Kwanini napinga mchakato wa Katiba Mpya ulivyo sasa na kwanini wewe pia yakupasa uupinge

No problem; ni mchakato wa CCM wa katiba mpya, wacha uendelee. Na kwa kuwa mchakato huu right from the begining ulishaonesha hautaleta katiba iliyokusudiwa, suala la Katiba Mpya ni endelevu regardless mchakato huu utazaa 'katiba mpya' ya aina gani. Itabaki kuwa ajenda ya kudumu hadi hapo Katiba Mpya ya Wananchi itakapopatikana na hili wala halizuiliki.

Haikuwahi kuwa kwenye Ilani wala ajenda za CCM, serikali nzima kuanzia mawaziri, Jaji Mkuu na watendaji wakuu wa CCM walikuwa wanapinga suala la katiba mpya mara ghafla kama vile wamekurupuka ndotoni wakaidaka ajenda na 'kuongoza' mchakato. Unategemea kuna kitu hapo? Another wastage of time and resources.

....Haikuwa ajenda ya CCM, JK wala serikali yake (Ushahidi upo). Hoja hii ni pandikizi kutoka kwa watu fulani wanaotaka kuutumia uwepo wake madarakani kuweka mambo yao sawa. Wamemtumia JK kwa sababu wanammudu. Dalili zote zipo wazi. Angalia mtiririko wa matukio tu utagundua. walianza na part one - kupitisha katiba ya Zanzbar inayoitambua Zanzbar kuwa ni nchi. part two tume iwe na wazanzbari na watanganyika nusu kwa nusu. Kuna strategy hapa - tusubiri part three. Ninachotabiri ni kuwa tume hii haitawagombanisha CCM na wapinzani, nahisi huko mbele hoja hazitakuwa CCM au CDM kwa kuwa naamini baadhi ya wanaCCM wataungana na wanaCDM na baadhi ya wanaCDM wataungana na wanaCCM hapo ndipo tutajua uamuzi wa ghafla kukubali kuunda katiba mpya ulikuwa wa nani, maana kwa hakika haukuwa wake.
 
inaweza kuonekana kuwa mchakato unapindishwa kwa makusudi lakini bado wananchi watakuwa na nafasi ya kutoa maoni yao kwa tume iliyoundwa.....kama itaonekana haikidhi haja iliyokusudiwa then wananchi watakuwa na nafasi ya kutoa kilio chao kupitia bunge la katiba(through the MPs)......kama itaonekana haikidhi then wananchi wana nafasi ya kutoa kilio chao kupitia referendum........na mwisho kabisa ili kumaliza mzizi wa fitna za CCM.. dawa ya mwisho na ya uhakika itakuwa kuwatoa CCM madarakani kupitia sanduku la kura mwaka 2015...ili CDM waendelee na mchakato wa kupata katiba yenye kukidhi matakwa ya watanzania wote......i think people should start to air their views strongly from now on.....to the very election day in 2015...hata kama watawala wamepanga hila...they can't go against PEOPLE'S VOICES every time.....experience has already shown us this.....
 
CDM ambao Katiba Mpya ilikuwa ni ajenda yao kuu 2010 wakakubali mchakato huu wakiamini ni wa ajili ya "maslahi ya taifa". Wakaubarikia na wakaamua kushiriki sasa wanaweza kuja baadaye na kutaka "mabadiliko". sasa hivi CDM wana option ya kuendelea kufanya "mazungumzo ya kuboresha mchakato" kwani option nhyingine pekee ni wao kujitoa kabisa na kuwataka wanachama wao wasishiriki; miaka mitatu si mingi. Kama watu wameweza kusubiri miaka 20 kupata Katiba Mpya wanaweza kusubiri miaka mitatu.

Lakini option nyingine - a technical one - ni kuwa CCM wakiendelea na kupitisha katiba wanayoitaka wao watakapokuaj kwenye kura ya maoni CDM watahamasisha wananchi kuivote down hiyo proposed constitution hasa kwa vile inahitajika 50 percent ili ikubalike.

Jamani nashukuru sana kwa mawazo mazuri, hivi kwahatua hii tuliyofikia hatuwezi kuweka pingamizi la Mahakama? Jamaa wameshaapishwa na kwamba wanaanza kazi tarehe 01.05.2012. Nini kifanyike haraka kuondoa au kurekebisha hili tatizo? Naona kama Watu wote tumeshakata tamaa kabisa. Hakuna njia nyingine yeyote?
 
Acha wajifurahishe kwa zoezi lao hili nasi tutafute 'sovereignty' ya nchi yetu kwanza then tutailinda hiyo kwakuiandikia katiba inayoendana na matamanio yetu tutakapo kuwa tume wang'oa hawa watu wasio na vision wala mission.
 
