AshaDii
Platinum Member
- Apr 16, 2011
- 16,190
- 18,080
Habari wana JF,
Kawaida kama wanadamu huwa tunakuwa na matarajio ya vitu mbali mbali, na matarajio hayo huegemea tokana na viashiria vinavyowezesha haya matarajio ku materialise. Tumetofautiana katika kusoma viashiria hasa pale amapo viashiria hivyo kuwa ni vya ku donoa donoa! Ingawa kuna viashiria vingine ambavyo huonesha WAZI kabisa kuwa matarajio ni haya iwe kwa kupenda ama kutopenda kwa watazamaji wote. Tokana na nyenendo, habari na matukio yanayotokea siku zote nchini kwetu hasa kwa yale yanayohusiana na masuala ya Siasa yananipa kutoa mtazamo huu nilotoa katika makala hii.
Ni wazi kuwa idadi kubwa ya Watanzania (na hata mataifa mengine baadhi) tunasubiri kwa hamu kuona na kushuhudia shughuli za uchaguzi mkuu 2015. Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania toka ipate uhuru mwaka 51 iliyopita itakuwa na idadi kubwa zaidi ya wanaharakati, wakereketwa na wafuasi wa vyama, wananchi wa kawaida kuvutiwa na kuwa na hamu kubwa kujua hatma ya uchaguzi na kama uongozi mkuu wa nchi utachukuliwa na Chama Pinzani ama bado kitabaki Chama tawala madarakani. Ni matumaini yangu hata idadi ya wapiga kura itaongezeka kuliko miaka ya nyuma.
Hakuna ubishi kuwa uchaguzi mkuu wa 2015 utakuwa ni kabambe, wenye kuvutia na wa muhimu pengine kuliko chaguzi nyingine zote zilizowahi kutokea. Ni uchaguzi ambao kubwa litakalotawala ni kutaka kwa shauku kuona ni nani hasa atashinda kiti cha Urais. Kwenye akili na fikra za wengi pengine hata haitajalisha na wala kutokuwa na nguvu huyo rais atakuwa ni nani; bali lenye nguvu ni kuona rais huyo atakuwa wa chama gani. Je, Chama Cha Mapinduzi bado kitakuwa kinashikilia nchi ama Wapinzani? 2015 baada ya uchaguzi ndiyo tutapata jibu kamili la swali hilo!
Hata hivyo licha ya kuwa baada ya Uchaguzi huo mkuu ndiyo tutakuwa na jibu kamili. Ukweli unabaki kuwa kuna vitu/viashiria/matendo ya vyama husika ambavyo hutoa picha kwa Wanaharakati, Wanasiasa, Wakereketwa na Wafuasi; ya kuwa Chama gani kinaonekana kinara na wana nafasi ya kuweza kushinda kiti hicho katika Uchaguzi.
Kila mmoja toka katika hayo makundi tajwa huwa na vigezo na sababu ambazo humpelekea aamini ushindi ni wa nani. Kwa mantiki hiyo siyo ajabu ukikutana na watu wawili wakawa na mawazo tofauti huku kila mmoja akiamini wazo lake ndiyo sahihi. Katika hili ambacho kinaweza toa mwanga na sababu ya kuamini mmoja kuliko mwingine ni tokana na sababu zake ambazo ataainisha kwa hoja ambazo yastahili ziwe nzito.
Maandalizi na mikakati ya kushika Uongozi wa juu wa Serikali huwa ni mzito na wakimahesabu na kwa maandalizi thabiti yaliyo jipanga vyema. Maandalizi hayo hayafanywi kwa siku moja, hayafanywi in Isolation na wala hayawezi fanikiwa kwa kubahatisha. Inahitaji nguvu ya Chama, nguvu ya uongozi wa Chama na kubwa zaidi nguvu ya wanachama ambao ndiyo Umma na ndiyo wana wajibu wa kumweka mtu katika kiti hicho kwa njia ya kura wakati wa Uchaguzi.
Hivyo basi kuna makundi matatu (Tokana na Mtazamo wangu) yanayotoa picha ya uchaguzi utakuwa vipi hasa:
A]. Kundi la wapiga Kura ambao ndiyo wananchi.
B]. Kundi la Chama Cha Mapinduzi ambacho ndio chama tawala.
C]. Kundi la wapinzani wakuu; kwa maana ya CHADEMA ambao wamekuwa ni wapinzani wakuu.
KUNDI LA WAPIGA KURA
Historia Kujirudia (hasa ya 2005)
Kuna kila dalili kwamba historia ya 2005 inaweza kujirudia i.e. watanzania wengi watakuwa wamejiandikisha kupiga kura ila wachache watakaopiga kura. Hata hivyo izingatiwe kuwa hili linaweza epushwa ama kupunguzwa kwa kiasi kikubwa kama: Kwanza iwapo Vyama pinzani, Vyombo Vya habari na Wanaharakai wa Demokrasia wataweza kuhamasisha wananchi juu ya umuhimu wa kujiandikisha kwa nguvu zaidi, na Pili ni kwa CHADEMA kuja na candidate mzuri, mashuhuri, mwenye experience ya kutosha ambaye ataweza himili na kushindana vyema na mgombea urais wa chama pinzani.
Kutokujifunga kwa wapiga kura
Watanzania wengi ambao ni wapiga kura na wanao kuwa na vitambulisho vya kupiga kura kwa nia hiyo ya kujiandikisha hawapo katika chama chochote, ni wachache ambao wapo katika vyama kwa maana ya kuwa yupo chama Fulani. So far, tunaona CHADEMA nguvu ya kuongeza wapiga kura ipo katika kubanana na hao ambao tayari ni wanachama wa CCM na wale wasio na chama ambao wanawapata pia. Tokana na furaha ipatikanapo pale wanapo faulu kuwavuta wana CCM wengi kuja Chadema inapelekea kuonekana kana kwamba Strategy yao ipo katika kuhakikisha wanachama wa CCM wanahamia CHADEMA badala ya nguvu katika kuhakikisha wanajenga &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];loyalties' kwa kuwavuta wale wasio na chama.
Woga wa Mabadiliko
Kura nyingi zipo vijijini, na wengi wao ni CCM ingawa inaenda inapungua na ni kwa sababu sio tu kwa sababu hawana upeo au elimu ya uraia bali by default, watu maeneo ya vijijini huwa ni &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];conservatives'. Hawapendi mabadiliko na ni waoga wa mabadiliko, wapo katika hali mbaya lakini bado wana amini kuwa uongozi mwingine unaweza waangamiza zaidi na kabisa.
