Kwanini kufufua Air Tanzania kwa fedha zetu wenyewe badala ya ubia?

Huo ni uchambuzi wako wa kitaalamu kiuchumi au nawe unasukumwa na hisia za kisiasa.

Moja ya vichocheo vya kukua kwa uchumi ni ubora, uimara na uwezo wa miundo mbinu. Mali yoyote haina thamani kama jinsi ya kuifikia ni shida.

Kwafano kilimo hakitakuwa na tija kama mazao hayataweza kuondolewa mashambani na kufikishwa sokoni kwa wakati na ubora ule ule. Vivyo hivyo mbuga zetu hazina thamani kama hakuna njia rahisi (kwa gharama ndogo na uhakika, nk) ya kuzifikia. Mfano ni Kisiwa cha Rubondo, Ziwa Victoria, Mkoa wa Geita, ambacho kina kila aina na sifa za utalii wa samaki na ndege. Je, nani anakifahamu. Na anayekifahamu kufika huko ni shida. Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Chato unabezwa, kwa sababu tu ndio kwao na Rais!

Safi ni mwendo wa nondozz ndio raha ya JF ....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hayo mapendekezo yako ni sahihi lakini bila usafiri wa uhakika tutakosa advantages nyingi. Kama watalii wangeweza kufika direct K.I.A bila kupita Nairobi gharama ingekuwa chini na kuvutia wageni zaidi Tanzania kuliko Kenya.

Mkuu, siyo kweli kwamba ndege direct ni gharama nafuu kuliko ndege za kuzunguka. Mara nyingi direct flights ni gharama kuliko ruti za kungukuza. Hata sasa hivi ukienda Google flights kafanye utafiti. Gharama za kuja Bongo (Dar na KIA) kutoka JKF, kwa mfano, ni kubwa kuliko kwenda Nairobi. Gharama ya kutua kwenye uwanja/nchi yoyote inazingatia vitu mbalimbali ikiwemo kodi katika nchi hizo. Je, Tanzania kodi zetu za kutua na kutua kwenye viwanja vyetu ni vipi?

Tatu, kuna suala la brand recognition. Watalii wengi hawaanzi Bongo ambako tuna allegiance na ATCL. Mfano, mtalii kama anatoka Uholanzi na bei kati ya ATCL na KLM ni sawa, unadhani atapanda ndege ipi?

Tukubaliane kwamba tunafufua ATCL kwa sababu na sisi tunataka kudandia #MeToo movement ya nchi za Kiafrika, ila siyo kupanua utalii. Takwimu zinaonesha watalii wameongezeka Bongo wakati ATCL ni mfu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu,

Nilikuwa nikifuatilia ziara ya Uhuru Kenyatta huko U.S.A na moja ya kitu kilichonivuta ni message iliyotolewa na BBC kuwa Kenya Airways wataanza route za moja kwa moja kwenda New York kuanzia October 2018.Kwa ufupi shirika la Kenya Airways limekuwa sehemu ya msingi wa uchumi wa Kenya hasa multiplier effects zake hata kama shirika hilo linaendeshwa kwa hasara. Hata sisi Tanzania kwa kipindi kirefu tumetegemea sana shirika hili kama kiungo cha kibiashara na utalii.

Shirika letu la Air Tanzania limepitia mapito mengi mabaya yakichangiwa na utawala mbovu, kukosa uzalendo n.k moja ya juhudi kulikwamua shirika hili ilikuwa ni kuingia ubia kupitia South Afica Airways ambapo pia hali ilizidi kuwa mbaya Zaidi na ubia kufa huku shirika likibakia na madeni yasiyolipika.

Shirika hili lilikuwa haliuziki kwa namna ambayo taifa lingefaidika sasa wala usoni. Hakuna mfanyabiashara ambaye angeweka pesa zake kwenye shirika lililokuwa na hali ya kiwango hiki. Kutokana na umuhimu wa shirika la ndege la taifa kwa manufaa ya Taifa Mh Rais JPM akaona tutumie fedha zetu kurudisha shirika hili kuweza kujimudu na kuweza kuendesheka hata kwa ubia miaka ya usoni.

Hivi kweli wale wanaobeza juhudi hizi walitaka kazi hii ifanywe na Precision Air, Fastjest? Hivi kwa hali ya ushindani wa uchumi kwa nchi zetu hizi tuendelee kutegemea watalii wanaopitia Kenya kwa asilimia karibia zote? Kwanini tusianze wenyewe kwa manufaa ya vizazi vijavyo? Kwanini tunabeza kila jambo hata vitu vyenye manufaa kwa Taifa?

