Kwanini Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tanzania 2015

Kuliko kikwete,sita yaani ndani ya ccm lowasa is the best candidate,seriously i say,wengine wote wanafiki
 
Ungejua uchafuzi na mchezo wa jk towards 2015 ndiyo utajua lowassa si mchafu kiasi hicho he is the best,kiongozi anaweza onyesha mamlaka aliyopewa kuliko kuonyesha meno na wengine kujipendekeza
 
Jairo kasafishwa karudi karudi kazini. Lowasa alitoswaa? mbona tuhuma za lowasa hazikuwa na mshiko wowote? nani aliyejitokeza hadharani na kutamka bayana kuwa zile 154,000,000 za Richmond zilikuwa ni service charge tu? na makampuni mengine yanapata kubwa zaidi ya hizo, who came out? who explained this????? why now? Au jamaa anatisha eeh. Go Lowasa Go
 
Hivi EL ataendelea kuteseka na kinyongo moyoni mpaka lini? Kwani asije front akawambia watanzania A-Z ya maroroso yoooote ya JK na walivyokuwa wakifanya madudu yao. Hiyo pekee ndiyo itatuthibitishia kuwa EL ni msafi na kupata tena kura yangu
anasubiri wakati wa kampeni usidhani ye mjinga unadhani kwa nini ccm wenyewe wamefyata mkia kwa EL????
there is something behind
 
kwa mliotumwa na huyu baba au vibaraka wa karibu wa huyu baba, habari ni hii: yawezekana ana mazuri yake, ila tukiweka kwenye mizani na tukapima hayo mazuri na mabaya, bakuli la mabaya yamkini ni zito zaidi. Sasa basi, tunamshukuru kwa jitihada zake mbali mbali za kusogeza maendeleo katika nchi yetu lakini hatuko tayari aongoze nchi yetu kwasababu yaonesha si mwepesi kuzuia tamaa zake. Pia si vema, kujiaminisha kuwa awezaye kuongoza nchi ni fulani tu kana kwamba kuna sauti ilitoka mbinguni na kutuambia hivyo, kama wakati Yohana mbatizaji akimbatiza Yesu.
Sina ill-feelings na Lowassa na ninamuunga mkono kwenye utumishi wake kwa wana-monduli
 
anafaa mara kumi elfu ya jk, ila ukimpambanisha na slaa kazi anayo
 
Ukimpambanisha na nani?CDM wanajua EL ndiye mgombea aliyebaki mwenye Nguvu nyingi ndani ya Sisiem kuweza kutoa Upinzani Mkali na kuingangusha kambi ya Upinzani ndio maana wanamwandama ili sisiem wamtose....Mimi nasema EL asimamishwe na ataiangusha kambi ya Upinzani..

Kwa Upande wa Dr.Slaaaaa,mimi sina neno naye,na yeye ni Smart sana,mzee yule mimi namkubali sanaaaaa,ana uwezo kwakweli,mtu yoyote aliye na Elimu Kichwani ya Kutosha,hata kama Hana Elimu anamkubali.But he is not Experienced like EL,kwa maoni yangu Slaaaaa hana uzoefu wa kutosha katika Siasa na Uongozi kama EL. Haya ni maoni yangu.


EL GO go GO gooooooooooooooooooooooooo
 
Mods ondoeni thread hii, inaidhalilisha JF kana kwamba inawafanyia kampeni mafisadi.Nawasilisha.
 
ltanzania imekuwepo kabla ya lowasa na itakuwepo baada ya lowasa,anapigiwa debe kama mungumtu,mod ondoa upuuzi huu kwenye jukwaa.
 
Nakuonea huruma sana wewe unayesema Thread hii ifutwe, unaonekana namna ulivyo FIRSIKA kimawazo sana,kama huna hoja waache wenye Hoja waseme,kwa Taarifa yako ni kwamba wanadamu hatupo sawa,kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake na ndio maana Jamii Forums imejipatia Heshima kubwa sana Tanzania na Duniani kote,hatuwezi kusema mambo ambayo wewe tu ndo unataka kuyasikia,kila mtu ana akili zake na Utashi wake,thats why si busara kupinga wazo la mtu humu.