Ukichanganya hili na kwamba tangia kupata uhuru wengi wanaishi maisha ya kujitosheleza (pa kulala, chakula, nguo) hivyo wao hawaguswi sana na matatizo ya kiuchumi kama wale wananchi ambao wapo mijini wanaotegemea formal, monetary and market based economy kuendesha maisha yako ya kila siku. Vijijini ni moja ya sababu CCM itaendelea kushinda urais na kama katika ngazi ya ubunge, ikitokea upinzani unapata kura za vijijini basi ni kutokana na wananchi husika kuvutiwa na mgombea ambae ni msomi, makini n.k. Ikiwa ni sifa ya kutukuka miongoni mwao (mfano labda Mnyaturu) kuonesha hata wao pia wana wasomi wa kuwang'arisha katika anga za siasa za nchi na siyo tu Wanyakyusa, Wachaga, Wahaya n.k wanaweza kuwa hivo.
KUNDI LA CHAMA CHA MAPINDUZI
Ni mengi ambayo Serkali ya CCM imewakosea na inaendelea kuwakosea wananchi wake, kukiwa na matukio ya kuudhunisha, sikitisha, katisha tamaa kila kunapo kucha! Hakuna unafuu popote pale na Serkali imekuwa kama imefuzu katika kupiga kote kote kwa wananchi tena panapo uma! Haya yamekuwa yakiendelea siku zote na bado yanaendelea kwa miaka kadhaa sasa.
Kwanza tujiulize ni kwa namna ipi CCM wame survive hadi hapo walipo?! Tuache yote hayo na tuanzie pale ambapo tulipata orodha ya "List of Shame" toka kwa Dr. Slaa, Orodha iliyotikisa na kusababisha viongozi hao wa juu kumaka kumfungulia kesi Dr. Slaa - suala ambalo halijafanikiwa hadi leo. Ile Orodha ilikuwa ni tosha kabisa kuwa hamasa kwa wananchi na wanaharakati kuing'oa CCM kwenye uchaguzi wa 2010. Lakini haikuwa hivyo...
Katika miongo ya miaka kumi kumekuwa na transparency kwa kiwango cha jamii nzima kujua madhaifu ya Serkali ya CCM juu ya Ufisadi uliyo kithiri kama pesa za Uswizi, Mikataba ya Madini yenye walakini kama vile wa Buzwagi, Magumashi na rushwa zilizokithiri katka utendaji kama masuala ya EPA na Richmond.
Kumekuwa na kuongezeka kwa matukio katika jamii dhidi ya wanajamii na vyama pinzani. Tumeona ni namna ipi Serkali imekuwa ikitumia vyombo vya Ulinzi na Usalama wa wananchi kwa kuharibu huo huo usalama wa wananchi na ni suala la kusikitisha kuwa tumepoteza watu katika jamii kwa kuonewa, kimakosa ama kukosa umakini wa utendaji wa vyombo hivyo vya usalama. Hali zinazidi kuwa mbaya karibu katika taasisi zote za ambazo Serkali ina wajibu wa kusimamia na kuhakikisha hali ni nzuri na huduma stahili zinatimizwa na kuwafikia wana nchi. Elimu, Uchumi, Afya, Usalama na mengine mengi yanazidi kuzorota huku Serikali ikizidi kujitazama yenyewe pamoja na viongozi wake wakuu. Kazi na nguvu yao ya Ziada kubwa imeelekezwa katika kuhakikisha wapo katika uongozi huo wa juu daima. Hili linafanya Serikali kufanya kila wanalo weza katika kuhakikisha wanafanikiwa.
Mbaya zaidi kumekuwa na kuongezeka kwa kasi juu ya suala la "Udini", tena basi udini huo ukisababishia ukosefu wa amani, uharibifu wa mali na kupoteza kwa maisha ya wananchi na viongozi wa dini. Chuki kati ya Waislamu na Wakristo inaenda kukuzwa tena kwa kubembeleza sababu tu Serkali kwa udhaifu mkubwa imeshindwa kabisa kudhibiti na kukomesha udini huo. Hali na sasa inaonesha kuwa &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];future' na usalama wa nchi ni walakini sana. Sad.
Hawajali kuwa wanawaumiza wananchi, hawajali kuwa inatoa implication gani kwa Wanasiasa, Wanaharakati, Wakereketwa na Wafuatiliaji wa mambo. Inafanya kutoa maamuzi ya kujikoroga kama vile la kujadili Bungwe lisiangaliwe 'Live' na mra tena kubadilisha msimamo. Na pia inafanya Serikali kutoa maamuzi ambayo kimsingi na kimantiki hayaeleweki; kama vile kuvunjwa kwa POAC. Ukichukulia uzito na umuhimu wa Kamati yenyewe ikiwa ilikuwa inaangalia na kufuatilia asset zenye thamani ya trillion za shilingi, inafanya kuamini kuwa ni mtu asiye na akili tu ndiyo anaweza futa ama kukubali ifutwe LA SIVYO zinatakiwa sababu za Msing sana kuwakilishwa.
Hata hivyo pamoja na matendo ya kidhaifu hayo yote, ukweli (kwa mtazamo wangu) unabaki kuwa kwa hali ilivyo sasa kisiasa ikiambatanishwa na matendo, attitude za wananchi na baadhi ya Viongozi pia na matukio infanya niamini kuwa 2015 CCM bado wana uwezo wa kuwa vinara wa Uraisi hata kama ni kwa asilimia ndogo kuliko siku zote za chaguzi kwa sababu hizi zifuatazo;
Wamejipanga Vyema
Kujipanga haijialishi ni njia ipi unatumia, kama ni chafu/safi, halali/si haliali, haki/siyo haki - inachojalisha ni mipango yako kuweza kufanikisha azma ya malengo ya mipango hiyo. Serikali ya CCM imekuwa hodari katika kuhakikisha inatengeneza mazingira wezeshi kwa wao kuweza kushinda uchaguzi mkuu ujao. Wamejitosheleza vyema katika Nyanja mbali mbali, tokana na vita baridi waliyo nayo dhidi ya wapinzani wao wakuu CHADEMA. Wamejikita katika kujizatiti kuwanyong'onyeza nguvu CHADEMA kwa kila namna inayowezekana hasa kwa kutumia madhaifu yao.
Viongozi wao wamekuwa wakijitahidi na kuweza kufanya kazi hiyo ya kwa bidii, Tumeona namna shutuma za CHADEMA kuingia mikataba na Wafadhili wa mabillioni ya shilingi (Sijui hii kesi iliishia wapi?); Tumeona suala la Kadi ya CCM ya Dr. Slaa vile ilisambaa katika vyombo vya habari ambayo mwanzo ilichukuliwa kwa wepesi na hatimaye kuweza ku 'divert' attention ya baadhi ya viongozi wa CHADEMA kwa kulitatua tatizo badala ya kuangalia mambo mengine ya msingi na yalo na tija kwa shughuli za Chama.
