Elections 2010 Kwa hali ya muungano ilivyo kisingizio cha 'sasa zamu ya wazanzibar' hakitaeleweka

Dumelambegu

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
1,052
257
Kwa maoni yangu, hali ya muungano inaendelea kuwa mbaya. Wanaosema muungano ni imara ni viongozi tena wa chama fulani. Chuki ya wananchi wa pande hizi mbili inaendelea kukua. Sasa kwa mwenendo huo nawaonya viongozi wa hicho chama fulani wasije wakalogwa na kusema sasa ni zamu ya visiwani, wataangukia pua na watajuta. Siasa za nchi hii chini ya uongozi wa sasa zimekuza ufa kati ya bara na visiwani. Wabara hawatakubali kudanganywa tena.
 
Mzanzibari hana haki ya kutawala wabara kama mtu wa bara asivyo na haki ya kutawala zanzibar
 
Chama cha magamba kisifanye kosa hilo la kutuletea mgombea kutoka zanzibar kwa kisingizio cha sasa ni zamu yao. Nilisema kwenye threads zangu kuwa kikwete anamwandaa husein mwinyi na amemkumbatia muda mrefu ili wabara waendelee kumzoea. Nataka nimtahadhirishe tu ajifunze kilichomtokea Mzee Moi huko Kenya alipotaka Uhuru Kenyata awe rais wa nchi. Watanzania bara wa miaka 10 iliyopita siyo wa leo.
 
tetetetetete!
Kumbe mnaikubali CHI CHI MENYU enh!!
Mwajua bila CHI CHI MENYU hakuna kiongoji!!!
chacha pirika pirika ja Dr. chilala janini?
 
Kwa maoni yangu, hali ya muungano inaendelea kuwa mbaya. Wanaosema muungano ni imara ni viongozi tena wa chama fulani. Chuki ya wananchi wa pande hizi mbili inaendelea kukua. Sasa kwa mwenendo huo nawaonya viongozi wa hicho chama fulani wasije wakalogwa na kusema sasa ni zamu ya visiwani, wataangukia pua na watajuta. Siasa za nchi hii chini ya uongozi wa sasa zimekuza ufa kati ya bara na visiwani. Wabara hawatakubali kudanganywa tena.

Tanganyika wameitawala Zanzibar kwa miaka yote hii na tulivumilia.

Sisi tumeanza kulalamika kwa tunaloliamini, sioni sababu kwanini na nyinyi msonyeshe hisia zenu.

Hata hivyo, ingekuwa vyema mkadai Tanganyika yenu kuliko kutoa misimamo hii msioweza kuisimamia.

Ni ushauri tu Wakuu.
 
Nitawapongeza chama cha magamba wakichagua mgombea toka zenj kwa sababu CDM itakuwa haina mpinzani na nafasi ya urais itakuwa nyeupe.Acha wawape nafasi wazenji si ndo sera za magamba za chini chini!.Na akichaguliwa mgombea wa zenj kuwa rais kitakuwa kipimo kizuri cha ujinga walio nao watanganyika. Kama unaakili timamu kwa nini umchague mtu wa nchi nyingine awe rais wa nchi yako.AU WADANGANYIKA BADO HAMUELEWI KWAMBA ZANZIBAR NI NCHI.kalagabaho na ushamba wako!
 
Tanganyika wameitawala Zanzibar kwa miaka yote hii na tulivumilia.

Sisi tumeanza kulalamika kwa tunaloliamini, sioni sababu kwanini na nyinyi msonyeshe hisia zenu.

Hata hivyo, ingekuwa vyema mkadai Tanganyika yenu kuliko kutoa misimamo hii msioweza kuisimamia.

Ni ushauri tu Wakuu.

Sasa kama Tanganyika haipo, tunatakiwa tuidai Tanganyika yetu, ni wakati gani ambao Tanganyika ilitwala Zanzibar? Think between the line. Ukweli unabaki kuwa Wazanzibari wameendelea kushika nafasi kwenye serikali ya muungano na kuwatawala watanganyika, lakini watanganyika hawana nafasi yoyote kwenye utawala wa serikali ya Zanzibar
 
Sasa kama Tanganyika haipo, tunatakiwa tuidai Tanganyika yetu, ni wakati gani ambao Tanganyika ilitwala Zanzibar? Think between the line. Ukweli unabaki kuwa Wazanzibari wameendelea kushika nafasi kwenye serikali ya muungano na kuwatawala watanganyika, lakini watanganyika hawana nafasi yoyote kwenye utawala wa serikali ya Zanzibar

Kwetu sisi hakuna tofauti baina ya Tanzania yenu mnayoiamini na Tanganyika yenu mlioiua.

Tuliposema daini Tanganyika yenu namaanisha muandike Katiba ya Tanganyika itakayowaondoa Wazanzibari wanaoshika hizo nafasi zinazowatoa roho zenu.

Watanganyika wapate nafasi gani za utawala wa Zanzibar wakati utawala wenu wa kivamizi upo?

Kama kweli hio hali hamuitaki, onyesheni hisia zenu na sio kulalamika.

Nyie vipi?
 
Kwetu sisi hakuna tofauti baina ya Tanzania yenu mnayoiamini na Tanganyika yenu mlioiua.

Tuliposema daini Tanganyika yenu namaanisha muandike Katiba ya Tanganyika itakayowaondoa Wazanzibari wanaoshika hizo nafasi zinazowatoa roho zenu.

Watanganyika wapate nafasi gani za utawala wa Zanzibar wakati utawala wenu wa kivamizi upo?


Nyie vipi?

Tunataka serikali moja, huo ndo utakuwa muungano wa kweli, Serikali 3 zitaongeza gharama za uendeshaji nchi.

Hapo kwenye red, kwa nini unaamini kitu ambacho hakipo? Serikali ya awamu ya 2 iliongozwa na Mzanzibar, kwa hiyo huyo naye alikuwa anaongoza serikali ya tanganyika?
 
Back
Top Bottom