Leta Hoja kama unayo ndugu yangu,Leta ushahidi kama unao wa kuweza kupinga Hoja iliyowasilishwa,Ofcoz mimi sipo hapa kumtetea wala kumjenga mtu hapa,nimewasilisha Hoja na kila mwenye Mchango atachangia.

Hatuwezi kujenga Nchi ya Majungu jamani,kama una HOJA lete na wana Jamiii wataipima na Kama una Ushahidi pia ulete hapa tuuone na si kukimbilia Majungu jamani,hii sio Forum ya Majungu.

Katiba ya Tanzania ipo na Sheria zipo,Bunge lipo na Mahakama zipo,lete HOJA hapa Bwana,kama huna Hoja,umefirisika mawzo na endelea kuwa mtazamaji tu.

Karibuni katika Sehemu ya Pili ya Hoja iliyowasilishwa hapa ,''Kwanini EL anafaa kuwa Raisi wa Tanzania?'' kuanzia January 2012 mada hii itarushwa hapa tena,msikose!!!!
 
Sasa kazi imeisha kukamilika,Habari zilizotufikia zinasema,Kundi la Wabunge wafuasi wa EL wamekamilisha Ushahidi na Nyaraka zote kuhusu Sakata linalomkabili aliyewashi kuwa Spikaaaa wa Bunge letu la Tanzania Mhhhh.Pyuuusi Msweeekwa na zitawsilishwa kwenye kikao cha NEC mwezi Ujao.Wabunge hao wakiongozwa na Mbunge mwanamke aliyetokea kuwa machachari sana wameapa kwamba siku ya kikao Hicho na Mh.Msweeekwa nayeye atang'olewa madarakani kabla hajaanza kuendesha kikao Hicho.

Wachunguzi wa masuala ya Kisiasa wanasema,Kutakuwa na MALUMBANO makali kati ya Wafuasi Wabunge ambao ni Wafuasi wa EL na Kambi ya Wavua Magamba inayoongozwa na '' Naye Huyooo Peke yakeee'' na wamemwonya Mwenyekiti kujiepusha Mbali na Makamu wake huyo ili kuzuia Malumbano makali ya Kambi hizo.

EL ,Moja ya Wanasiasa Jabali na Kisiki ndani ya Sisiema,ameapa kwamba atafichua kile kinachosemwa na wengi ''SIRI NZITO'' na huenda pakatokea Patashika na Ghasia kubwa sana siku ya kikao hicho..

Karibuni
 
Kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake kwa mujibu wa mawzo yake kwakuwa ana utashi wake binafsi so naomba nitoa mtizamo wangu na sitatoa maoni ili kumfurahisha mtu humu ndani ya Forum ni maoni yangu na nina haki ya kuwa tofauti au sawa kimawazo na mtu yoyote.EL anaifaa Tanzania kwa sababu zifuatazo:-

Ni Kiongozi huyu shupavu,jasiri na mwenye ushawishi mkubwa ndani ya chama na serikali kwa upande wa serikali hili linadhihirika aliposhika nyazfa mbali mbali kama:-

a.Kusimamia Sekta ya Elimu ambayo ndiyo Uti wa mgongo wa maendeleo ya Taifa lolote hapa Duniani.Alisimamia kwa ukakamavu kutekeleza mpango wa kupanua Elimu ya Sekondari na alihimiza kwa nguvu zake zote ujenzi wa Shule za Kata Nchi nzima ili kuwapa Fursa Mamilioni ya Watanzania wenzetu waishio Vijijini kupata Fursa ya Elimu.

Zoezi hili lilihitaji uwekezaji mkubwa sana na Tukumbuke kwamba Taifa letu ni Maskini sana,changamoto zilizo ikabili Sekta ya Elimu kama Ukosefu wa vifaa vya maabara,Nyumba za Walimu,Madarasa ya Kutosha na upungufu wa Vitabu si kosa la mtu Fulani bali umaskini wa Taifa letu ndio maana WB na IMF hutoa misaada kwa nchi maskini kusaidia maendeleo ya Elimu kwakuwa ni Sekta inayohitaji uwekezaji mkubwa kifedha na Rasilimali zingine.

