Kwako Mtanzania: Usajili kwenye Chama cha Utajiri

Je, umeipenda Poem hii?

  • Ndio, nimelipenda

    Votes: 8 80.0%
  • Nimelipenda kiasi

    Votes: 1 10.0%
  • Hapana sijalipenda

    Votes: 1 10.0%

  • Total voters
    10

Mitch McDeere

JF-Expert Member
Feb 24, 2017
299
619
USAJILI, UTAJIRI, UMAHIRI

Kuanzia sasa ninafanya usajili,
Kuanzia sasa ninajisajili,
Najiunga kwenye chama cha utajiri.

Kwanza nitaboresha uwezo wangu wa akili,
Kila jambo nitafanya kwa kufikiri,
Na kwenye kazi yangu nitaongeza umahiri.

Kwa nini nimeanza na akili?
Kwa sababu nilimsikia tajiri Bill,
Kuwa utajiri huanza na mindset, yaani namna unavyofikiri.

Pili nitaongeza ujasiri,
Changamoto zote nitazikabili,
Na mikikimikiki ya utafutaji nitaihimili.

Tatu, nitaongeza "kidoogo" ubahili,
Ila ninaapa sitakuwa na ukatili,
Nitatafuta bila utu wangu kujiathiri.

Nne, nitakuwa na bajeti za bili,
Za mapato, maokoto na maduhuli,
Vyote nitaviandika na nitavikariri.

Tano, nitafanya kazi kwa bidii kamili,
Vyanzo vyangu vya mapato nitaviongeza kwa utitiri,
Nitapambana huku na huko hata ikibidi kusafiri.

Mwisho, wanasema utajiri una siri,
Hivyo, nitaendelea kujifunza siri za utajiri,
Bila kuathiri yangu dhamiri.

Karibu Tajiri.

By Mitch McDeere
 
USAJILI, UTAJIRI, UMAHIRI

Kuanzia sasa ninafanya usajili,
Kuanzia sasa ninajisajili,
Najiunga kwenye chama cha utajiri.

Kwanza nitaboresha uwezo wangu wa akili,
Kila jambo nitafanya kwa kufikiri,
Na kwenye kazi yangu nitaongeza umahiri.

Kwa nini nimeanza na akili?
Kwa sababu nilimsikia tajiri Bill,
Kuwa utajiri huanza na mindset, yaani namna unavyofikiri.

Pili nitaongeza ujasiri,
Changamoto zote nitazikabili,
Na mikikimikiki ya utafutaji nitaihimili.

Tatu, nitaongeza "kidoogo" ubahili,
Ila ninaapa sitakuwa na ukatili,
Nitatafuta bila utu wangu kujiathiri.

Nne, nitakuwa na bajeti za bili,
Za mapato, maokoto na maduhuli,
Vyote nitaviandika na nitavikariri.

Tano, nitafanya kazi kwa bidii kamili,
Vyanzo vyangu vya mapato nitaviongeza kwa utitiri,
Nitapambana huku na huko hata ikibidi kusafiri.

Mwisho, wanasema utajiri una siri,
Hivyo, nitaendelea kujifunza siri za utajiri,
Bila kuathiri yangu dhamiri.

By Mitch McDeere
Ooh kumbe ni USHAHIRI,
Wacha kwanza NIFIKIRI,
Maana wengi MATAJIRI,
Husema utajiri una SIRI.

Kiukweli nataka MALI,
Nami niitwe TAJIRI,
Hohehahe yangu HALI,
Utajiri una SIRI.

Ninao huo UJASIRI,
Wa kusaka hizo MALI,
Ila huu mfumo wa KIBEPARI,
Wengi wetu MAFAKIRI.

Kaka wacha tu TUJIAJIRI,
Naanza na BAISIKERI,
Kesho nina mawili MALORI,
Ndivyo tuambiwavyo na MATAJIRI.

Kaka nami NISAJILI,
Mnikopeshe laki MBILI,
Nianze na KACHUMBALI,
Kesho nimiliki HOTELI.


Ngoja nirudie kusoma ushairi wako, niache akili za usiku
 
Ooh kumbe ni USHAHIRI,
Wacha kwanza NIFIKIRI,
Maana wengi MATAJIRI,
Husema utajiri una SIRI.

Kiukweli nataka MALI,
Nami niitwe TAJIRI,
Hohehahe yangu HALI,
Utajiri una SIRI.

Ninao huo UJASIRI,
Wa kusaka hizo MALI,
Ila huu mfumo wa KIBEPARI,
Wengi wetu MAFAKIRI.

Kaka wacha tu TUJIAJIRI,
Naanza na BAISIKERI,
Kesho nina mawili MALORI,
Ndivyo tuambiwavyo na MATAJIRI.

Kaka nami NISAJILI,
Mnikopeshe laki MBILI,
Nianze na KACHUMBALI,
Kesho nimiliki HOTELI.


Ngoja nirudie kusoma ushairi wako, niache akili za usiku
Mkuu Tembeleni 01,

Umeongeza maneno fulani mazuri,
Yanayohusiana na dhana ya utajiri,
Kwa mfano ubepari, ufakiri, na mali,

Ahsante kwa kutumia muda wako kufikiri,
Na nimependa wazo lako la kujiajiri,
Anza kidogo na baiskeli,
Miaka michache utamiliki malori.
 
Hata uchutame na kudhikiri, kamwe hutapata utajiri kwa yako macho mawili.

Wengi hujifanya majasiri kuusaka utajiri, kamwe yakupasa utumie akili.

Mwendoni uwapo kuusaka utajiri, kamwe usigeuke fahali.

Pumzi imekata namshukuru jalari, ila nahisi kama uzi tayali.
 
Hata uchutame na kudhikiri, kamwe hutapata utajiri kwa yako macho mawili.

Wengi hujifanya majasiri kuusaka utajiri, kamwe yakupasa utumie akili.

Mwendoni uwapo kuusaka utajiri, kamwe usigeuke fahali.

Pumzi imekata namshukuru jalari, ila nahisi kama uzi tayali.
Kisima, Tajiri
Umetoa nasaha zenye uzamivu na uzamili,
Hasa hapo kwenye utajiri kwa macho mawili,
Na ninakupa kongole kwa kweli.

Jim Rohn, msemaji mashuhuri,
Alisema kuna kuona kwa aina mbili,
Moja, kuona kwa macho mawili,
Mbili, kuona kwa kutumia akili.

Utajiri unahitaji kuona kwa aina ya pili.



"Remember, there are two ways to see.
Seeing with your eyes.
Seeing with your mind."
Jim Rohn
 
Back
Top Bottom