Inawezekana kuna vitu havitupendezi hasa hali ya kisiasa lakini tusisahau kuna Taifa, kama yupo anayechoma nyumba kwa moto wa kiberiti tusimwagie petrol kuuzima. Vipo vizazi vitatushangaa sisi tunaoishi leo hata kama wewe si mwanasiasa. Hii beza beza kila kitu ipo siku nchi itavamiwa alafu tuanze kubezana kisiasa! Tuchore mstari kwenye mambo ya kitaifa ili hata hawa viongozi wetu wasipoheshimu katiba yetu tuwe na uwezo wa kuwakemea na kila mtu akaelewa badala ya sasa kila jambo kubeba sura ya kisiasa.

Hapa chini nimeweka orodha ya mashirika ya ndege makubwa Zaidi barani Afrika na airline holding (source ni Wikipedia) ili tujue tupo kwenye ushindani gani na kama tupo sahihi kufanya juhudi hizi.

Please note; Huu ni Mtazamo binafsi kama Mtanzania wa kawaida ambaye sina uzoefu wala utaalamu wa airlines business.


View attachment 849379
Watalii ambao wanakuja kenya tanganyika na zanzibar huwa hawatumii mashirika ya kiafrika . Hao kenya wanafanya Safari kwa miaba ya KLM kule europ . Unakata tikeki ya KLM unapandishwa kenya Air . Wazungu hawayaamini mashirika ya Afrika . Wanatumia ya kwao au ya waarabu . Hiyo ethiopia basi hawaiamini vizuri
 
Huo ni uchambuzi wako wa kitaalamu kiuchumi au nawe unasukumwa na hisia za kisiasa.

Moja ya vichocheo vya kukua kwa uchumi ni ubora, uimara na uwezo wa miundo mbinu. Mali yoyote haina thamani kama jinsi ya kuifikia ni shida.

Kwafano kilimo hakitakuwa na tija kama mazao hayataweza kuondolewa mashambani na kufikishwa sokoni kwa wakati na ubora ule ule. Vivyo hivyo mbuga zetu hazina thamani kama hakuna njia rahisi (kwa gharama ndogo na uhakika, nk) ya kuzifikia. Mfano ni Kisiwa cha Rubondo, Ziwa Victoria, Mkoa wa Geita, ambacho kina kila aina na sifa za utalii wa samaki na ndege. Je, nani anakifahamu. Na anayekifahamu kufika huko ni shida. Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Chato unabezwa, kwa sababu tu ndio kwao na Rais!


Mkuu umesoma na kufahamu nilichoandika au umekurupuka kujibu,haya uliyoandika hayaendani kabisa na niliyoandika,kwanza nataka ufahamu mimi sio mpenzi wa chama ćhochote cha siasa...

ATCL haiwezi kabisa kushindana na mashirika makubwa akina Emirates,Qatar na mingeneo,mtazamo wangu mimi ,Serikali ya Tanzania ingeyaacha hayo mashirika yakamwaga watalii kutoka nje,lakini usafiri wa anga wa ndani ya nchi unadhibitiwa na ATCL,..

Hizo sehemu ulizo zitaja kama Kisiwa cha Rubondo, Ziwa Victoria, Mkoa wa Geita nk,watalii wangelifikishwa kwa kutumia usafiri wa ndani wa shirika la ATCL,lakini usafiri wa anga wa ndani mbovu serikali imeenda kukurupuka kununua Ndege ambayo ni ya masafa marefu...

Sasa Mkuu hebu nambie Boing Dreamliner itakwenda kufanya nini Chato?
 
Mkuu kuna kitu unapaswa kuelewa. Mfanyabiashara/mtalii ambaye angepanda Air Tanzania kutoka New York to Dar gharama ingekuwa nafuu zaidi kuliko New York to Nairobi then aje Dar. Huwezi kukuta Kenya Airways inaanza safari za New York to Dar moja kwa moja hata kama wasafiri wapo kulinda maslahi ya nchi yao hasa competitive advantages ambazo wanazijua kutokana na weakness zetu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Siku utakapofahamu mikakati ya ushindani ya mashirika ya ndege utashangaa. K.m. utakutana na idadi kubwa ya wasafiri kati ya Johannesburg na Beijing au Johannesburg na London ndani ya ndege ya Ethiopian ilhali kuna direct flights za SAA kati ya majiji hayo. Mara nyingi nimekutana hata na Watanzania wenzangu wakielekea Johannesburg kupitia Addis Ababa wakidai wamegundua unafuu wa nauli. Direct flights si kigezo cha unafuu wa gharama. Bila shaka ATC itapata changamoto kubwa katika route za intercontinental. Kenya sio tatizo pekee. Ijiandae kwa vita kali za bei.
 