EL ni mtu anayeamini katika Elimu ndi maana motto wake ni tofauti kidogo na Motto wa Chama chake na anasema '' ELIMU KABLA,KILIMO KWANZA'' Ni kweli kabisa kwamba hakuna linaloweza kufanikiwa bila Elimu,Unaweza kuwaambia watu wasio na Elimu ya kutosha Walime Kilimo cha Kisasa?Me I agree kwamba Elimu KABLA na Kilimo Kwanza.

Mataifa Makubwa yaliondelea leo Duniani yalifanya uwekezaji Mkubwa kwanza katika Elimu,hasa Elimu ya Msingi(Kwa mfano China,Brazil na USA) na Baadaye kufanya Mapinduzi Makubwa ya Kilimo,baadaye Viwanda Vidogo na baadaye Viwanda vikubwa ambavyo vilichochea kukua kwa kasi kwa Sekta za Huduma na kupelekea mfumuko wa nafasi kibao za ajira kwa Vijana!!!

b.Kuwafukuza bila woga hadi kuwasindikiza Airport wawekezaji wababaishaji wa Kampuni ya City Water hadi kuwapandisha ndege uwanja wa
Taifa:

Akiwa Waziri wa Maji na Maendeleo ya Mifugo ,EL alitekeleza wajibu wake kwa umahili mkubwa na bila uwoga na moja ya mambo ambayo yatakumbukwa ni kufukuzwa kwa wawekezaji wababaishaji wa Kampuni ya Kitapeli ya City Water ambao walishindwa kutekeleza wajibu wao,aliwatimua na kuwasindikiza hadi Airport!EL ni Kiongozi Shupavu sana na asiyeogopa mtu!

c.Kiongozi Mwajibikaji na asiyeogopa kufanya maamuzi magumu hata kama yatamuuza

Kujiuzulu kwake kutoka katika Wadhfa wake wa Uwaziri Mkuu kufuatia Kashfa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond inachukuliwa na wengi kama kuhusika kwake katika Saga hilo.Napenda kuwakumbusha Watanzania wenzangu kwamba Waziri Mkuu ndiye mtendaii Mkuu wa Shughuli za Serikali na mtekelezaji wa Maagizo ya Baraza la Mawaziri ambacho kimsingi ndicho chombo kikubwa cha Utendaji wa serikali (Govt. Machine) na hivyo kama kuna Kosa linafanyika basi Linatosha kuiangusha Serikali nzima so katika SAGA ile ilibidi Serikali Nzima akiwa ni Pamoja na Rais wajiuzuru lakini EL akubali mwenyewe kwa ajili ya kulinda heshima ya Chama chake na Serikali, huu ni mfano mzuri wa kuigwa kwa Waafrika wote.

Siku zote tatizo letu waafrika ni kukosa kuwajibika pale inapobainika uzembe umefanyika,ukweli umebaki kuwa wazi mpake leo hii NCHI IPO GIZANI migao ya Umeme inaendele kama kawaida na dada wa Richmond ambaye ni Dowans Mitambo yake inawashwa na tumerudi pale pale!! Mimi nasema kwa kosa la Richmond,Serikali nzima ilikuwa imeanguka.

d.Mfuatiliaji na asiyechoka kufuatilia kero za na hakai ofisini kungoja taarifa
Wakati wa janga la Njaa lilisababishwa na ukame kwa msimu wa mwaka 2007/08 ni huyu EL alikuwa akishirikiana na Wakuu wa Wilaya zote zenye njaa na wakati mwingine alishiriki yeye mwenyewe kupita nyumba kwa nyumba kusimamia zoezi la ugawaji wa chakula kwenye Familia zenye njaa ili kuhakikisha kwamba azma ya serikali ya kwamba hakuna mwananchi atakayekufa kwa njaa inatimizwa ni huyu huyu EL.


Mtu hawezi kukosa mapungufu hata siku moja,nakubali ana mapungufu yake lakini EL ni embe dodo lililoiva tayari kuvunwa na Watanzania Mwaka ukifika 2015.