Wapo juu ya Taasisi
Wamekuwa wapo juu ya taasisi mbalimbali ambazo ni mhimu, msingi na kugusa jamii kwa upana. Tukiacha taasisi nyingine zote tuangalie taasisi ya Bunge letu tukufu kwa namna ambavyo limekuwa likiendishwa kwa matakwa ya Chama Cha Mapinduzi. Kumekuwa na sarakasi nyingi Bungeni hadi kupelekea lawama zilizo kithiri dhidi ya Madame Anne Makinda na ndugu Job Ndugai tokana na matendo yasiyowaridhisha wabunge wengi na wananchi kwa ujumla. Kubwa kuliko hapa karibuni kumefutwa na kuvunjwa kwa Kamati mbili (1) Kamati ya Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje iliyokua inaongozwa na Edward Lowassa na (2) Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) iliyokuwa inaongozwa na Zitto Zuberi Kabwe ambayo ilifutwa kabisa. Inaleta uwalakini sana 'timing' ya events hizi hasa tokana na kuwa ripoti za kamati hizo zilikuwa zikae wiki chache baada ya tukio. Ikumbukwe ripoti ya mwisho ya Zitto ilipeleka kura ya kutokuwa na Imani kwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda na hivo kusababisha kusimamishwa kwa mawaziri 8.
Katiba (ya sasa) inasimama upande wa Serikali iliyopo Madarakani
Katiba mpya ilitakiwa ipatikane walau 2010 ili kuwe na miaka walau mitano ya utawala chini ya Katiba mpya ili kufikia 2015, mabadiliko mengi yawe tayari yamejitokeza katika kila Nyanja hivyo kuisaidia CHADEMA na vyama vingine pinzani. Vipengele vingi vya katiba ya sasa vinakumbatia na kulinda nafasi za Uongozi uliyopo madarakani tokana na wajibu na majukumu yaliyo ainishwa kwa mujibu wa katiba. Nje ya nafasi ya Rais ambazo ni nzito na nyeti (Kama vile Mkuu wa Serikali nan chi; Amiri Jeshi Mkuu wa vikosi vya usalama na Ulinzi; Ana mamlaka ya kutaifisha mali yoyote; Ndiye anayeteua viongozi wakuu akiwemo na Jaji mkuu, wakuu wa vyombo ya ulinzi na Usalama n.k); Pia ndiye ambae anawajibika kuteua Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano ambayo ndiyo tegemezi katika chaguzi kuu.
Madhaifu ya Rais Jakaya Kikwete
Katika ila tatizo, kila uozo, kila ufisadi ama uchemvu uliotokea lawama zote zimekuwa zikienda kwa Rais JK. Hilo limepelekea kutamkwa kwa wengi wa wanaharakati, wanasiasa, wananchi na wakereketwa kuwa ni 'Udhaifu wa Kikwete'. Hii kauli inatowa picha kuwa katika akili za wengi matatizo yoote tuliyo nayo ni kana kwamba yalikuwepo tu baada ya JK kushika Urais na hayakuwepo awali. Rais Kikwete amekuwa akilaumiwa kwa matatizo yote yaliyopo toka Ufisadi, Kutowajibika, Kuangamiza nchi kuliko Serkali yake ya CCM. Kwa maana nyingine hili linaweza kupelekea Kingozo Mkuu (rais) toka CCM akapokelewa kwa mikono miwili kwa kuamini kuwa atairudisha CCM katika mstari.
KUNDI LA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
Chadema wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha wananchi wanatambua umuhimu wa Demokrasia hasa kwa njia ya mikutano na harakati za Movement for Change (M4C) ambazo zimekuwa zikifanywa katika kila maeneo ya nchi. Jitihada zao na 'results' ya hizo harakati zimekuwa wazi kiasi kwamba zimefanya viongozi wa CCM (hasa wa kitengo hicho) kuhangaika usiku na mchana namna ambayo wanaweza kuwachafua na kuwanyong'onyeza Chadema.
Imefanya kuwajengea baadhi ya Wanachadema kuamini kuwa CCM wanatishika na Slaa to the extent ambayo they are potraying, Imefanya kuzuka kwa kashfa mbali mbali dhidi ya Dr. Slaa nyingi zikiwa hazina tija wala mantiki.
Imefanya wajikite na kwa kiasi Fulani kuweza kuwayumbisha Chadema kwa kuingilia kupitia vipandikizi wao maslahi ya Chama. Kwa kiasi kikubwa Chadema wamefaulu katika kuwawezesha viongozi wengi wa CCM na serkali yenyewe kukosa usingizi. Hiyo ni 'achievement' kubwa sana; Lakini hata hivyo Chadema wanatakiwa wajitazame upya kuweza kuhakikisha wanajipanga, jikita na kuhakikisha kuwa wanashinda uchaguzi mkuu 2015.
Bado tuna miaka miwili hadi Uchaguzi mkuu kama mambo yataenda inavyostahili. Ni muda tosha wa Chadema kuweza kufanya mabadiliko. Ninachoweza kusema, hadi hapa tulipo kwa mtazamo wangu Chadema bado wana kazi kubwa kuweza kuhakikisha inafanikiwa, naamini kuwa ni muhimu wajitazame wapi nut zimelegea na wakaze katika maeneo yote husika ili kuhakikisha yanatolewa ama kufutwa kabisa.
Wameingia mtego "Siasa za Ligi na Mipasho" dhidi ya CCM
CCM ikiwa kama chama ambacho ni kikongwe na kimejijenga kuliko CHADEMA ambayo ni changa, wana nafasi kubwa, watu wa kutosha na walio jidhatiti hapo kwa ajili ya kuendesha ligi za mipasho na kushindana kwa kutafuta kwa udi na uvumba kitu gani kinaweza ivunja nguvu CHADEMA ambayo inakuwa siku kwa siku na kuonekana dhahiri kuwa ni tishio kwa CCM.
Tatizo ni kwamba CCM ni mabingwa wa Siasa za FITINA, wana uzoefu mkubwa sana katika hili hata katika siasa za ndani ya chama; CHADEMA hawana ujuzi huu na hilo litawagharimu kwani kuna kura nyingi sana ambazo zinapatikana kwa fitina, sio kwa kupitia tu nguvu ya hoja au ukweli diama fitina mwiko, kwani watanzania wengi ni mashabiki wa siasa za matukio na vituko CHADEMA wameshindwa kuja na counter strategy ya siasa za fitina kama vile za akina Nchemba, Nape na wengineo. Wananchi wengi hasa vijijini ambako ndio kuna kura nyingi - wananunua hoja za Nchemba (haijalishi wamepewa Tisheti ama lah) kuliko tunavyofikiri kwani wengi ni illiterate and ignorant.
Centralisation ya Uongozi toka Kaskazini
Inawezekana kabisa hili halikuwa kwa lengo mbaya; Lakini ni muhimu tukaelewa kwamba kwa kipindi kufikia 2010, inawezekana ilikuwa ni lazima CHADEMA kufanya hivyo kwani bado kilikuwa hakina true loyalists wengi kutoka maeneo mengine ya nchi wenye uwezo na uzoefu katika masuala ya uongozi. Ni suala ambalo CHADEMA haiwezi sema kwa jamii LAKINI ni muhimu pakawepo na mbinu mpya ya kuhakikisha hii imani ya kuwa ni "Chama cha Kaskazini" inatutwa na kufa kabisa.
Pia waeleze kuwa sasa wameshapata watu wengi wenye uwezo na muda ukifika Watanzania watajionea ni namna ipi CHADEMA itadhihirisha kwa uma kuwa Chama siyo cha Kaskazini bali cha Watanzania wote. CHADEMA wakiwa makini na wakajipanga wanaweza tumia dhaifu hili la ukanda "Kaskazini" kama strength, huku waki appeal kwa umma kwamba wawapatie watu makini toka maeneo mbali mbali ya Mkoa ili wawe msaada kwa Chama na wananchi ambao wanawataumikia. Kama ilivyo wazi hapa karibuni, Umaaruru wa Chadema umekuwa ukikuwa na kusambaa karibu nchi nzima. Hili pia linaweza punguzwa kwa kuangalia nafasi za viongozi na wajibu walio nao hasa katika Chama. Naamini kuna Watanzania wengi wana uwezo wa kuwa viongozi, inakuwa haina mantiki mtu mmoja anapokuwa na vyeo ziaidi ya Vitano na hali anaweza saidiwa na kupunguziwa majukumu.
Mapungufu makubwa ya Movement for Change (M4C)
Madhaifu ya M4C ambayo inaonesha inatokana na upungufu wa mfuko wa pesa kuweza kuendeshea. Namna harakati za M4C zilianza ni tofauti na sasa. Pengine tokana na kuchafuliwa kwake kwa kuhusishwa na vurugu ama lah, ila kama CHADEMA wana niya ya kushika Urais inabidi kuongeza nguvu na kasi katika harakati hizi.
Pia M4C imekuwa ikitumia nguvu kubwa katika kuichongea serikali ya CCM kwa uma kuliko kuhakikisha na kupigania idadi ya wapiga kura inaongezeka; Lengo ilitakiwa iwe kuhamasisha wananchi kujiandikisha kupiga kura huku chama kikijenga uwigo mpana na kukuwa idadi ya wana CDM na pia kujenga database yake mpya ambayo ingetumia katika tathmini za uchaguzi mikuu iliyopita nay a sasa
Kujenga kwa maadui wasio na Tija
CHADEMA wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha nidhamu inafanyika na viongozi wao na dhidi ya viongozi na wananchi pia. Hata hivo kwa mtazamo wangu wamekuwa haraka sana katika maamuzi ya kuchukua hatua ya kufukuza mara moja viongozi wao hadi pengine kutilia mashaka kama kweli huwa kuna chunguzi za dhati huwa zinafanywa dhidi ya watuhumiwa hao. Tayari tumeona reactions za akina Chriss Lukosi, Juliana Shonza, Mtela Mwampamba - Hawa watu walikuwa ni viongozi wa CHADEMA, hivo ina maana wanawajua vema. Ni wazi kuwa mtu ambaye ni adui mkuu ni Yule akujuae vema, maana anajua wapi pa kubofya.
Kupokea kwa Oil Chafu toka CCM
Ni ajabu sana kuwa CHADEMA wapo haraka sana katika kupokea viongozi toka chama kingine (hasa cha wapinzani wao wakuu CCM) kwa mbwembwe na matangazo. Utata unakuja pale ambapo huyo aliyejitoa CCM ni Kiongozi na akifika CDM anapewa uongozi; Hiyo ni hatarishi kama huyo mtu ni pandikizi, pia kwa namna moja ama nyingine kuwanyima haki wale ambao wanaweza hiyo nafasi nje ya huyo mgeni. Hili litatokea na ni moja ya mambo ambayo yataigharimu CHADEMA urais 2015; CHADEMA wanaweza kuepuka kuwa chama chakupokea wale wote ambao wanaogopa kusimama kama wagombea wa CCM e 2015 kutokana na nguvu ya CHADEMA
Bahati mbaya siyo kutokana na Mapenzi juu ya CHADEMA na taifa, bali kwa nafsi na ubinafsi wao. Ni muhimu CHADEMA wakaliangalia upya hili; pengine CHADEMA waje na tamko kwamba mtu yeyote ambaye atahama kutoka CCM dadika ya mwisho hatopata nafasi ya kugombea kwani ni kuwanyima haki loyalists. Chama kije na kanuni kwamba ni lazima ujiunge na CHADEMA miaka miwili kwa mfano before uchaguzi ili uweze kupata experience na chama etc
My General Take
Hadi hapa naamini kuwa Kuna kila dalili kuwa CCM itashinda, hata kama itakuwa kwa asilimia 51% za kura zote; Tofauti itakayokuwepo katika ushindi huo ni kuwa CCM itashinda kwa margine ndogo kuko zote katika historia za Chaguzi Tanzania. Mwenyekiti wa CHADEMA Mheshima Freeman Mbowe yeye kishajiapia kuwa ikishinda CCM 2015 atajiuzuru na naomba nimnukuu "Iwapo CCM itashinda uchaguzi mwaka 2015, basi nitajiuzulu Siasa". Ni kauli ya kutia moyo ya kuwa Chama kimejipanga vipi, kuwa kina uhakika wa Kazi na nguvu zake na kuwa Chama kitaikomboa nchi ifikipo 2015.
Vile vile iwapo kutakuwa na ushindi wa CHADEMA kama vile wengi wa Watanzania, Wanaharakati na Viongozi wa Chama hicho wanavyo dhania na kuamini; basi ni kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa hasa iwapo CHADEMA watapata kura nyingi ngazi ya Urais na wabunge wengi &[HASHTAG]#8211[/HASHTAG]; ila nikiri kuwa tatizo ni kwamba suala la ndoa za vyama, CHADEMA walishajifunga na umma unajua fika na kwa kiasi kikubwa namna gani CHADEMA hawakubaliani a wazo la 'Government of National Unity' kule ZNZ. Swali linabaki je ikitokea uwezekano wa GNU Tanzania bara na ikaonekana ndiyo suluhu pekee, CHADEMA watakula matapishi yao wenyewe? Hata hivyo naomba hili niliache hapa kwani ni mjadala mwingine mpya kabisa. Wanachadema... Hii nakala ni katika ku challengiana na kujitazama upya kuweza kufanikisha safari ya Ikulu.
Naomba nitumie hii nukuu ya vita from the Legendary Sun Wu. Naamini kuwa hii nukuu, inatumika vema na CCM katika tactics zake zake chafu za kisiasa hasa hizi za &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];Gutter Politics' ambazo ndio sababu pekee bado wapo hapo walipo. It is time Chadema start doing the same... (IMO).
Pamoja Saana,
AshaDii.
Kawaida kama wanadamu huwa tunakuwa na matarajio ya vitu mbali mbali, na matarajio hayo huegemea tokana na viashiria vinavyowezesha haya matarajio ku materialise. Tumetofautiana katika kusoma viashiria hasa pale amapo viashiria hivyo kuwa ni vya ku donoa donoa! Ingawa kuna viashiria vingine ambavyo huonesha WAZI kabisa kuwa matarajio ni haya iwe kwa kupenda ama kutopenda kwa watazamaji wote. Tokana na nyenendo, habari na matukio yanayotokea siku zote nchini kwetu hasa kwa yale yanayohusiana na masuala ya Siasa yananipa kutoa mtazamo huu nilotoa katika makala hii.
Ni wazi kuwa idadi kubwa ya Watanzania (na hata mataifa mengine baadhi) tunasubiri kwa hamu kuona na kushuhudia shughuli za uchaguzi mkuu 2015. Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania toka ipate uhuru mwaka 51 iliyopita itakuwa na idadi kubwa zaidi ya wanaharakati, wakereketwa na wafuasi wa vyama, wananchi wa kawaida kuvutiwa na kuwa na hamu kubwa kujua hatma ya uchaguzi na kama uongozi mkuu wa nchi utachukuliwa na Chama Pinzani ama bado kitabaki Chama tawala madarakani. Ni matumaini yangu hata idadi ya wapiga kura itaongezeka kuliko miaka ya nyuma.
Hakuna ubishi kuwa uchaguzi mkuu wa 2015 utakuwa ni kabambe, wenye kuvutia na wa muhimu pengine kuliko chaguzi nyingine zote zilizowahi kutokea. Ni uchaguzi ambao kubwa litakalotawala ni kutaka kwa shauku kuona ni nani hasa atashinda kiti cha Urais. Kwenye akili na fikra za wengi pengine hata haitajalisha na wala kutokuwa na nguvu huyo rais atakuwa ni nani; bali lenye nguvu ni kuona rais huyo atakuwa wa chama gani. Je, Chama Cha Mapinduzi bado kitakuwa kinashikilia nchi ama Wapinzani? 2015 baada ya uchaguzi ndiyo tutapata jibu kamili la swali hilo!
Hata hivyo licha ya kuwa baada ya Uchaguzi huo mkuu ndiyo tutakuwa na jibu kamili. Ukweli unabaki kuwa kuna vitu/viashiria/matendo ya vyama husika ambavyo hutoa picha kwa Wanaharakati, Wanasiasa, Wakereketwa na Wafuasi; ya kuwa Chama gani kinaonekana kinara na wana nafasi ya kuweza kushinda kiti hicho katika Uchaguzi.
Kila mmoja toka katika hayo makundi tajwa huwa na vigezo na sababu ambazo humpelekea aamini ushindi ni wa nani. Kwa mantiki hiyo siyo ajabu ukikutana na watu wawili wakawa na mawazo tofauti huku kila mmoja akiamini wazo lake ndiyo sahihi. Katika hili ambacho kinaweza toa mwanga na sababu ya kuamini mmoja kuliko mwingine ni tokana na sababu zake ambazo ataainisha kwa hoja ambazo yastahili ziwe nzito.
Maandalizi na mikakati ya kushika Uongozi wa juu wa Serikali huwa ni mzito na wakimahesabu na kwa maandalizi thabiti yaliyo jipanga vyema. Maandalizi hayo hayafanywi kwa siku moja, hayafanywi in Isolation na wala hayawezi fanikiwa kwa kubahatisha. Inahitaji nguvu ya Chama, nguvu ya uongozi wa Chama na kubwa zaidi nguvu ya wanachama ambao ndiyo Umma na ndiyo wana wajibu wa kumweka mtu katika kiti hicho kwa njia ya kura wakati wa Uchaguzi.
Hivyo basi kuna makundi matatu (Tokana na Mtazamo wangu) yanayotoa picha ya uchaguzi utakuwa vipi hasa:
A]. Kundi la wapiga Kura ambao ndiyo wananchi.
B]. Kundi la Chama Cha Mapinduzi ambacho ndio chama tawala.
C]. Kundi la wapinzani wakuu; kwa maana ya CHADEMA ambao wamekuwa ni wapinzani wakuu.
KUNDI LA WAPIGA KURA
Historia Kujirudia (hasa ya 2005)
Kuna kila dalili kwamba historia ya 2005 inaweza kujirudia i.e. watanzania wengi watakuwa wamejiandikisha kupiga kura ila wachache watakaopiga kura. Hata hivyo izingatiwe kuwa hili linaweza epushwa ama kupunguzwa kwa kiasi kikubwa kama: Kwanza iwapo Vyama pinzani, Vyombo Vya habari na Wanaharakai wa Demokrasia wataweza kuhamasisha wananchi juu ya umuhimu wa kujiandikisha kwa nguvu zaidi, na Pili ni kwa CHADEMA kuja na candidate mzuri, mashuhuri, mwenye experience ya kutosha ambaye ataweza himili na kushindana vyema na mgombea urais wa chama pinzani.
Kutokujifunga kwa wapiga kura
Watanzania wengi ambao ni wapiga kura na wanao kuwa na vitambulisho vya kupiga kura kwa nia hiyo ya kujiandikisha hawapo katika chama chochote, ni wachache ambao wapo katika vyama kwa maana ya kuwa yupo chama Fulani. So far, tunaona CHADEMA nguvu ya kuongeza wapiga kura ipo katika kubanana na hao ambao tayari ni wanachama wa CCM na wale wasio na chama ambao wanawapata pia. Tokana na furaha ipatikanapo pale wanapo faulu kuwavuta wana CCM wengi kuja Chadema inapelekea kuonekana kana kwamba Strategy yao ipo katika kuhakikisha wanachama wa CCM wanahamia CHADEMA badala ya nguvu katika kuhakikisha wanajenga &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];loyalties' kwa kuwavuta wale wasio na chama.
Woga wa Mabadiliko
Kura nyingi zipo vijijini, na wengi wao ni CCM ingawa inaenda inapungua na ni kwa sababu sio tu kwa sababu hawana upeo au elimu ya uraia bali by default, watu maeneo ya vijijini huwa ni &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];conservatives'. Hawapendi mabadiliko na ni waoga wa mabadiliko, wapo katika hali mbaya lakini bado wana amini kuwa uongozi mwingine unaweza waangamiza zaidi na kabisa.
Ukichanganya hili na kwamba tangia kupata uhuru wengi wanaishi maisha ya kujitosheleza (pa kulala, chakula, nguo) hivyo wao hawaguswi sana na matatizo ya kiuchumi kama wale wananchi ambao wapo mijini wanaotegemea formal, monetary and market based economy kuendesha maisha yako ya kila siku. Vijijini ni moja ya sababu CCM itaendelea kushinda urais na kama katika ngazi ya ubunge, ikitokea upinzani unapata kura za vijijini basi ni kutokana na wananchi husika kuvutiwa na mgombea ambae ni msomi, makini n.k. Ikiwa ni sifa ya kutukuka miongoni mwao (mfano labda Mnyaturu) kuonesha hata wao pia wana wasomi wa kuwang'arisha katika anga za siasa za nchi na siyo tu Wanyakyusa, Wachaga, Wahaya n.k wanaweza kuwa hivo.
KUNDI LA CHAMA CHA MAPINDUZI
Ni mengi ambayo Serkali ya CCM imewakosea na inaendelea kuwakosea wananchi wake, kukiwa na matukio ya kuudhunisha, sikitisha, katisha tamaa kila kunapo kucha! Hakuna unafuu popote pale na Serkali imekuwa kama imefuzu katika kupiga kote kote kwa wananchi tena panapo uma! Haya yamekuwa yakiendelea siku zote na bado yanaendelea kwa miaka kadhaa sasa.
Kwanza tujiulize ni kwa namna ipi CCM wame survive hadi hapo walipo?! Tuache yote hayo na tuanzie pale ambapo tulipata orodha ya "List of Shame" toka kwa Dr. Slaa, Orodha iliyotikisa na kusababisha viongozi hao wa juu kumaka kumfungulia kesi Dr. Slaa - suala ambalo halijafanikiwa hadi leo. Ile Orodha ilikuwa ni tosha kabisa kuwa hamasa kwa wananchi na wanaharakati kuing'oa CCM kwenye uchaguzi wa 2010. Lakini haikuwa hivyo...
Katika miongo ya miaka kumi kumekuwa na transparency kwa kiwango cha jamii nzima kujua madhaifu ya Serkali ya CCM juu ya Ufisadi uliyo kithiri kama pesa za Uswizi, Mikataba ya Madini yenye walakini kama vile wa Buzwagi, Magumashi na rushwa zilizokithiri katka utendaji kama masuala ya EPA na Richmond.
Kumekuwa na kuongezeka kwa matukio katika jamii dhidi ya wanajamii na vyama pinzani. Tumeona ni namna ipi Serkali imekuwa ikitumia vyombo vya Ulinzi na Usalama wa wananchi kwa kuharibu huo huo usalama wa wananchi na ni suala la kusikitisha kuwa tumepoteza watu katika jamii kwa kuonewa, kimakosa ama kukosa umakini wa utendaji wa vyombo hivyo vya usalama. Hali zinazidi kuwa mbaya karibu katika taasisi zote za ambazo Serkali ina wajibu wa kusimamia na kuhakikisha hali ni nzuri na huduma stahili zinatimizwa na kuwafikia wana nchi. Elimu, Uchumi, Afya, Usalama na mengine mengi yanazidi kuzorota huku Serikali ikizidi kujitazama yenyewe pamoja na viongozi wake wakuu. Kazi na nguvu yao ya Ziada kubwa imeelekezwa katika kuhakikisha wapo katika uongozi huo wa juu daima. Hili linafanya Serikali kufanya kila wanalo weza katika kuhakikisha wanafanikiwa.
Mbaya zaidi kumekuwa na kuongezeka kwa kasi juu ya suala la "Udini", tena basi udini huo ukisababishia ukosefu wa amani, uharibifu wa mali na kupoteza kwa maisha ya wananchi na viongozi wa dini. Chuki kati ya Waislamu na Wakristo inaenda kukuzwa tena kwa kubembeleza sababu tu Serkali kwa udhaifu mkubwa imeshindwa kabisa kudhibiti na kukomesha udini huo. Hali na sasa inaonesha kuwa &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];future' na usalama wa nchi ni walakini sana. Sad.
Hawajali kuwa wanawaumiza wananchi, hawajali kuwa inatoa implication gani kwa Wanasiasa, Wanaharakati, Wakereketwa na Wafuatiliaji wa mambo. Inafanya kutoa maamuzi ya kujikoroga kama vile la kujadili Bungwe lisiangaliwe 'Live' na mra tena kubadilisha msimamo. Na pia inafanya Serikali kutoa maamuzi ambayo kimsingi na kimantiki hayaeleweki; kama vile kuvunjwa kwa POAC. Ukichukulia uzito na umuhimu wa Kamati yenyewe ikiwa ilikuwa inaangalia na kufuatilia asset zenye thamani ya trillion za shilingi, inafanya kuamini kuwa ni mtu asiye na akili tu ndiyo anaweza futa ama kukubali ifutwe LA SIVYO zinatakiwa sababu za Msing sana kuwakilishwa.
Hata hivyo pamoja na matendo ya kidhaifu hayo yote, ukweli (kwa mtazamo wangu) unabaki kuwa kwa hali ilivyo sasa kisiasa ikiambatanishwa na matendo, attitude za wananchi na baadhi ya Viongozi pia na matukio infanya niamini kuwa 2015 CCM bado wana uwezo wa kuwa vinara wa Uraisi hata kama ni kwa asilimia ndogo kuliko siku zote za chaguzi kwa sababu hizi zifuatazo;
Wamejipanga Vyema
Kujipanga haijialishi ni njia ipi unatumia, kama ni chafu/safi, halali/si haliali, haki/siyo haki - inachojalisha ni mipango yako kuweza kufanikisha azma ya malengo ya mipango hiyo. Serikali ya CCM imekuwa hodari katika kuhakikisha inatengeneza mazingira wezeshi kwa wao kuweza kushinda uchaguzi mkuu ujao. Wamejitosheleza vyema katika Nyanja mbali mbali, tokana na vita baridi waliyo nayo dhidi ya wapinzani wao wakuu CHADEMA. Wamejikita katika kujizatiti kuwanyong'onyeza nguvu CHADEMA kwa kila namna inayowezekana hasa kwa kutumia madhaifu yao.
Viongozi wao wamekuwa wakijitahidi na kuweza kufanya kazi hiyo ya kwa bidii, Tumeona namna shutuma za CHADEMA kuingia mikataba na Wafadhili wa mabillioni ya shilingi (Sijui hii kesi iliishia wapi?); Tumeona suala la Kadi ya CCM ya Dr. Slaa vile ilisambaa katika vyombo vya habari ambayo mwanzo ilichukuliwa kwa wepesi na hatimaye kuweza ku 'divert' attention ya baadhi ya viongozi wa CHADEMA kwa kulitatua tatizo badala ya kuangalia mambo mengine ya msingi na yalo na tija kwa shughuli za Chama.
Wapo juu ya Taasisi
Wamekuwa wapo juu ya taasisi mbalimbali ambazo ni mhimu, msingi na kugusa jamii kwa upana. Tukiacha taasisi nyingine zote tuangalie taasisi ya Bunge letu tukufu kwa namna ambavyo limekuwa likiendishwa kwa matakwa ya Chama Cha Mapinduzi. Kumekuwa na sarakasi nyingi Bungeni hadi kupelekea lawama zilizo kithiri dhidi ya Madame Anne Makinda na ndugu Job Ndugai tokana na matendo yasiyowaridhisha wabunge wengi na wananchi kwa ujumla. Kubwa kuliko hapa karibuni kumefutwa na kuvunjwa kwa Kamati mbili (1) Kamati ya Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje iliyokua inaongozwa na Edward Lowassa na (2) Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) iliyokuwa inaongozwa na Zitto Zuberi Kabwe ambayo ilifutwa kabisa. Inaleta uwalakini sana 'timing' ya events hizi hasa tokana na kuwa ripoti za kamati hizo zilikuwa zikae wiki chache baada ya tukio. Ikumbukwe ripoti ya mwisho ya Zitto ilipeleka kura ya kutokuwa na Imani kwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda na hivo kusababisha kusimamishwa kwa mawaziri 8.
Katiba (ya sasa) inasimama upande wa Serikali iliyopo Madarakani
Katiba mpya ilitakiwa ipatikane walau 2010 ili kuwe na miaka walau mitano ya utawala chini ya Katiba mpya ili kufikia 2015, mabadiliko mengi yawe tayari yamejitokeza katika kila Nyanja hivyo kuisaidia CHADEMA na vyama vingine pinzani. Vipengele vingi vya katiba ya sasa vinakumbatia na kulinda nafasi za Uongozi uliyopo madarakani tokana na wajibu na majukumu yaliyo ainishwa kwa mujibu wa katiba. Nje ya nafasi ya Rais ambazo ni nzito na nyeti (Kama vile Mkuu wa Serikali nan chi; Amiri Jeshi Mkuu wa vikosi vya usalama na Ulinzi; Ana mamlaka ya kutaifisha mali yoyote; Ndiye anayeteua viongozi wakuu akiwemo na Jaji mkuu, wakuu wa vyombo ya ulinzi na Usalama n.k); Pia ndiye ambae anawajibika kuteua Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano ambayo ndiyo tegemezi katika chaguzi kuu.
Madhaifu ya Rais Jakaya Kikwete
Katika ila tatizo, kila uozo, kila ufisadi ama uchemvu uliotokea lawama zote zimekuwa zikienda kwa Rais JK. Hilo limepelekea kutamkwa kwa wengi wa wanaharakati, wanasiasa, wananchi na wakereketwa kuwa ni 'Udhaifu wa Kikwete'. Hii kauli inatowa picha kuwa katika akili za wengi matatizo yoote tuliyo nayo ni kana kwamba yalikuwepo tu baada ya JK kushika Urais na hayakuwepo awali. Rais Kikwete amekuwa akilaumiwa kwa matatizo yote yaliyopo toka Ufisadi, Kutowajibika, Kuangamiza nchi kuliko Serkali yake ya CCM. Kwa maana nyingine hili linaweza kupelekea Kingozo Mkuu (rais) toka CCM akapokelewa kwa mikono miwili kwa kuamini kuwa atairudisha CCM katika mstari.
KUNDI LA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
Chadema wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha wananchi wanatambua umuhimu wa Demokrasia hasa kwa njia ya mikutano na harakati za Movement for Change (M4C) ambazo zimekuwa zikifanywa katika kila maeneo ya nchi. Jitihada zao na 'results' ya hizo harakati zimekuwa wazi kiasi kwamba zimefanya viongozi wa CCM (hasa wa kitengo hicho) kuhangaika usiku na mchana namna ambayo wanaweza kuwachafua na kuwanyong'onyeza Chadema.
Imefanya kuwajengea baadhi ya Wanachadema kuamini kuwa CCM wanatishika na Slaa to the extent ambayo they are potraying, Imefanya kuzuka kwa kashfa mbali mbali dhidi ya Dr. Slaa nyingi zikiwa hazina tija wala mantiki.
Imefanya wajikite na kwa kiasi Fulani kuweza kuwayumbisha Chadema kwa kuingilia kupitia vipandikizi wao maslahi ya Chama. Kwa kiasi kikubwa Chadema wamefaulu katika kuwawezesha viongozi wengi wa CCM na serkali yenyewe kukosa usingizi. Hiyo ni 'achievement' kubwa sana; Lakini hata hivyo Chadema wanatakiwa wajitazame upya kuweza kuhakikisha wanajipanga, jikita na kuhakikisha kuwa wanashinda uchaguzi mkuu 2015.
Bado tuna miaka miwili hadi Uchaguzi mkuu kama mambo yataenda inavyostahili. Ni muda tosha wa Chadema kuweza kufanya mabadiliko. Ninachoweza kusema, hadi hapa tulipo kwa mtazamo wangu Chadema bado wana kazi kubwa kuweza kuhakikisha inafanikiwa, naamini kuwa ni muhimu wajitazame wapi nut zimelegea na wakaze katika maeneo yote husika ili kuhakikisha yanatolewa ama kufutwa kabisa.
Wameingia mtego "Siasa za Ligi na Mipasho" dhidi ya CCM
CCM ikiwa kama chama ambacho ni kikongwe na kimejijenga kuliko CHADEMA ambayo ni changa, wana nafasi kubwa, watu wa kutosha na walio jidhatiti hapo kwa ajili ya kuendesha ligi za mipasho na kushindana kwa kutafuta kwa udi na uvumba kitu gani kinaweza ivunja nguvu CHADEMA ambayo inakuwa siku kwa siku na kuonekana dhahiri kuwa ni tishio kwa CCM.
Tatizo ni kwamba CCM ni mabingwa wa Siasa za FITINA, wana uzoefu mkubwa sana katika hili hata katika siasa za ndani ya chama; CHADEMA hawana ujuzi huu na hilo litawagharimu kwani kuna kura nyingi sana ambazo zinapatikana kwa fitina, sio kwa kupitia tu nguvu ya hoja au ukweli diama fitina mwiko, kwani watanzania wengi ni mashabiki wa siasa za matukio na vituko CHADEMA wameshindwa kuja na counter strategy ya siasa za fitina kama vile za akina Nchemba, Nape na wengineo. Wananchi wengi hasa vijijini ambako ndio kuna kura nyingi - wananunua hoja za Nchemba (haijalishi wamepewa Tisheti ama lah) kuliko tunavyofikiri kwani wengi ni illiterate and ignorant.
Centralisation ya Uongozi toka Kaskazini
Inawezekana kabisa hili halikuwa kwa lengo mbaya; Lakini ni muhimu tukaelewa kwamba kwa kipindi kufikia 2010, inawezekana ilikuwa ni lazima CHADEMA kufanya hivyo kwani bado kilikuwa hakina true loyalists wengi kutoka maeneo mengine ya nchi wenye uwezo na uzoefu katika masuala ya uongozi. Ni suala ambalo CHADEMA haiwezi sema kwa jamii LAKINI ni muhimu pakawepo na mbinu mpya ya kuhakikisha hii imani ya kuwa ni "Chama cha Kaskazini" inatutwa na kufa kabisa.