Huo ni uchambuzi wako wa kitaalamu kiuchumi au nawe unasukumwa na hisia za kisiasa.

Moja ya vichocheo vya kukua kwa uchumi ni ubora, uimara na uwezo wa miundo mbinu. Mali yoyote haina thamani kama jinsi ya kuifikia ni shida.

Kwafano kilimo hakitakuwa na tija kama mazao hayataweza kuondolewa mashambani na kufikishwa sokoni kwa wakati na ubora ule ule. Vivyo hivyo mbuga zetu hazina thamani kama hakuna njia rahisi (kwa gharama ndogo na uhakika, nk) ya kuzifikia. Mfano ni Kisiwa cha Rubondo, Ziwa Victoria, Mkoa wa Geita, ambacho kina kila aina na sifa za utalii wa samaki na ndege. Je, nani anakifahamu. Na anayekifahamu kufika huko ni shida. Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Chato unabezwa, kwa sababu tu ndio kwao na Rais!



Kwanini tusinunue ndege za mizigo sasa baadala ya hizo za abiria??
Kwa sasa kipi kipaumbele chetu? na nini tunafanya?

Kujenga miundo mbinu ni jambo jema lakini unaanza na miundo mbinu gani na kumalizia miundo mbinu gani.
Watanzania wanahitaji miundo mbinu gani kwa sasa kama kipaumbele chao?.
Je mazao yetu kutoka huko ujiji kigoma yanafikaje sokoni Dar es salaama au sokoni Mbeya au kule London Uingereza?
 
Mkuu umesoma na kufahamu nilichoandika au umekurupuka kujibu,haya uliyoandika hayaendani kabisa na niliyoandika,kwanza nataka ufahamu mimi sio mpenzi wa chama ćhochote cha siasa...

ATCL haiwezi kabisa kushindana na mashirika makubwa akina Emirates,Qatar na mingeneo,mtazamo wangu mimi ,Serikali ya Tanzania ingeyaacha hayo mashirika yakamwaga watalii kutoka nje,lakini usafiri wa anga wa ndani ya nchi unadhibitiwa na ATCL,..

Hizo sehemu ulizo zitaja kama Kisiwa cha Rubondo, Ziwa Victoria, Mkoa wa Geita nk,watalii wangelifikishwa kwa kutumia usafiri wa ndani wa shirika la ATCL,lakini usafiri wa anga wa ndani mbovu serikali imeenda kukurupuka kununua Ndege ambayo ni ya masafa marefu...

Sasa Mkuu hebu nambie Boing Dreamliner itakwenda kufanya nini Chato?
Naamini unataarifa iliyo kamili kuwa pamoja na usafiri wa ndege wa nje kuimarishwa hata wa ndani unaimarishwa. Hiyo ni pamoja na ujenzi wa wa viwanja vya ndege na barabara imara kila kona ya nchi. Utakumbuka rada za kuongozea ndege pia zimenunuliwa kuimarisha usafiri huo.

Japo wewe si mwanachama wa chama chochote cha siasa, lakini naamini unaijua na umeisoma "Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025" (Development Vision 2025). Iliandaliwa miaka mingi iliyopita. Nikuombe uoanishe hiyo Dira na Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015, utaona uwiano uliopo. Kwa maana hiyo, hakuna mkakati wa maendeleo unaotekelezwa kwa kukurupuka.

Wanaokurupuka ni hao wasio na Dira ya kuendesha nchi hii, lakini mabingwa wa kukosoa, kulaumu na kutukana.

Mimi na wewe tunawajibika, kama Watanzania, kutoa mapendekezo ya kuboresha mikakati ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali iliyoko madarakani, au kutoa tafsiri sahihi ya "Development Vision 2025" kwa wakati wa sasa, kiutekelezaji. Lakini, mimi kama mimi, nimeridhika na tafsiri iliyomo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM, 2015.
 
Kwanini tusinunue ndege za mizigo sasa baadala ya hizo za abiria??
Kwa sasa kipi kipaumbele chetu? na nini tunafanya?