Mwanakijiji,
Msome pia Jenerali Ulimwengu kwenye makala zake ndani ya RaiaMwema. Hoja zenu zinafanana. Nisichokifahamu mimi ni kwa vipi na kwa namna gani mchakato huu ungeikwepa CCM, serikali yake na hata Bunge lake. Tungeanzia wapi? Hebu ngoja tuuanze mchakato wenyewe hivyo ulivyo. Naamini mpo watu kama ninyi, vipo vyama makini vya upinzani, zipo asasi makini zisizo za kiserikali na above all wapo WATANZANIA makini wengi tu kwa sasa. Tupate KATIBA MPYA. Mengine yote ikiwemo Tume huru ya uchaguzi yatatokana na KATIBA hii. Ilikuwa ni ndoto mwaka 1995 chama cha upinzani kushinda uchaguzi mdogo kama ule wa AruMeru Mashariki lakini sasa kwa Katiba hii mbovu imewezekana! Tusijikatishe tamaa.

Haya mawazo ndiyo hasa yanayowapa nguvu CCM kuendelea na huu mchakato, wanajua kuwa wao wakiwa strategists na kwakua watu wetu wengi siyo rational (so ni rahisi sana kutokuona picha kubwa mbele) huko mbele kuna mambo watayaburuza kama walivyo fanya kwenye sheria yenyewe na katiba hiyo waitakayo itakapo patikana watakuwa na miaka kadhaa yakuendelea kusukuma gurudumu lao la ubinafsi na uchakachuaji.....
 
CDM ambao Katiba Mpya ilikuwa ni ajenda yao kuu 2010 wakakubali mchakato huu wakiamini ni wa ajili ya "maslahi ya taifa". Wakaubarikia na wakaamua kushiriki sasa wanaweza kuja baadaye na kutaka "mabadiliko". sasa hivi CDM wana option ya kuendelea kufanya "mazungumzo ya kuboresha mchakato" kwani option nhyingine pekee ni wao kujitoa kabisa na kuwataka wanachama wao wasishiriki; miaka mitatu si mingi. Kama watu wameweza kusubiri miaka 20 kupata Katiba Mpya wanaweza kusubiri miaka mitatu.

Lakini option nyingine - a technical one - ni kuwa CCM wakiendelea na kupitisha katiba wanayoitaka wao watakapokuaj kwenye kura ya maoni CDM watahamasisha wananchi kuivote down hiyo proposed constitution hasa kwa vile inahitajika 50 percent ili ikubalike.

mm ww ni mtu usiyeridhika hata siku moja,ni mwenye chuki ya asili na huna nia njema na watanzania kwa sababu ww una enjoy huko utumwani.tuache tupate katiba mpya plz
 
MM ni mchochezi na ni looser,unajaribu kupotosha ukweli na utawapata wasioshughulisha akili zao kufikiri.

ww endelea kutumwa na mabwana huko uliko acha sisi tuijenge nchi yetu
 
mm ww ni mtu usiyeridhika hata siku moja,ni mwenye chuki ya asili na huna nia njema na watanzania kwa sababu ww una enjoy huko utumwani.tuache tupate katiba mpya plz

Of course mtapata katiba mpya usiwe na shaka hata kidogo.
 
Hoja yeyote yenye manufaa kwa Taifa ikiwekwa basi mwanakijiji lazima aponde,huyu anaonesha kuwa lolote atalozungumza JK yeye kwake si sawa.kama ni siasa haziendi hivyo ndugu yangu na kama una chuki binafsi na president hiyo ni yako binafsi acha tupate katiba mpya yenye manufaa kwa wananchi na si yenye manufaa kwa ajili yako na chama chako.
 
MM ni mchochezi na ni looser,unajaribu kupotosha ukweli na utawapata wasioshughulisha akili zao kufikiri.

ww endelea kutumwa na mabwana huko uliko acha sisi tuijenge nchi yetu

Mkuu tatizo ni nini hasa? Yaani kuunga mkono katiba mpya kutengenezwa na Baraza la Katiba ndio imekuwa uchochezi? Ukweli usiopingika ni kwamba katiba huwa zinatengenezwa na Baraza la Katiba, sio tume (Commissions). Kawaulize hata maprofesa wa constitutional law watakuambia hivyo hivyo, unless nao ni wachochezi.

Kama unatoka from the elite group nitakuelewa unaposema ni uchochezi kwa sababu hakuna elite ambaye atakubali kumpa mwananchi wa kawaida uwezo wa kujitengenezea katiba yake.

