Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

ukweli unaweza pata uchizi kwa biashara hii,nilishataka kunywa sumu baada ya kuamka asubuhi na kukuta kuku 322 kati ya 500 wamekufa na takriban 40 wameparalise,na ndiyo kwanza wamefikisha wiki nne na nusu,yaani nilichanganyikiwa nikatamani afadhali hela yangu ningepigia lagha nikaongeza damu na kuweka heshima bar

Pole kuku hawa hawataki mchezo, hapa itakuwa ni chanjo ulichelewa au hukuwapa vizuri, pili ku paralise au miguu kwisha nguvu ni kukosa calcium, wiki ya 3 unatakiwa uwape mifupa ili kuwaongezea uimara kwenye miguu kwasababu wiki ya nne wanaanza kuwa na uzito mkubwa kulingana na mwili. Pia chakula unachowapa jaribu kuona wenzio wanaokitumia kuku wao wakoje, kwani chakula kisichokuwa na dagaa ya kutosha ndio huwa kinamadhara zaidi.

Vifo vingi ni kutokana na Newcastle infection, Gumboro na multiple infection kwa kukosa hewa safi kama kuku ni wengi kulingana na ukubwa wa banda., pia typhoid fevers kutokan na maji yasiyo safii au uchafu kwenye vyombo vya maji
Lakini ukifata kanuni zao, yaani huwezi kutana na hivi vifo hata kidogo
 
Mama Joe asante; swali la nyongeza kwenye hawa kuku wa kisasa; upande upi unafaa kwa tunaoanza lets say mtaji ni 3ml; wa nyama ama wa mayai? Na ni kiasi gani kwa gharama kuanzia banda lao?
 
Mama Joe asante; swali la nyongeza kwenye hawa kuku wa kisasa; upande upi unafaa kwa tunaoanza lets say mtaji ni 3ml; wa nyama ama wa mayai? Na ni kiasi gani kwa gharama kuanzia banda lao?
Kwa mtaji huo unaweza kuanza na wote, kikubwa soko umeulizia lina uhakika la nini?
Wa nyama wanaenda fast kiasi matokeo unayaona katika wiki 6 tu, ila inabidi nawe uende fast, kutafuta soko ili usikae na kuku wiki 5+

Wa nyama wanaenda taratibu, utawalisha miezi 6 bila kuona faida, then utaokota mayai kwa miezi 18 baadae utawauza wenyewe kwa bei kubwa pia.

Wa nyama ni kama mtu anataka hela kuanzia mwezi mmoja toka aanze kufuga mfano Access bank wanakukopesha ukiwa nao ili kulipa itabidi uweke hawa kama huna other source of income.
Kwa swali lako:

Angalia budget yako, kuku wangapi utaweka, soko hasa wa nyama,

Naweza kukupa mchanganuo wa kuku wa nyama kwa kila banda la kuku 200
vifaranga 200 au 210 ili kufidia vitavyokufa: (@ 1000)
starter mifuko 4 kwa wiki 1 hadi 4 (25,000 - 27,000 @)
Finisher 6 kwa wiki ya 4 - 5 ( 25,000 - 27,000 @)
madawa, mifupa na chanjo havizidi 20,000, randa haizidi 10,000. Hizi bei zinatofautiana sana ukienda mfano Ubungo Assad au Tegeta Eagle bei nafuu ila wakileta hawa maduka ya mtaani utaumia. Kwa hiyo angalia hizo bei kwanza, bei ya sokoni ujue kabisa faida kabla (kwangu wastani kwa chakula cha kununua ni sh 180,000 - 200,000 kwa kila kuku 200)

Kuku wamayai utawalisha chakula sawa na wanyama hadi wiki ya 4, halafu unaanza Layers mash, nayo nadhani bei ni hii ya finisher (sijawafuga muda ila mdogoangu anao hawa, hivy kadiria chakula chao miezi sita then unaanza kupata mayai yankusidia kurudisha hela ya chakula na zaidi.

(Wastani hawa band la kuku 300 unapata 50,000 kwa siku ingawa inaweza badilikabadilika kwani sio kila siku watataga, uzuri wake ni kwamba unaweza kaa na mayai yako ukitafuta soko taratibu bila hasara kama kulisha broiler na fida ya mwisho ni kuwauza wenyewe pia.)
 
Nilianza biashara hii mwishoni mwa mwaka jana lakini inaelekea I was carried away na hizi statement kuwa soko ni kubwa sana. sasa napata sghida sana kuwauza ingawa nilifanya akikl ya kutoanza na kuku wengi. Nina batch ya kuku 200 ambao next week wanafikisha wiki 6 tayari kwa kuuza, anayejua soko tafadhali anifahamishe

Assuming uko Dar, week sita kuuza kama hukuwa na soko ulilotafiti ni ngumu kuuza kwa bei ya faida. Wale wachuuzi wa kisutu huwa wanauziwa wa week nne kutokana na bei yao ndogo. (3000 - 3500). Kuku 200 siyo wengi sana, ningekushauri uwachinje wote, wagandishe wakati unatafuta soko, otherwise utakula hasara wakati uliowauzia wakishangilia kuku wako wakubwa.
 