Kujenga miundo mbinu ni jambo jema lakini unaanza na miundo mbinu gani na kumalizia miundo mbinu gani.
Watanzania wanahitaji miundo mbinu gani kwa sasa kama kipaumbele chao?.
Je mazao yetu kutoka huko ujiji kigoma yanafikaje sokoni Dar es salaama au sokoni Mbeya au kule London Uingereza?
Nimemjibu Chabuso tayari hapo juu.
 
Siku utakapofahamu mikakati ya ushindani ya mashirika ya ndege utashangaa. K.m. utakutana na idadi kubwa ya wasafiri kati ya Johannesburg na Beijing au Johannesburg na London ndani ya ndege ya Ethiopian ilhali kuna direct flights za SAA kati ya majiji hayo. Mara nyingi nimekutana hata na Watanzania wenzangu wakielekea Johannesburg kupitia Addis Ababa wakidai wamegundua unafuu wa nauli. Direct flights si kigezo cha unafuu wa gharama. Bila shaka ATC itapata changamoto kubwa katika route za intercontinental. Kenya sio tatizo pekee. Ijiandae kwa vita kali za bei.

Mkuu, hapo kwenye bei umenena. Kwanini mashirika kama Delta ya Marekani inapiga ukunga kwamba ushindani kati yao na mashirika ya ndege za Uarabuni sio fair? Kwa sababu Waarabu wanafungulia bomba la mafuta kama subsidies kwa mashirika yao.

Siyo kwamba hatupendi chetu, ila tunasema ukweli. Kagame kama ndo kamshauri Jiwe afanye hivi, kamuingiza mkenge. Cha pili, hivi tumewahi kujiuliza kwa nini Marekani ambako ndege ziligunduliwa haina shirika la ndege la taifa na watalii kibao wako New York kila siku?
 
Mkuu, hapo kwenye bei umenena. Kwanini mashirika kama Delta ya Marekani inapiga ukunga kwamba ushindani kati yao na mashirika ya ndege za Uarabuni sio fair? Kwa sababu Waarabu wanafungulia bomba la mafuta kama subsidies kwa mashirika yao.

Siyo kwamba hatupendi chetu, ila tunasema ukweli. Kagame kama ndo kamshauri Jiwe afanye hivi, kamuingiza mkenge. Cha pili, hivi tumewahi kujiuliza kwa nini Marekani ambako ndege ziligunduliwa haina shirika la ndege la taifa na watalii kibao wako New York kila siku?

..nasubiri wajibu hoja zako.

..tukiwaambia hawa ndugu zetu ATCL itakuja kuwa KUPE wanachukia.
 
Mkuu, hapo kwenye bei umenena. Kwanini mashirika kama Delta ya Marekani inapiga ukunga kwamba ushindani kati yao na mashirika ya ndege za Uarabuni sio fair? Kwa sababu Waarabu wanafungulia bomba la mafuta kama subsidies kwa mashirika yao.

Siyo kwamba hatupendi chetu, ila tunasema ukweli. Kagame kama ndo kamshauri Jiwe afanye hivi, kamuingiza mkenge. Cha pili, hivi tumewahi kujiuliza kwa nini Marekani ambako ndege ziligunduliwa haina shirika la ndege la taifa na watalii kibao wako New York kila siku?
..nasubiri wajibu hoja zako.

..tukiwaambia hawa ndugu zetu ATCL itakuja kuwa KUPE wanachukia.
Wote nyie mnajua anayemiliki na kuendesha utajiri wa Marekani siyo Serikali bali mabepari.

Nani hapa kwetu ana uwezo wa kumiliki ndege za abiria awezd kibiashara kushindana na hayo mashirika?

Inatia ukakasi na ni tusi kwa Watanzania Jazzie unapodai Kagame ndiye mshauri wa Rais wetu. Ebu soma "Dira ya Maendeleo ya 2025" na "Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015" ujiridhishe kuwa mipango na mikakati ya maendeleo ni yetu wenyewe Watanzania. Rais na viongozi wenzake wa Serikali ni wanatekelezaji tu.

Jazzie, unajitukana na kuonesha upeo wako wa uchambuzi wa masuala ya kitaifa ulivyo finyu.
 
Kwanini tusinunue ndege za mizigo sasa baadala ya hizo za abiria??
Kwa sasa kipi kipaumbele chetu? na nini tunafanya?

