbia "Kaka inabidi uoe sasa" huku anacheka (kiumri jamaa kanizidi na anaishi na pisi yake, jamaa ni dokta na pisi yake ni nurse). Me nikamjibu tu kwamba asijali siku akipatikana mwanamke sahihi kwa muda sahihi nitaoa.
Wazazi wangu hawajawahi kuniambia chochote kuhusu kuoa tena, mama ndio huniambia nitulize kiherere cha kuharakia me bado m-little.
Sasa maswali ninayojiuliza kichwani "Hivi ni kigezo kipi cha kuoa? Je, ni kwamba nina vigezo vyote vinavyoonekana ila mimi ndo nafeli au? Au je, ni kwamba ki-Africa kijana ukishakuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji yako muhimu unapaswa kuoa?
Au umri wangu ni mkubwa vya kutosha (naelekea 23 sasa)? Au ni kwasababu ya wanavyoniona najifanyia zile shughuli zangu kama kupika, kufua na kujioshea vivyombo vyangu? Au wanahofia nitatafuna pisi zao?
Ebu wakuu nishaurini hapa, hawa watu wakirudia tena haya maneno niwajibuje? Au kama ni kweli ni muda wa kufaa kuoa niambieni? Ila kiukweli kabisa najiona bado nauhitaji huu wepesi hadi baada ya kama 5 years + hivi maana nikiwa hivi naona inanifanya niwe mwepesi ku-risk maisha popote nitakapo.
Tiririka chochote chenye tija kunijenga.
Hapa ninapoishi ni mimi pekee ambae sina mke na nilishawahi kuleta uzi hapa ➡️ Thread 'Ninapoishi ni mimi pekee ambae sijaoa' Ninapoishi ni mimi pekee ambae sijaoa
Sasa imekuwa kawaida mwenye nyumba kunitania kila siku kwamba nioe (mwenye nyumba wangu ni mtani wangu kikabila). Maneno haya yamekuwa yakirudia kila wakti jambo ambalo linaanza kunifanya nione au ni kweli sasa napaswa kuoa.
Tuachane na hilo kuna mpangaji mwenzangu leo kanikuta nafanya zangu viusafi akanimbia "Kaka inabidi uoe sasa" huku anacheka (kiumri jamaa kanizidi na anaishi na pisi yake, jamaa ni dokta na pisi yake ni nurse). Me nikamjibu tu kwamba asijali siku akipatikana mwanamke sahihi kwa muda sahihi nitaoa.
Wazazi wangu hawajawahi kuniambia chochote kuhusu kuoa tena, mama ndio huniambia nitulize kiherere cha kuharakia me bado m-little.
Sasa maswali ninayojiuliza kichwani "Hivi ni kigezo kipi cha kuoa? Je, ni kwamba nina vigezo vyote vinavyoonekana ila mimi ndo nafeli au? Au je, ni kwamba ki-Africa kijana ukishakuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji yako muhimu unapaswa kuoa?
Au umri wangu ni mkubwa vya kutosha (naelekea 23 sasa)? Au ni kwasababu ya wanavyoniona najifanyia zile shughuli zangu kama kupika, kufua na kujioshea vivyombo vyangu? Au wanahofia nitatafuna pisi zao?
Ebu wakuu nishaurini hapa, hawa watu wakirudia tena haya maneno niwajibuje? Au kama ni kweli ni muda wa kufaa kuoa niambieni? Ila kiukweli kabisa najiona bado nauhitaji huu wepesi hadi baada ya kama 5 years + hivi maana nikiwa hivi naona inanifanya niwe mwepesi ku-risk maisha popote nitakapo.
Tiririka chochote chenye tija kunijenga.