Hoja yeyote yenye manufaa kwa Taifa ikiwekwa basi mwanakijiji lazima aponde,huyu anaonesha kuwa lolote atalozungumza JK yeye kwake si sawa.kama ni siasa haziendi hivyo ndugu yangu na kama una chuki binafsi na president hiyo ni yako binafsi acha tupate katiba mpya yenye manufaa kwa wananchi na si yenye manufaa kwa ajili yako na chama chako.

Mkuu unaweza kutuambia kwa nini tume na sio baraza la katiba ndio chombo muhimu cha kutengeneza katiba mpya? Why tume? Why not Baraza la Katiba?
 
Mkuu tatizo ni nini hasa? Yaani kuunga mkono katiba mpya kutengenezwa na Baraza la Katiba ndio imekuwa uchochezi? Ukweli usiopingika ni kwamba katiba huwa zinatengenezwa na Baraza la Katiba, sio tume (Commissions). Kawaulize hata maprofesa wa constitutional law watakuambia hivyo hivyo, unless nao ni wachochezi.

Kama unatoka from the elite group nitakuelewa unaposema ni uchochezi kwa sababu hakuna elite ambaye atakubali kumpa mwananchi wa kawaida uwezo wa kujitengenezea katiba yake.



Mkuu unaweza kutuambia kwa nini tume na sio baraza la katiba ndio chombo muhimu cha kutengeneza katiba mpya? Why tume? Why not Baraza la Katiba?


Why not tume?
 
David Webb wewe ni lateral thinker, you think out of the box, hivo kwa mtu anayefikiria kwa kina kwako ni mchochezi but ukweli ndo huo alousema MMM. Jamani watanzania tuamkeni ili kazi isonge mbele kwa vizazi vyetu vijavyo. Tunataka Tanzania isibaki hii hii hata miaka mia ijayo, kwani lazima watoto na vitukuu vyetu vije kuishi mahali salama penye kila aiana nzuri ya huduma.
 
Wao waendelee tu na machakato, ninachokijua toka mwanzo ni kuwa CCM hawajawahi kuwa na ajenda ya katiba mpya, na kwa kweli hawawwezi kuleta katika ya kweli kwa sababu wanajua it is a suicidal to them!! Umungu mtu, kiburi, wizi, ufisadi, ni maneno mabaya sana kwa watu wasafi wenye kujali utaifa na watu wake!! Kwa wana CCM haya ni maneno mazuri tu, yaliyotungiwa majina mazuri sana, yenye kuendelezwa na kuwalinda "wenzetu" na maslahi ya chama.

Mchakato uende tu, kwani haizuii hapo baddaye kuuanzisha pia. Ninachoomba saaaaaana na CC na NEC ipitishe mgombea tofauti na mnywele ambaye najua kwa sasa analala na kuuota URAIS, wakifanya hivyo, ni manywele ndiye atakaye vunja CCM in pieces, na chama cha upinzani kuchukua nchi!! Haya yalitokea Kenya na amini nawaambie yatatokea hapa.
 
Mwanakijiji,

Barvo!

Hapo kwenye mamlaka ya wananchi pako wazi kabisa tangu mwanzo.Ukiangalia mchakato ulivyo kwa nchi zote zinazojivunia katiba bora kama India,Ghana,Uswisi na US maamlaka ya umma yalitamkwa na yakaonekana kushirikishwa kabisa kwenye mchakato.Katiba ya Us imeweza kudumu kwa muda wa zaidi ya miaka 200 na ammendments takribani 26 tu.Katiba hiyo iliyobeba maono ya mudfa mrefu iliweza kuhimili Vita kuu ya Dunia,Mtikisiko wa Uchumi (1930's),Vita kuu ya Pili,Cold war,Post cold war,Utandawazi n.k kwa amendments chache tu.sisi tunatunga katiba kuangalia maslahi binafsi na matamanio ya chama cha siasa.nonesense!

Huu mchakato tangu mwanzo tulijadili kwamba njia hii siyo sahihi.Tutatumia nguvu nyingi tuishie kupata matokeo yanayolingana na cosmetic amendments tu.Wacha nitafute ile thread

Ndiyo maana niliona vituko kweli tarehe 6 April Rais alipotangaza majina ya wajumbe.Tatizo na sisi emotions zinatuzuia kuwa objective tunashangilia vitu ambavyo hatujavielewa
 
Tatizo ninaloliona ndani ya CCM hakuna mwenye maono ya mbele sight zao zinaishia kwenye vitambi vyao na hawapendi kushughulisha ubongo.
 
Mi sioni shida ya wingi wa waislam ili mradi hawana dhamira ya dini zao.mkt na makamu wake ni wakristo mmesahau? tusibaguane kwa udini hata kwnye mamb yasio ya lazima
 
Back
Top Bottom