Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,867
- 41,937
Zama hizi, utambulisho mkubwa wa CCM kwa jamii ni UOVU. CCM inaonekana ni chama ambacho kipo kwaajili ya kujenga, kulinda na kuendeleza uovu na waovu:
1. UKOSEFU WA UZALENDO:
Watuhumiwa wote wa kupora na kuuza rasilimali za Taifa kama bandari, mbuga za wanyama na hifadhi za misitu ni viongozi wa CCM.
2. RUSHWA
Siku zote watuhumiwa wakuu wa rushwa, ukichunguza, utakuta ama ni viongozi, makada au wafadhili wakuu wa CCM.
3. UPORAJI
Watuhumiwa wote wa uporaji wa mali za watu kwa kutumia madaraka, siku zote ni viongozi wa CCM.
4. WADHULUMAJI WA HAKI
Watuhumiwa wa udhulumaji wa haki za wananchi, kuanzia udhulumaji wa haki za watu za kuishi (wauaji) mpaka mali za watu kama vile pesa na ardhi, ni viongozi, makada, wapambe na wafadhili wa CCM.
5. UDIKTETA
Madikteta na wapenzi wa udikteta, wasiotaka uchaguzi ulio wa haki na huru, wasiotaka katiba nzuri yenye kulinda haki ya kila mwananchi, wanaotaka mahakama na Bunge viwe idara za kupokea maelekezo toka CCM, badala ya kusimamia haki, wote ama ni viongozi, makada au wanachama wa CCM.
6. SIASA ZA UWONGO, UNAFIKI NA ULAGHAI.
Wanasiasa na viongozi waongo na laghai, wamejaa CCM. Tena kwao ukisikia wanasema kuwa fulani ni mwanasiasa hasa, wanamaanisha ni mwongo na laghai sana.
7. UFISADI
Zile reports za CAG, zinazoonesha ufisadi mkubwa ndani ya serikali na taasisi zake, wahusika wote ni viongozi, makada na wanachama wa CCM. CCM inaliamgamiza Taifa, na kwa vile wote ni mazao ya uovu, hakuna wa kupambana na uovu.
CCM inajipambanua kwa uovu badala ya wema mbele za wananchi. Kwa nini imekuwa hivyo? Ni shetani gani ameingia CCM kiasi cha kuifanya CCM ionee fahari uovu badala ya wema? CCM sasa imeanza kulifuta taifa taratibu. Taifa ambalo rasilimali zake zote zinapowa na wageni, ni Taifa marehemu, maana wananchi wake watakuwa katika ardhi yao lakini wakiishi kama wageni. Huku ndiyo kufa kwa Taifa.
Viongozi wetu mliotangulia mbele za haki, Julius, Benjamin na John, pamoja na mapungufu yenu, lakini tuna uhakika mlilipenda Taifa hili, msingependa Taifa hili, siku moja rasilimali zake ziporwe kiasi cha kutishia uhai wake huko mbeleni, kama inavyofanyika. kwa maombi yenu na ya wote wenye dhamira njema, waliotangulia na walio hai, yamfikie aliyetupa huu urithi, naye atujalie ujasiri wa kuukataa uovu huu unaolipeleka Taifa kwenye maangamizi.
1. UKOSEFU WA UZALENDO:
Watuhumiwa wote wa kupora na kuuza rasilimali za Taifa kama bandari, mbuga za wanyama na hifadhi za misitu ni viongozi wa CCM.
2. RUSHWA
Siku zote watuhumiwa wakuu wa rushwa, ukichunguza, utakuta ama ni viongozi, makada au wafadhili wakuu wa CCM.
3. UPORAJI
Watuhumiwa wote wa uporaji wa mali za watu kwa kutumia madaraka, siku zote ni viongozi wa CCM.
4. WADHULUMAJI WA HAKI
Watuhumiwa wa udhulumaji wa haki za wananchi, kuanzia udhulumaji wa haki za watu za kuishi (wauaji) mpaka mali za watu kama vile pesa na ardhi, ni viongozi, makada, wapambe na wafadhili wa CCM.
5. UDIKTETA
Madikteta na wapenzi wa udikteta, wasiotaka uchaguzi ulio wa haki na huru, wasiotaka katiba nzuri yenye kulinda haki ya kila mwananchi, wanaotaka mahakama na Bunge viwe idara za kupokea maelekezo toka CCM, badala ya kusimamia haki, wote ama ni viongozi, makada au wanachama wa CCM.
6. SIASA ZA UWONGO, UNAFIKI NA ULAGHAI.
Wanasiasa na viongozi waongo na laghai, wamejaa CCM. Tena kwao ukisikia wanasema kuwa fulani ni mwanasiasa hasa, wanamaanisha ni mwongo na laghai sana.
7. UFISADI
Zile reports za CAG, zinazoonesha ufisadi mkubwa ndani ya serikali na taasisi zake, wahusika wote ni viongozi, makada na wanachama wa CCM. CCM inaliamgamiza Taifa, na kwa vile wote ni mazao ya uovu, hakuna wa kupambana na uovu.
CCM inajipambanua kwa uovu badala ya wema mbele za wananchi. Kwa nini imekuwa hivyo? Ni shetani gani ameingia CCM kiasi cha kuifanya CCM ionee fahari uovu badala ya wema? CCM sasa imeanza kulifuta taifa taratibu. Taifa ambalo rasilimali zake zote zinapowa na wageni, ni Taifa marehemu, maana wananchi wake watakuwa katika ardhi yao lakini wakiishi kama wageni. Huku ndiyo kufa kwa Taifa.
Viongozi wetu mliotangulia mbele za haki, Julius, Benjamin na John, pamoja na mapungufu yenu, lakini tuna uhakika mlilipenda Taifa hili, msingependa Taifa hili, siku moja rasilimali zake ziporwe kiasi cha kutishia uhai wake huko mbeleni, kama inavyofanyika. kwa maombi yenu na ya wote wenye dhamira njema, waliotangulia na walio hai, yamfikie aliyetupa huu urithi, naye atujalie ujasiri wa kuukataa uovu huu unaolipeleka Taifa kwenye maangamizi.