Kujenga miundo mbinu ni jambo jema lakini unaanza na miundo mbinu gani na kumalizia miundo mbinu gani.
Watanzania wanahitaji miundo mbinu gani kwa sasa kama kipaumbele chao?.
Je mazao yetu kutoka huko ujiji kigoma yanafikaje sokoni Dar es salaama au sokoni Mbeya au kule London Uingereza?
Maua na mboga mboga mpaka twende kenya
 
Naamini unataarifa iliyo kamili kuwa pamoja na usafiri wa ndege wa nje kuimarishwa hata wa ndani unaimarishwa. Hiyo ni pamoja na ujenzi wa wa viwanja vya ndege na barabara imara kila kona ya nchi. Utakumbuka rada za kuongozea ndege pia zimenunuliwa kuimarisha usafiri huo.

Japo wewe si mwanachama wa chama chochote cha siasa, lakini naamini unaijua na umeisoma "Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025" (Development Vision 2025). Iliandaliwa miaka mingi iliyopita. Nikuombe uoanishe hiyo Dira na Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015, utaona uwiano uliopo. Kwa maana hiyo, hakuna mkakati wa maendeleo unaotekelezwa kwa kukurupuka.

Wanaokurupuka ni hao wasio na Dira ya kuendesha nchi hii, lakini mabingwa wa kukosoa, kulaumu na kutukana.

Mimi na wewe tunawajibika, kama Watanzania, kutoa mapendekezo ya kuboresha mikakati ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali iliyoko madarakani, au kutoa tafsiri sahihi ya "Development Vision 2025" kwa wakati wa sasa, kiutekelezaji. Lakini, mimi kama mimi, nimeridhika na tafsiri iliyomo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM, 2015.
Mkuu,kila raia anataka maendeleo ya nchi yake,kubali kuwa utawala wa Magufuli na chama chake cha CCM wamekurupuka kwa hili,mimi silahaiwi wala kurubuniwa na siasa,hasa hichi kikundi cha siasa kinachoitwa CCM..

Kama wewe unamini "Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025" inayoongozwa na dira ya CCM ndio itawaletea watanzania mabadiliko na maendeleo wanayoyataka basi hongera mkuu,CCM imekaa madarakani zaidi ya miaka 50 hamna chochote cha maana kilichowaletea watanzania isipokuwa ruswa na unyanyasaji wa raia,...

CCM haina dira,matatizo makubwa yaliyokuwa nayo hichi chama ni kutojitambua siasa gani waifuate,kama wafuate "Socialism" au "Capitalism",hayo yanajionesha hata katika utawala wa Magufuli..

Kufufua shirika la ndege la Tanzania ni kitu kizuri sana lakini mbinu zinazotumika sizo,zinatumika mbinu za kisiasa sio za kitaalamu,Wangeanza kuimarisha usafiri wa ndani kwanza,hivyo viwanja vya ndege vitatumika vipi kama usafiri wa anga wa ndani ya nchi haujaimarishwa,...?

Wangelimwaga Bombardier za kutosha ili Mtanzania na Watalii wanaokuja kuitembelea Tanzania wangeliweza kufika kila kona ya nchi,Kununuliwa kwa Boing Dreamliner ni mihemko na kiki za kisiasa,hii ndege ni mzigo kwa shirika la ndege la Tanzania
 
Wote nyie mnajua anayemiliki na kuendesha utajiri wa Marekani siyo Serikali bali mabepari.

Nani hapa kwetu ana uwezo wa kumiliki ndege za abiria awezd kibiashara kushindana na hayo mashirika?

Inatia ukakasi na ni tusi kwa Watanzania Jazzie unapodai Kagame ndiye mshauri wa Rais wetu. Ebu soma "Dira ya Maendeleo ya 2025" na "Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015" ujiridhishe kuwa mipango na mikakati ya maendeleo ni yetu wenyewe Watanzania. Rais na viongozi wenzake wa Serikali ni wanatekelezaji tu.

Jazzie, unajitukana na kuonesha upeo wako wa uchambuzi wa masuala ya kitaifa ulivyo finyu.