Pia waeleze kuwa sasa wameshapata watu wengi wenye uwezo na muda ukifika Watanzania watajionea ni namna ipi CHADEMA itadhihirisha kwa uma kuwa Chama siyo cha Kaskazini bali cha Watanzania wote. CHADEMA wakiwa makini na wakajipanga wanaweza tumia dhaifu hili la ukanda "Kaskazini" kama strength, huku waki appeal kwa umma kwamba wawapatie watu makini toka maeneo mbali mbali ya Mkoa ili wawe msaada kwa Chama na wananchi ambao wanawataumikia. Kama ilivyo wazi hapa karibuni, Umaaruru wa Chadema umekuwa ukikuwa na kusambaa karibu nchi nzima. Hili pia linaweza punguzwa kwa kuangalia nafasi za viongozi na wajibu walio nao hasa katika Chama. Naamini kuna Watanzania wengi wana uwezo wa kuwa viongozi, inakuwa haina mantiki mtu mmoja anapokuwa na vyeo ziaidi ya Vitano na hali anaweza saidiwa na kupunguziwa majukumu.
Mapungufu makubwa ya Movement for Change (M4C)
Madhaifu ya M4C ambayo inaonesha inatokana na upungufu wa mfuko wa pesa kuweza kuendeshea. Namna harakati za M4C zilianza ni tofauti na sasa. Pengine tokana na kuchafuliwa kwake kwa kuhusishwa na vurugu ama lah, ila kama CHADEMA wana niya ya kushika Urais inabidi kuongeza nguvu na kasi katika harakati hizi.
Pia M4C imekuwa ikitumia nguvu kubwa katika kuichongea serikali ya CCM kwa uma kuliko kuhakikisha na kupigania idadi ya wapiga kura inaongezeka; Lengo ilitakiwa iwe kuhamasisha wananchi kujiandikisha kupiga kura huku chama kikijenga uwigo mpana na kukuwa idadi ya wana CDM na pia kujenga database yake mpya ambayo ingetumia katika tathmini za uchaguzi mikuu iliyopita nay a sasa
Kujenga kwa maadui wasio na Tija
CHADEMA wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha nidhamu inafanyika na viongozi wao na dhidi ya viongozi na wananchi pia. Hata hivo kwa mtazamo wangu wamekuwa haraka sana katika maamuzi ya kuchukua hatua ya kufukuza mara moja viongozi wao hadi pengine kutilia mashaka kama kweli huwa kuna chunguzi za dhati huwa zinafanywa dhidi ya watuhumiwa hao. Tayari tumeona reactions za akina Chriss Lukosi, Juliana Shonza, Mtela Mwampamba - Hawa watu walikuwa ni viongozi wa CHADEMA, hivo ina maana wanawajua vema. Ni wazi kuwa mtu ambaye ni adui mkuu ni Yule akujuae vema, maana anajua wapi pa kubofya.
Kupokea kwa Oil Chafu toka CCM
Ni ajabu sana kuwa CHADEMA wapo haraka sana katika kupokea viongozi toka chama kingine (hasa cha wapinzani wao wakuu CCM) kwa mbwembwe na matangazo. Utata unakuja pale ambapo huyo aliyejitoa CCM ni Kiongozi na akifika CDM anapewa uongozi; Hiyo ni hatarishi kama huyo mtu ni pandikizi, pia kwa namna moja ama nyingine kuwanyima haki wale ambao wanaweza hiyo nafasi nje ya huyo mgeni. Hili litatokea na ni moja ya mambo ambayo yataigharimu CHADEMA urais 2015; CHADEMA wanaweza kuepuka kuwa chama chakupokea wale wote ambao wanaogopa kusimama kama wagombea wa CCM e 2015 kutokana na nguvu ya CHADEMA
Bahati mbaya siyo kutokana na Mapenzi juu ya CHADEMA na taifa, bali kwa nafsi na ubinafsi wao. Ni muhimu CHADEMA wakaliangalia upya hili; pengine CHADEMA waje na tamko kwamba mtu yeyote ambaye atahama kutoka CCM dadika ya mwisho hatopata nafasi ya kugombea kwani ni kuwanyima haki loyalists. Chama kije na kanuni kwamba ni lazima ujiunge na CHADEMA miaka miwili kwa mfano before uchaguzi ili uweze kupata experience na chama etc
My General Take
Hadi hapa naamini kuwa Kuna kila dalili kuwa CCM itashinda, hata kama itakuwa kwa asilimia 51% za kura zote; Tofauti itakayokuwepo katika ushindi huo ni kuwa CCM itashinda kwa margine ndogo kuko zote katika historia za Chaguzi Tanzania. Mwenyekiti wa CHADEMA Mheshima Freeman Mbowe yeye kishajiapia kuwa ikishinda CCM 2015 atajiuzuru na naomba nimnukuu "Iwapo CCM itashinda uchaguzi mwaka 2015, basi nitajiuzulu Siasa". Ni kauli ya kutia moyo ya kuwa Chama kimejipanga vipi, kuwa kina uhakika wa Kazi na nguvu zake na kuwa Chama kitaikomboa nchi ifikipo 2015.
Vile vile iwapo kutakuwa na ushindi wa CHADEMA kama vile wengi wa Watanzania, Wanaharakati na Viongozi wa Chama hicho wanavyo dhania na kuamini; basi ni kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa hasa iwapo CHADEMA watapata kura nyingi ngazi ya Urais na wabunge wengi &[HASHTAG]#8211[/HASHTAG]; ila nikiri kuwa tatizo ni kwamba suala la ndoa za vyama, CHADEMA walishajifunga na umma unajua fika na kwa kiasi kikubwa namna gani CHADEMA hawakubaliani a wazo la 'Government of National Unity' kule ZNZ. Swali linabaki je ikitokea uwezekano wa GNU Tanzania bara na ikaonekana ndiyo suluhu pekee, CHADEMA watakula matapishi yao wenyewe? Hata hivyo naomba hili niliache hapa kwani ni mjadala mwingine mpya kabisa. Wanachadema... Hii nakala ni katika ku challengiana na kujitazama upya kuweza kufanikisha safari ya Ikulu.
Naomba nitumie hii nukuu ya vita from the Legendary Sun Wu. Naamini kuwa hii nukuu, inatumika vema na CCM katika tactics zake zake chafu za kisiasa hasa hizi za &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];Gutter Politics' ambazo ndio sababu pekee bado wapo hapo walipo. It is time Chadema start doing the same... (IMO).
"If your enemy is secure at all points, be prepared for him. If he is in superior strength, evade him. If your opponent is temperamental, seek to irritate him. Pretend to be weak, that he may grow arrogant. If he is taking his ease, give him no rest. If his forces are united, separate them. If sovereign and subject are in accord, put division between them. Attack him where he is unprepared, appear where you are not expected."
Pamoja Saana,
AshaDii.