kipindupindu
JF-Expert Member
- Dec 16, 2010
- 1,053
- 170
kwa muda wa miezi 6 iliyopita nimekua katika harakati za kukusanya coins za shilingi moja za kitanzania na kufanikiwa kupata jumla ya shilingi mia mbili,niliamua kwenda dukani kununulia sabuni bila mafanikio kwa sababu kila duka nilililopita niliambiwa hizi hela hazitumiki.katika kumbukumbu zangu sikuwahi kusikia tangazo kutoka bank kuu ya tanzania kwamba fedha hizi sio halali kutumika.naomba tujadili kwa nini fedha hii halali ya kitanzania haikubaliwi na wafanyabiashara?