Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Kila nikikaa na kuangalia naona yale makeke ya Chama kinachojiona ni cha pili kwa Upinzani hapa Tz (CHADEMA) yamefulia na kupooza.
Baada ya kupigwa mkwala wa hali ya juu na Serikali kule Arusha na baadhi ya viongozi wao kubamizwa kwenye kona kwa kupelekwa kortini kujibu tuhuma za kuwalazimisha watu au kuwashawishi watu kufanya maandamano yaliyopigwa marufuku na jeshi la polisi ,maandamano ambayo yalikuwa na agenda za siri ambazo zilidakwa na wajeshi hao wa usalama wa raia na mali za wananchi.
Hadi hii leo baada ya Chadema kuona hali imewakalia vibaya kwa upande wa washtakiwa wao sasa wamekuja chini na kufulia kabisa ,yaani huwezi kuamini kuwa WaTz wengi nikiwemo mimi tulikuwa tumeanza kujenga matumaini ya mkombozi mpya yaani kwa lugha za kisasa tunaweza kusema mkombozi mbadala ,matumaini kwa wazalendo yamefifia na kuzama kabisa baada ya kuona kile Chama wanachokitegemea kwa ukakamavu wawapo majukwaani ni magoigoi na kitisho kilichotolewa na serikali kusambaratisha maandamano yao kimewafanya wasinyae kabisa na kuwa cool.
Baada ya kupigwa mkwala wa hali ya juu na Serikali kule Arusha na baadhi ya viongozi wao kubamizwa kwenye kona kwa kupelekwa kortini kujibu tuhuma za kuwalazimisha watu au kuwashawishi watu kufanya maandamano yaliyopigwa marufuku na jeshi la polisi ,maandamano ambayo yalikuwa na agenda za siri ambazo zilidakwa na wajeshi hao wa usalama wa raia na mali za wananchi.
Hadi hii leo baada ya Chadema kuona hali imewakalia vibaya kwa upande wa washtakiwa wao sasa wamekuja chini na kufulia kabisa ,yaani huwezi kuamini kuwa WaTz wengi nikiwemo mimi tulikuwa tumeanza kujenga matumaini ya mkombozi mpya yaani kwa lugha za kisasa tunaweza kusema mkombozi mbadala ,matumaini kwa wazalendo yamefifia na kuzama kabisa baada ya kuona kile Chama wanachokitegemea kwa ukakamavu wawapo majukwaani ni magoigoi na kitisho kilichotolewa na serikali kusambaratisha maandamano yao kimewafanya wasinyae kabisa na kuwa cool.