Nawaleteeni EL

Umesahau ni yeye aliyewanyang'anya visiwa watu waliokuwa wamemilikishwa visiwa vidogo vidogo katika bahari ya Hindi enzi za awamu ya pili. Alipopewa tu uwaziri wa ardhi akatangaza kuvirudisha serikalini visiwa vyote
 
Sasa kazi imeisha kukamilika,Habari zilizotufikia zinasema,Kundi la Wabunge wafuasi wa EL wamekamilisha Ushahidi na Nyaraka zote kuhusu Sakata linalomkabili aliyewashi kuwa Spikaaaa wa Bunge letu la Tanzania Mhhhh.Pyuuusi Msweeekwa na zitawsilishwa kwenye kikao cha NEC mwezi Ujao.Wabunge hao wakiongozwa na Mbunge mwanamke aliyetokea kuwa machachari sana wameapa kwamba siku ya kikao Hicho na Mh.Msweeekwa nayeye atang'olewa madarakani kabla hajaanza kuendesha kikao Hicho.

Wachunguzi wa masuala ya Kisiasa wanasema,Kutakuwa na MALUMBANO makali kati ya Wafuasi Wabunge ambao ni Wafuasi wa EL na Kambi ya Wavua Magamba inayoongozwa na '' Naye Huyooo Peke yakeee'' na wamemwonya Mwenyekiti kujiepusha Mbali na Makamu wake huyo ili kuzuia Malumbano makali ya Kambi hizo.

EL ,Moja ya Wanasiasa Jabali na Kisiki ndani ya Sisiema,ameapa kwamba atafichua kile kinachosemwa na wengi ''SIRI NZITO'' na huenda pakatokea Patashika na Ghasia kubwa sana siku ya kikao hicho..

Karibuni

Sisiemu pambalamaa,.... sisiemu pambalamaa
Kocheleni sisiemu eeh,... kocheleli sisiemu pambalamaa,
ama kocheleni Sisiemu eeh, ama kocheleli sisemu pambalamaa,...
sisiemu pambalama kocheleli sisiemu eeh
Kocheleli sisiemu pambalama...ama kocheleli sisiemu eh

Binafsi sijui ni kilugha gani, lakini nakumbuka miaka ya '70 wimbo huu ulikua maarufu sana
kwenye redio mkulima. Watu walikua na fikra za kimapinduzi za kujikomboa kutoka kwenye
utegemezi. Haikuwahi kufikiriwa eti kutakua na watu(tena wajumbe wa vikao nyeti) wanunuliwe
na mtu mmoja, kwa nia ya kwenda kujidhalilisha na kuuza utu wao kwa sababu ya pesa.

Hii ndio ilikua CCM ya Mwalimu. Chama ambacho maadili yaliheshimiwa na kusimamiwa. Asiyetaka
aliambiwa wazi usoni kuwa wewe sasa umekua mzigo, tupishe!

Enzi hizo hata shutuma ya kuwa fisadi ilitosha kukutimua kwenye nyadhifa zako zote.

Leo hii ni kama Chama kinaelea tu... mafisadi wameshika hatamu. Na wamenunua na midomo ya
kuwasemea kwenye vikao vya maamuzi wao wenyewe wakiwa kimya. Nchi imefikia pabaya sana...

Lowasa hebu kaa pembeni uinusuru nchi yako kama kweli unamapenzi ya dhati na nchi hii. Hii hali
ya kutaka mapambano yasiyo na tija ni kutokana na wapambe wako wengi hawana ajira wanauza
maneno na kuchonganisha watu ili waishi mjini.

Hivi Urais ni kitu gani mpaka usakamwe wewe tu? Au kuna biashara umepania kuifanya ukifika IKULU?
Yasije yakawa yaleyale ya JK yanajirudia, tumeona vyeo kwa kulipa fadhila, nawewe Lowasa je hayo mabilioni
na hilo kundi kubwa lote likifanikiwa kukuingiza IKULU tutegemee nini? Hasa ikizingatiwa linaratibiwa tena
na Rostam... GOD PLEASE SAVE OUR BELOVED MOTHERLAND!
 
Kundi la Wabunge wafuasi wa EL tena kwa mara nyingine tena limefanikisha adhma yao ya kuiyumbisha sirikali katika kile kinachoelezwa na wapambe wa Kiongozi huyo kuwa utekelezaji wa Kauli yake wakati akijiuzulu mwaka 2008..

''NANI ATASIMAMA''

Kundi la Wabunge hao liliamka kwa hasira na kuamrisha JD kurudishwa kifungoni ili kupisha Uchunguzi wa Kadhia yake unaofanywa na Kamati Teule ya Bunge,katika kile kinachoelezwa na wengi kwamba ni kukaribia kufumuka kwa ''SIRI NZITO'' huenda kuundwa kwa Kamati hiyo kukapelekea kufumuliwa kwa mambo mengine mengi zaidi na zaidi wakati wa Uchunguzi huo.

Kwakweli EL ni Kiongozi Shupavu na mwenye mtandao mkubwa sana ndani ya chama na sirikali,nguvu yake kubwa na ushawishi alionao ndani ya chama kwa sasa ni wazi kwamba ndio unaotawala sasa.

Hali inazidi kuwa tete huku Wabunge wafuasi wa EL wakiwa wamekamilisha mikakati yao ya kutikisa Sirikali kwa kufanya yafuatayo mara tuu baada ya Hotuba ya ''TANZANIA INAJUA,DUNIA INAJUA'' wakati wa kikao hiki cha Bunge linalomalizika leo.

1.Kushawishi kukataliwa kwa Bajeti ya Wizara ya Nishati

2.Kukataliwa na kushinikizwa kuongezwa kwa Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi ili kutekeleza Agizo la EL la kutaka Sirikaliii kufanya maamuzi magumu na kufufua Bandari kuu na Reli

2.Kumdhoofisha Makami mwenyekiti kwa kufichua maovu yake ambayo yamemny'onyeza na kumpunguzia mvuto kwa wana Sisiem wakati wa kuelekea kikao cha NEEC mwezi September,sasa Spiika huyo wa zamani ameshavikwa jina la GAMBA jipya

3.Kushinikiza JD kurudishwa Likizo ya bila malipo baada ya kusafishwa na CAAAG na Ikuuuuluuuu

4.Kumshawishi RA ajiuzulu ili kukipatia chama wakati mgumu wa kutete Jimbo kwa Uchaguzi na hivyo kijisahau kushughulikia mambo ya msingi ,kama kujivua Gamba

Wafuasi hao wa EL Wameapa kuendelea na harakati zao kufa na kupona na wanamshihikiza EL kutoa kile kinachoitwa ''SIRI NZITO'' kwa wanachi woote wa Tanzania.

Habari zinasema kwamba katika mkakati huo wa wafuasi wa EL,vyombo vya Habari vya magazeti ya DIRA na TBC vimechaguliwa na wajumbe wa Kamati Teule ya Wabunge wafuasi wa EL kutumika katika harakati zao..

Nawasilisha
 
Namkubali sana Mshikaji..Ni kweli kila mmoja na mtazamo wake..mwingine atasema hasafishiki..mwingine atahoji kwanini Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tanzania ? Kimsingi hakuna aliyepangwa kuwa Rais,.Makamu wa Rais.,Waziri mkuu.,Waziri.,Mkuu wa mkoa,Mkuu wa wilaya.,Mbunge.,Diwani,Mwenyekiti wa mtaa/Kitongoji n.k bila jitihada zake binafsi pamoja na mambo mengine.Labda niseme kwamba.,sina maslahi na chama chochote cha siasa,wala mtu yeyote..natoa maoni yangu kama wadau waliotangulia hapo juu na nikiwa mtanzania huru.,siipendi siasa kutokana na haya yanayojiri kuihusu siasa.,lakini naifuatilia sana ukichukulia kwamba siasa ndio inayoongoza Dunia.Lowassa alifanya uamuzi mgumu sana kujiuzuru kuinusuru Serikali na Chama Chake,inawezekana alijua consequences zake,na labda amesalitiwa;kama kuna lolote analolijua(Siri) aitoe ili apate relief ,nionavyo mimi kwake Lowassa SIASA ni YEYE na YEYE ni SIASA.,hivyo basi kama anafikiria kuwa anafanya jitihada zozote za kuwa Rais wa Tz hapo baadae..aendelee na jitihada kwani hayo ndio maisha aliyochagua(SIASA)...Kumbuka lowassa binafsi utendaji wako nilikuwa naupenda sana ulikua unaendana na kasi ya vijana..Thinkers!..Jacob Zuma alikua na Scandal ya Uzinzi kabla hajawa Rais wa South Africa..ultimately ndie Rais wa sasa wa nchi ya MADIBA...tueleze siri Lowass tutakuunga mkono....Ni mawazo yangu...Dr Know how.
 
Back
Top Bottom