Assuming uko Dar, week sita kuuza kama hukuwa na soko ulilotafiti ni ngumu kuuza kwa bei ya faida. Wale wachuuzi wa kisutu huwa wanauziwa wa week nne kutokana na bei yao ndogo. (3000 - 3500). Kuku 200 siyo wengi sana, ningekushauri uwachinje wote, wagandishe wakati unatafuta soko, otherwise utakula hasara wakati uliowauzia wakishangilia kuku wako wakubwa.

Mpendwa jambo jingine kuwa makini sana wakati wa kuuza hasa kwa hawa jamaa wa kisutu ni wezi stadi wana mbinu kali utashangaa umepata shoti ya kuku hata 100 usipokuwa makini,na wala usilogwe kumwachia house girl pekeyake wana huwa wanatumia mbinu mmoja anakaa mlangoni mwingine anaingia ndani anarusha kuku wawili hata watatu na kuhesabu mmoja utajuta kuzaliwa walishamliza dada yangu akataka kumfukuza house girl amemwibia kumbe sivyo
 
nikiwa nimesimama nakupongeza Mama Joe! Mungua akubariki
Thanks MJ, just to inspire you, biashara imenisaidia sana nilianza na mtaji mdogo sana (500,000) tu, tena kipindi nimesimama kazi. lakini kutokana na hii biashara na mishahara tuna shamba, tunajenga tena na tunasomesha watoto hata ndugu. My only regret ni kuwa sijaweza kuitanua sana hadi shambani kutokana na majukumu mengi. but all potential are there
Ni biashara ambayo hata mtu mmoja tu (labour) hata mwanamke,anaweza kuifanya kuanzia kutunza vifaranga hadi kuuza,
 
Shukrani zangu kwa Mlachake; kwa kuleta mada na wachangiaji wote kwa upendo wenu na kujitoa kutufunza! Mie nimepata akili mpya na mmenitoa woga niliojijengea kuhusu biashara hii na nikapoteza muda kwenye biashara zilizonifilisi!
 
Nakushauri utembelee wanunuzi wa kuku aina unayotaka kufuga kuweza kupata uhakika na ukubwa wa soko. Unatakiwa kupata taarifa za soko la kuku kwa msimu mzima wa mwaka. Kama kuna kuyumba kwa bei unatakiwa kujua vema. Pili tembelea wafugaji wanaofuga maeneo yako kupata gharama halisi za uzalishaji na njia wanazotumia kupunguza gharama. Angalia gharama za uwekezaji hasa mabanda bora (bwana shamba/vitabu vinavyotolewa wizara ya mifugo).

Baada ya hapo unatakiwa kusoma (literature) kuhusiana na standard za kitaifa za utunzaji na utengenezaji wa chakula cha kuku na uzalishaji kwa ujumla wake. Orodhesha gharama za uzalishaji kwa kila mwezi, Fanya makisio ya mapato ya kila mwezi kutokana na takwimu toka wanunuzi na uzalishaji na standard za kitaifa za uzalishaji. (Mabwana shamba wanaweza kukusaidia)

Hapo unaweza kuangalia kama una mtaji wa kufanya shughuli hii. kama ndivyo basi andaa mpango kamili wa shughuli. andiko liwe na sehemu muhimu kama ufupisho, maelezo ya awali, mpango wa masoko, uendeshaji na usimamizi na mpango wa fedha
 
Habari wakuu:

Bila shaka kuna watu ambao wanafuga kuku au walishawahi kufuga kuku...naomba watU wenye uzoefu na maarifa kuhusu kufuga kuku,,wanipe mawazo, maana nataka kuanza kufuga kuku na sijawahi kufanya hivyo, hivyo nahitaji mawazo yenu wakuu.

Natanguliza shukrani zangu wakuu:
 
Kuna thread moja ilianzishwa na Mama Joe ilikuwa inaongelea mambo ya ufugaji wa kuku. Wadau walichangia sana kwenye hiyo thread. Itafute humu ndani utapata mawazo yote unayohitaji kuhusu ufugaji wa kuku aina zote.
 
Hivi kwani hujaanza kufuga mpaka leo au mambo yameingiliana??

Mipango, matahalani mie nilikuwa namsaka mtaalamu wa kufundisha ufugaji wa kisasa kwa kuku hawa kienyeji nimewasiliana na wadau wa Breakthrough business support kwa muda wamekuwa wakitoa sababu lukuki za kutopatikana na hatimaye hivi sasa hawapokei simu yangu! Jaribuni na nyie wenzangu 0656 004001 ama 0656 004002

Naomaba atafutwe mtaalamu atengeneze Darasa la weekend moja. Tuko tayari kumlipa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom