Kwa kutaja mshahara wa rais,TZ yenye neema inakaribia

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
49,238
103,910
Sio maneno yangu ni maneno ya mhariri wa Gazeti Nipashe.Anasema kwa Magufuli kutaja mshahara wake Tanzania yenye neema imekaribia.Naomba kusaidiwa kuhusishanisha mambo haya mawili
 
Sio maneno yangu ni maneno ya mhariri wa Gazeti Nipashe.Anasema kwa Magufuli kutaja mshahara wake Tanzania yenye neema imekaribia.Naomba kusaidiwa kuhusishanisha mambo haya mawili
Wewe mwenyewe unatakiwa kwanza ujisaidie namna ya kuunda swali ili unayemuuliza akuelewe vizuri!

Ni ushauri tu!
 
Aiiiiiiiiii ujinga ni mzigo hata angetaja laki vibaraka wake wangeshangilia tuu! Pia movie siku zote inakuwa na behind the scene.
 
Hoja kubwa hapa ni uwazi. Kama Rais amekuwa mwazi kiasi hicho hakika mambo yatakuwa murua kabisa
 
Umesoma taarifa yote?

Kwa nini usiweke taarifa yote hapa ili tujadili points alizoziandika kuliko kujadili mstari mmoja wa mawazo yako?
 
Napita tu. Ni tajibu swali baadae, ngoja niende kanisani kwanza nikamuombee rais wetu
 
Hakuna cha neema hapo. Unadhani wale walimu wanaolipwa mshahara wa sh. Laki tatu (basic salary) kwa mwezi wanaweza kupewa nyongeza ya 100% na kufikia laki sita? Hii ni ndoto ya mchana.
 
Sio maneno yangu ni maneno ya mhariri wa Gazeti Nipashe.Anasema kwa Magufuli kutaja mshahara wake Tanzania yenye neema imekaribia.Naomba kusaidiwa kuhusishanisha mambo haya mawili
Wabongo bwana,kila jambo mnataka misaada. Sasa napo hapa unataka msaada upi wa mcc waje wakusaidie kwa hili pia? Endeleeni kudumaa kiakili kwa kutegemea misaada kwa kila jambo kwani kuna siku mtaomba misaada kwenye ndoa zenu kwa kuwataka wazungu wazae na wake/waume zenu. Nasema hivi kwa kuwa ulicho post hapa ni kama title tu ya mhariri wa gazeti la Nipashe lakini amefafanua vizuri sana kwa uandishi wake,vinginevyo kama una lengo lingine. Ushauri,nunua kwanza gazeti usome na ulielewe then utajitathmini mwenyewe kama post yako ilistahili kuwekwa hapa.
 
Back
Top Bottom