Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
KWANINI MWANAMUME AKIFA NDUGU WA MWANAMUME WANADAI MALI ZA MTOTO WAO HATA KAMA ANA WATOTO KWA NINI NDUGU WA MWANAMKE HAWANA HAKI YA KUDAI?
Mimi ni mwanamke niliyeolewa nimekuwa nikiona matukio mengi hasa upande mmoja wao anapoitwa mbele za haki na Baba yetu wa Mbinguni. Nitaongelea upande wa mwanamume mara nyingi nimekuwa nikiona tofauti sana na kujiuliza ni kwanini inakuwa hivyo?
Ikitokea mwanamume akafa utakuta ndugu wa waupande wa mwanamume wanaanza kudai mali alizochuma ndugu yao hata kama ana watoto na mke aliyebaki hawaangalii hilo wao ni mali tu sababu mtoto wao ndo alikuwa mtafutaji. Hawakumbuki kuwa wakati wanatafuta hizo mali alikuwa na mke wake wanashauliana saa nyingine wanajima vitu Fulani Fulani ili wawe na maendeleo kama watu wengine. Chakushangaza mke athaminiwe tena hasa akiwa na watoto wadogo ndo basi make wakiwa wakubwa kunakuwa na hofu kidogo lakini maneno hayatakosa, utakuta wakati wanaoana walikuwa hawana kitu hata kimoja lakini wakajibana wakapambana na maisha wakawa na kitu kidogo lakini walijibanaje wanajua wao hasa mama na baba sasa kwa nini inapotokea baba akaondoka kunakuwa na vurugu hasa kuhusu mali?
Niongelee tena upande wa mwanamke inapotokea mama ameitwa mbele ya haki kwanini ndugu upande wa mwanamke hawana haki ya kudai mali ya mtoto wao aliyochuma na mume wake? Sababu mali alizobaki nazo mwanamume zilitafutwa na wote wawili sasa kwa nini haki iende upande mmoja? Naomba kujua hilo toka kwa wadau. Ikumbukwe mwanamke anapokufa baba ana haki ya kuoa mke mwingine na kumuolea kwenye nyumba aliyojenga na mke wa kwanza na wakaendelea na maisha lakini anapokufa baba mwanamke haruhusiwi kumiliki tena mali za mume wa kwanza kwa nini? Na tujue asilimia ya wengi hasa mama akifa wa kwanza watoto huwa wanapata shida sana na utakuta matunzo ya watoto yanaegemea upande wa mama tofauti na upande wa baba na utakuta watoto wanadhulumiwa hasa na upande wa baba ni kwanini?
Mimi nashauri wanapotunga katiba nahili waliangalie hasa upande wa mwanamke wawe na haki ya kudai mali endapo mtoto wao ametangulia
Mimi ni mwanamke niliyeolewa nimekuwa nikiona matukio mengi hasa upande mmoja wao anapoitwa mbele za haki na Baba yetu wa Mbinguni. Nitaongelea upande wa mwanamume mara nyingi nimekuwa nikiona tofauti sana na kujiuliza ni kwanini inakuwa hivyo?
Ikitokea mwanamume akafa utakuta ndugu wa waupande wa mwanamume wanaanza kudai mali alizochuma ndugu yao hata kama ana watoto na mke aliyebaki hawaangalii hilo wao ni mali tu sababu mtoto wao ndo alikuwa mtafutaji. Hawakumbuki kuwa wakati wanatafuta hizo mali alikuwa na mke wake wanashauliana saa nyingine wanajima vitu Fulani Fulani ili wawe na maendeleo kama watu wengine. Chakushangaza mke athaminiwe tena hasa akiwa na watoto wadogo ndo basi make wakiwa wakubwa kunakuwa na hofu kidogo lakini maneno hayatakosa, utakuta wakati wanaoana walikuwa hawana kitu hata kimoja lakini wakajibana wakapambana na maisha wakawa na kitu kidogo lakini walijibanaje wanajua wao hasa mama na baba sasa kwa nini inapotokea baba akaondoka kunakuwa na vurugu hasa kuhusu mali?
Niongelee tena upande wa mwanamke inapotokea mama ameitwa mbele ya haki kwanini ndugu upande wa mwanamke hawana haki ya kudai mali ya mtoto wao aliyochuma na mume wake? Sababu mali alizobaki nazo mwanamume zilitafutwa na wote wawili sasa kwa nini haki iende upande mmoja? Naomba kujua hilo toka kwa wadau. Ikumbukwe mwanamke anapokufa baba ana haki ya kuoa mke mwingine na kumuolea kwenye nyumba aliyojenga na mke wa kwanza na wakaendelea na maisha lakini anapokufa baba mwanamke haruhusiwi kumiliki tena mali za mume wa kwanza kwa nini? Na tujue asilimia ya wengi hasa mama akifa wa kwanza watoto huwa wanapata shida sana na utakuta matunzo ya watoto yanaegemea upande wa mama tofauti na upande wa baba na utakuta watoto wanadhulumiwa hasa na upande wa baba ni kwanini?
Mimi nashauri wanapotunga katiba nahili waliangalie hasa upande wa mwanamke wawe na haki ya kudai mali endapo mtoto wao ametangulia