ministrant
JF-Expert Member
- Jan 17, 2014
- 554
- 1,134
Wasalaam,
Kumekuwa na changamoto kubwa kwa vijana wengi wenye sifa kujiunga na Vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama kama vile Polisi, Magereza na JWTZ kukwama kujiunga kutokana na kukosa kigezo kimoja tu kuwa hawakupita mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa.
Hii inapelekea vyombo hivi kupoteza vijana wengi wenye weledi kujiunga na vyombo hivyo kwa kukosa fursa ya kupita JKT kutokana na mifumo iliyopo kujiunga na JKT.
Napendekeza hiyo ibaki tu kuwa sifa ya ziada ili kutoa fursa sawa ya ushindani kutokana na mifumo ya kielimu kutowapa fursa ya wao kupita huko.
Kwa mfano kijana amemaliza kidato cha nne au sita lakini shule yake haikuwamo katika orodha ya wanaotakiwa kupatiwa mafunzo hayo kwa mwaka husika, hivyo kupelekea kijana huyu kwenda chuo moja kwa moja mathalani na kuchukua masomo ya udaktari wa Binadamu na baada ya kuhitimu akakosa sifa ya kujiunga na vyombo hivyo eti kwakuwa tu hakupita JKT.
Napendekeza Serikali ifanyie marejeo utaratibu huu ukiachilia mbali uwezo mdogo wa kambi za JKT kutoa mafunzo kwa kila kijana aliyefikisha umri wa miaka 18 na kuendelea.
Pia hivi sasa kumeibuka ubaguzi hata kwa hao waliopitia JKT katika ajira kipaumbele kinatolewa kwa waliojitolea miaka 2 na kuwakataa wale waliopitia mafunzo hayo hayo kwa mujibu wa sheria baada ya kuhitimu kidato cha 6.
Kupita JKT ni jambo jema lakini kuna nguvu kazi kubwa na yenye weledi wa hali ya juu inapotes mtaani ambayo ingekuwa msaada kwa vyombo vyetu lakini inakutana na changamoto hiyo.
Nawasilisha
Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
Kumekuwa na changamoto kubwa kwa vijana wengi wenye sifa kujiunga na Vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama kama vile Polisi, Magereza na JWTZ kukwama kujiunga kutokana na kukosa kigezo kimoja tu kuwa hawakupita mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa.
Hii inapelekea vyombo hivi kupoteza vijana wengi wenye weledi kujiunga na vyombo hivyo kwa kukosa fursa ya kupita JKT kutokana na mifumo iliyopo kujiunga na JKT.
Napendekeza hiyo ibaki tu kuwa sifa ya ziada ili kutoa fursa sawa ya ushindani kutokana na mifumo ya kielimu kutowapa fursa ya wao kupita huko.
Kwa mfano kijana amemaliza kidato cha nne au sita lakini shule yake haikuwamo katika orodha ya wanaotakiwa kupatiwa mafunzo hayo kwa mwaka husika, hivyo kupelekea kijana huyu kwenda chuo moja kwa moja mathalani na kuchukua masomo ya udaktari wa Binadamu na baada ya kuhitimu akakosa sifa ya kujiunga na vyombo hivyo eti kwakuwa tu hakupita JKT.
Napendekeza Serikali ifanyie marejeo utaratibu huu ukiachilia mbali uwezo mdogo wa kambi za JKT kutoa mafunzo kwa kila kijana aliyefikisha umri wa miaka 18 na kuendelea.
Pia hivi sasa kumeibuka ubaguzi hata kwa hao waliopitia JKT katika ajira kipaumbele kinatolewa kwa waliojitolea miaka 2 na kuwakataa wale waliopitia mafunzo hayo hayo kwa mujibu wa sheria baada ya kuhitimu kidato cha 6.
Kupita JKT ni jambo jema lakini kuna nguvu kazi kubwa na yenye weledi wa hali ya juu inapotes mtaani ambayo ingekuwa msaada kwa vyombo vyetu lakini inakutana na changamoto hiyo.
Nawasilisha
Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app