JWTZ linachukua proffessionals kwa mahitaji maalum na kwa utaratibu maalum pale wanapohitajika na unaomba kazi kama unavyoomba kazi zingine japo ni kweli kipaumbele huwa ni kwa vijana waliopo makambini tayari (waliojiendeleza) na kutoka jkt. Lakini wapo wanaoajiriwa bila kutoka sehemu hzo (inatemea sasa na mahitaji)
Duh, ila kwa kigezo cha umri sizani kama Jkt itakua na graduate alaf wanasema kabisa kua wanataka darasa la saba mpaka form six
Kwani huko chuoni ulikua unasomea nini?
Unataka jeshi kwani fani yako uliosomea ni Military science?
Jeshi halitaki waliosoma nasikia mnakua na viburi halafu waoga.
Jeshi linaitaji wahasibu, madokta, madereva, store na manunuzi sasa wewe sijui unaongelea jeshi la nchi gani lisiloitaji graduates! Na kama kuna graduate aliyekuzalau huyo ni tabia yake ila si wote wenye zarau
Jeshi linaitaji wahasibu, madokta, madereva, store na manunuzi sasa wewe sijui unaongelea jeshi la nchi gani lisiloitaji graduates! Na kama kuna graduate aliyekuzalau huyo ni tabia yake ila si wote wenye zarau
Kama hujui uliza,jeshi wanavyuo vyao kwa ajili ya mambo yao.
Madaktari,manesi chuo kipo Lugalo.
Madereva,stores,na fani zingine chuo kipo Pangawe Morogoro.
Ukiona wanachukua watu wa mitaani ni kuzima mapengo machache tu.
Sasa kama wewe umesomea ustawi wa jamii jeshi likuhitaji kwa kazi ipi?
Mimi sijasoma ustawi na istoshe kuna rafiki zangu wengi tu walihitimu vyuo kama UDSM, TIA, IAA , MZUMBE wamejoin army na wanafanya kazi katika fani zao!
Ndo nakueleza sasa madhaifu yao yameonekana ktk utendaji kijeshi wengi wao wanakua na uraia fulani, ndo maana siku hizi nasikia wanachukua wanajeshi waliojiendeleza wakiwa makazini na kuwapeleka kusomea uafisa jeshini.
Swala la uofisa siku nyingi ndivyo ilivyo kwamba lazima uwe askari (private) alaf ndo unaenda kusomea uofisa, ila ishu ya kuchukua watu kwenye ivyo vyuo ulivyosema ndonalisikia leo
Kwani baada ya kuhitimu RTS sindo unakua private au, embu nieleweshe kama niko wrong
Ukitoka kozi ya RTS unaenda kozi nyingine za specialization kutokana na fani na kamandi uliyopo na kuwa private
Ndo mana private wa kamandi ya anga,ardhini,majini au jkt wanatofautiana ki elimu ya medani
Duh, Sasa tukiludi kwenye mada nini maoni yako juu ya hawa jkt kutaka watu wenye miaka 23 mwisho wakati kwa mfumo wetu wa elimu mtu anaitimu chuo akuwa na 25 au 26, hauna tetesi juu ya intake ya watu kama hao?