Kwa nini Waafrika tunabuguana wenyewe kwa wenyewe na kuoneana gere?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,620
46,261
Ukiangalia makubaliano, tenda na mikataba mbalimbali ya kibiashara ambayo nchi za Africa huwa zinaingia na nchi au hizo kampuni za nje kutoka Ulaya, Marekani, China, Uarabuni n.k ni ya kunufaisha zaidi hizo nchi na kampuni ila Waafrika wenyewe kwa wenyewe kukubaliana katika mambo ya kibiashara ambayo yatanufaisha Waafrika wenzao ni vigumu sana. Yani Waafrika ni kama tunaona bora zaidi mtu wa bara lingine apate lakini Mwafrika mwenzetu jirani akose!

Kwa mfano nimeona Ruto amemteua Mdachi kuwa Chancellor wa Chuo kikuu cha Nairobi lakini sio rahisi kabisa kwa Mwafrika mwingine tofauti na Mkenya kuteuliwa kushika nafasi chuo katika hiko. Rwanda walikuwa wanapokea wakimbizi kutoka Uingereza wakati Africa imejaa wakimbizi, TANESCO walienda kuchukua kampuni ya IT huko India wakati Kenya na Rwanda kuna kampuni za IT zinafanya vizuri sana, Kuna wakati Kenya ilizuia maziwa ya Uganda lakini ukienda maduka ya Kenya kuna maziwa ya Ulaya na Uarabuni!

Mifano ni mingi sana, Waafrika inabidi tujitafakari katika kufanya biashara pamoja kwa ushirikiano kati yetu sisi zaidi kuzidi mataifa ya mabara mengine. Tunahitaji kuelewa fursa ya biashara kati ya mataifa yetu ina faida kubwa zaidi kuliko na mataifa ya mbali.
 
Akili za Mwafrika hazieleweki.Ndiyo maana amejitungia yafuatayo:-
-viazi ulaya
-mitaa ya uzunguni/uhindini
-kwenda na muda kama mzungu
-kula kidogo kama mzungu
-amependeza na mzuri kama mwarabu n.k.
Kwa ufupi ni kutojiamini na kutoaminiana,kubaguana,kuchukuliana kama daraja la chini,kuchukiana bila sababu na hat kudharauliana tu.Anyway,(nimeweka kizungu hapo ili kukutisha)naomba chai nusu kikombe ninywe.Nina pua ndefu kama "mzungu" nachelea kuungua.
 
Akili za Mwafrika hazieleweki.Ndiyo maana amejitungia yafuatayo:-
-viazi ulaya
-mitaa ya uzunguni/uhindini
-kwenda na muda kama mzungu
-kula kidogo kama mzungu
-amependeza na mzuri kama mwarabu n.k.
Kwa ufupi ni kutojiamini na kutoaminiana,kubaguana,kuchukuliana kama daraja la chini,kuchukiana bila sababu na hat kudharauliana tu.Anyway,(nimeweka kizungu hapo ili kukutisha)naomba chai nusu kikombe ninywe.Nina pua ndefu kama "mzungu" nachelea kuungua.
Inakera sana kwenye nchi nyingi za Africa unakuta Wazungu, Wachina na Waarabu katika huduma nyingi wanapata hospitality nzuri kuliko wewe Mwafrika.
 
Sisi watu weusi tuna laana ambayo haitakaa iishe, tuna ubinafsi, roho mbaya na chuki.

Ukitaka kuthibitisha hilo angalia kwenye vituo vya mwendokas wale maaskari wanavyopata shida kusimamia abiria wapange foleni. Hapo ndo utajua mtu mweusi hawezi kujiongoza
 
Ukiangalia makubaliano, tenda na mikataba mbalimbali ya kibiashara ambayo nchi za Africa huwa zinaingia na nchi au hizo kampuni za nje kutoka Ulaya, Marekani, China, Uarabuni n.k ni ya kunufaisha zaidi hizo nchi na kampuni ila Waafrika wenyewe kwa wenyewe kukubaliana katika mambo ya kibiashara ambayo yatanufaisha Waafrika wenzao ni vigumu sana. Yani Waafrika ni kama tunaona bora zaidi mtu wa bara lingine apate lakini Mwafrika mwenzetu jirani akose!

Kwa mfano nimeona Ruto amemteua Mdachi kuwa Chancellor wa Chuo kikuu cha Nairobi lakini sio rahisi kabisa kwa Mwafrika mwingine tofauti na Mkenya kuteuliwa kushika nafasi chuo katika hiko. Rwanda walikuwa wanapokea wakimbizi kutoka Uingereza wakati Africa imejaa wakimbizi, TANESCO walienda kuchukua kampuni ya IT huko India wakati Kenya na Rwanda kuna kampuni za IT zinafanya vizuri sana, Kuna wakati Kenya ilizuia maziwa ya Uganda lakini ukienda maduka ya Kenya kuna maziwa ya Ulaya na Uarabuni!

Mifano ni mingi sana, Waafrika inabidi tujitafakari katika kufanya biashara pamoja kwa ushirikiano kati yetu sisi zaidi kuzidi mataifa ya mabara mengine. Tunahitaji kuelewa fursa ya biashara kati ya mataifa yetu ina faida kubwa zaidi kuliko na mataifa ya mbali.
Sio Waafrika, sema Watu weusi ambao ni wajinga sana na Wabinafsi kuliko race yoyote duniani
 
Back
Top Bottom