Mkuu ngoja nikujibu:
1. Nani hapa kwetu ana uwezo wa kumiliki ndege za abiria awezd kibiashara kushindana na hayo mashirika? - Unafanya assumption kwamba ilikuwa lazima Tanzania nayo iwe na shirika la ndege. Hiyo hoja imeshapanguliwa hapo juu na wachangiaji wengi. Siyo lazima Tanzania iwe na shirika la ndege ili ipate maendeleo au watalii waje. Pili, tumeshakubaliana kwamba Tanzania ni nchi ya soko huria, na ndiyo maana tuna wawekezaji binafsi kama akina FastJet etc (Ilani ya CCM ukurasa wa 70 inaongelea mpango wa PPP, kwa hiyo utaka kusema CCM ni vichaa kuamini watu binafsi wana uwezo wa kununua ndege?). Kama kuna manufaa/faida, wawekezaji lazima watapatikana tu. Unadhani ipi ni gharama zaidi, kununua ndege au kuwekeza kwenye uchimbaji wa madini, kwa mfano?

2. Ebu soma "Dira ya Maendeleo ya 2025" na "Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015" ujiridhishe kuwa mipango na mikakati ya maendeleo ni yetu wenyewe Watanzania. - Nimepitia Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015, hakuna sehemu imeanishwa kwamba serikali ya CCM itafufua ATCL peke yake (bali kupitia mpango wa PPP, soma ukurasa wa 70), both kwenye vipengelea vya utalii na usafiri wa anga (ambavyo vinasemwa kama sababu ya kufufua ATCL). Kwa hiyo tusidanganyane. Ukweli ni kwamba Kagame kamuingiza mjini Jiwe.
 
Mkuu Mtazamo, ukisoma habari za mitandaoni unaweza kudhani kuwa huko mtaani pamewaka moto kama ilivyokuwa Harare wakati wakisubiri matokeo ya uchaguzi.

ATCL na TCAA zinaendeshwa kisomi sana, waliopewa nafasi ya kuongoza wamepewa na uhuru wa kutekeleza kazi zao kitaalam.

Achana na hizi siasa za wawakilishi wa wananchi bungeni, zile chanzo chake ni maslahi binafsi ya watu fulani kuminywa na madalali kubaki na njaa.

Nidhamu ilikuwa inakosekana, sasa hivi mkuu wa nchi hachelewi kumtimua mtu kazi kama anafanya mambo ya kijinga.
 
Mkuu ngoja nikujibu:
1. Nani hapa kwetu ana uwezo wa kumiliki ndege za abiria awezd kibiashara kushindana na hayo mashirika? - Unafanya assumption kwamba ilikuwa lazima Tanzania nayo iwe na shirika la ndege. Hiyo hoja imeshapanguliwa hapo juu na wachangiaji wengi. Siyo lazima Tanzania iwe na shirika la ndege ili ipate maendeleo au watalii waje. Pili, tumeshakubaliana kwamba Tanzania ni nchi ya soko huria, na ndiyo maana tuna wawekezaji binafsi kama akina FastJet etc (Ilani ya CCM ukurasa wa 70 inaongelea mpango wa PPP, kwa hiyo utaka kusema CCM ni vichaa kuamini watu binafsi wana uwezo wa kununua ndege?). Kama kuna manufaa/faida, wawekezaji lazima watapatikana tu. Unadhani ipi ni gharama zaidi, kununua ndege au kuwekeza kwenye uchimbaji wa madini, kwa mfano?

2. Ebu soma "Dira ya Maendeleo ya 2025" na "Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015" ujiridhishe kuwa mipango na mikakati ya maendeleo ni yetu wenyewe Watanzania. - Nimepitia Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015, hakuna sehemu imeanishwa kwamba serikali ya CCM itafufua ATCL peke yake (bali kupitia mpango wa PPP, soma ukurasa wa 70), both kwenye vipengelea vya utalii na usafiri wa anga (ambavyo vinasemwa kama sababu ya kufufua ATCL). Kwa hiyo tusidanganyane. Ukweli ni kwamba Kagame kamuingiza mjini Jiwe.
Fursa ya sector binafsi ilikuwepo muda mrefu kuwekeza kwenye anga lakini uwekezaji wake unafahamika hata coverages kwenye internal routes ilikuwa tatizo.

Ili serikali iweze kutekeleza sera zake za maendeleo kupitia maboresho ya miundombinu ikiwemo usafiri wa anga lazima wawe na shirika ambalo ni lao 100% au wanahisa za kutosha kushawishi uendeshaji utaoendana na sera za ushindani wa kibiashara kimataifa.

Tusidanganyane, fatilia historia za mashirika makubwa ya ndege ya nchi zilizoendelea na mchango wa serikali kuyasaidia kimtaji.

Hii ATCL ikienda vizuri tutaweza kuruhusu wawekezaji ambao wataleta mtaji wenye tija lakini kwasasa hatua hizi zilikuwa hazikwepeki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom