thetallest
JF-Expert Member
- Oct 21, 2017
- 8,256
- 9,085
Ukweli lazima usemwe, kuna tatizo gani kutambua juhudi za hayati Magufuli kwenye mradi huu wa umeme (JNHP), hasa kwenye hotuba zenu?
Wazo lilikuwa la Mwalimu Nyerere akashindwa, awamu zilizofuata kuanzia ya pili mpaka ya NNE, hawakuwa na habari na mradi huo, waliupa kisogo.
Hayati Magufuli kwa nguvu kubwa na ujasiri usio na shaka akaamua kutekeleza wazo hilo.
Miongoni mwa waliohujumu juhudi za ujenzi wa hili bwawa ni wewe waziri wa sasa wa nishati, January Makamba, kwa kisingizio cha uharibifu wa mazingira, ikapelekea mpaka kuondolewa baraza la mawaziri.
Leo hotuba ya mkurugenzi mkuu Maharage Chande na waziri wake wamejificha kwenye kichaka cha mipasho hasa waziri Makamba.
Nijielekeze kwenye usanii wa waziri Makamba kutambua juhudi za watangulizi kwenye ujenzi wa bwawa hilo, katengeneza zawadi za kutambua michango ya mzee Mwinyi ,na Jakaya, wana mchango gani ikiwa mradi waliupa kisogo?
Makamba junior kawapa medali za kinafiki sana, hata wao wamejisikia aibu sana kupewa medali za ushiriki wao kwa mradi wakati hawajashiriki hata kidogo.,dhambi kubwa sana ikiambatana na unafiki wa hali ya juu.
Huyu kijana ndio anawaza kuwa rais wa hii nchi. Tuna hasara kubwa kama taifa.
Nimpongeze rais Samia kwa kujaribu kuusema ukweli kuhusu kazi kubwa ya hayati Magufuli katika kufanikisha mradi huu.
Kumekuwa na syndicate kupoteza Juhudi za hayati Magufuli kwa kuzimeza kijumla jumla na wasiostahili. Mojawapo ni hilo tukio la kinafiki la kutambua mchango wa hao watangulizi kuhusu bwawa hili, wakati si washiriki.
Namalizia kwa kumwambia waziri Makamba na walio nyuma yake kwamba watanzania hawadanganyiki tena, Magufuli aliwafumbua macho.
Huu mchezo wa kujaza vijana mitandaoni kumdhihaki, mmeona leo jinsi likitajwa jina lake makofi na shangwe kama lote.
Nikiashiria kwamba kimwili hatuko naye ila kifikra tukonae, acheni majungu dhidi ya marehemu.
Wazo lilikuwa la Mwalimu Nyerere akashindwa, awamu zilizofuata kuanzia ya pili mpaka ya NNE, hawakuwa na habari na mradi huo, waliupa kisogo.
Hayati Magufuli kwa nguvu kubwa na ujasiri usio na shaka akaamua kutekeleza wazo hilo.
Miongoni mwa waliohujumu juhudi za ujenzi wa hili bwawa ni wewe waziri wa sasa wa nishati, January Makamba, kwa kisingizio cha uharibifu wa mazingira, ikapelekea mpaka kuondolewa baraza la mawaziri.
Leo hotuba ya mkurugenzi mkuu Maharage Chande na waziri wake wamejificha kwenye kichaka cha mipasho hasa waziri Makamba.
Nijielekeze kwenye usanii wa waziri Makamba kutambua juhudi za watangulizi kwenye ujenzi wa bwawa hilo, katengeneza zawadi za kutambua michango ya mzee Mwinyi ,na Jakaya, wana mchango gani ikiwa mradi waliupa kisogo?
Makamba junior kawapa medali za kinafiki sana, hata wao wamejisikia aibu sana kupewa medali za ushiriki wao kwa mradi wakati hawajashiriki hata kidogo.,dhambi kubwa sana ikiambatana na unafiki wa hali ya juu.
Huyu kijana ndio anawaza kuwa rais wa hii nchi. Tuna hasara kubwa kama taifa.
Nimpongeze rais Samia kwa kujaribu kuusema ukweli kuhusu kazi kubwa ya hayati Magufuli katika kufanikisha mradi huu.
Kumekuwa na syndicate kupoteza Juhudi za hayati Magufuli kwa kuzimeza kijumla jumla na wasiostahili. Mojawapo ni hilo tukio la kinafiki la kutambua mchango wa hao watangulizi kuhusu bwawa hili, wakati si washiriki.
Namalizia kwa kumwambia waziri Makamba na walio nyuma yake kwamba watanzania hawadanganyiki tena, Magufuli aliwafumbua macho.
Huu mchezo wa kujaza vijana mitandaoni kumdhihaki, mmeona leo jinsi likitajwa jina lake makofi na shangwe kama lote.
Nikiashiria kwamba kimwili hatuko naye ila kifikra tukonae, acheni majungu dhidi ya marehemu.