Kwa Fikra, Siasa na Sera hizi; Tanzania itabaki maskini!

nafikiri kauli mbiu iwe KILIMO NA VIWANDA,na tuwe na viongozi ambao ni committed,wazalendo wenye uchungu na taifa hili.waliopo sasa ni wasanii,kilimo kwanza kinaubiriwa kempinsy hotel pamoja na kunywa mvinyo.
 
nafikiri kauli mbiu iwe KILIMO NA VIWANDA,na tuwe na viongozi ambao ni committed,wazalendo wenye uchungu na taifa hili.waliopo sasa ni wasanii,kilimo kwanza kinaubiriwa kempinsy hotel pamoja na kunywa mvinyo.

Kwa muda huu siwezi amini kama tuwe tunatumia kauli hizi TUWE NA VIONGOZI WAZALENDO KWANZA. Kauli hizi bado zinatufanya tutegemee kundi la watu fulani hili kupata maendeleo.Haitawezeka kuwapa viongozi wazalendo kama wananchi wenyewe siyo wazalendo,sisi wenyewe ni viongozi tusitake kuwasubiri hao ambao tunaamini kuwa siyo wazalendo.
Kilimo hiki miaka hamsini bado umaskini na ninajiuliza ingekuwa je kama viwanda vingesisitizwa kuliko kilimo. MOST AGRALIAN SOCIETIES ARE POOR COMPARED TO INDUSTRIAL SOCIETIES. VIWANDA KWANZA.
 
Fikra,siasa na sera hizi zinazo tumiwa na viongozi na kuwaaminisha watanzania zitaifanya Tanzania ibaki maskini na tegemezi milele.

Leo nimekumbuka tangia nianze kusoma huko primary nilifundishwa kuwa KILIMO NI UTI WA MGOGO WA TAIFA. Mpaka leo nimemaliza kidato cha nne bado ninaambiwa kauli, fikra na sera hiyo hiyo.

Najiuliza kama kilimo ndo uti wa mgongo mbona mpaka leo maskini wengi ni wakulima?

Kama tunategemea kilimo sasa tutashindanaje na mataifa mengine na je hii si inaendelea kutufanya tegemezi wa watu wenye viwanda ambao wao ndo wanapanga bei?

NADHANI NI WAKATI MUAFAKA WA KUSEMA UTI WA MGONGO WA NCHI YETU NI VIWANDA KULIKO KILIMO.

TZ inaweza kufanikiwa kwa kutegemea Kilimo. Tunatakiwa tuwe na Commercial Agriculture na tuache kilimo cha mkono. Commercial Agr. inatakiwa ibase na IT ili kuongeza efficiency, hii itafanya TZ kutokuwa tegemezi kwa nchi za nje.

Price ktk global market inategemeana na supply and demand. It is true that WTO ni big SCAM ya West, lakini kama tukiwa na Technology tunaweza tukawa na comperative advantage, kwa sababu bado tutakuwa na cheap labor, ardhi, nk.
 
Mkuu unaposema IT na Commercial Agriculture and mechanised agriculture hayo yote yanapegemea viwanda mfano tractors and other farm implements lazima zitoke kwenye viwanda.
Most of advanced farms tunaimport kutoka nchi hizo hizo ambazo zinanua raw-agriculture products.Angalia bei za hizo zana za kilimo na bei ya mazao tunayo wauzia.
VIWANDA KWANZA.
 
Jamani MODS siyo kila post iweinakabalika hapa jamvini!Sasa huyu sijui form four leaver ameandika nini upupu tu.Anaijua tanzania,hajui maana ya sera,uelewa mdogo sana,tatizo shule za kata.Ukiangalia post zake hazina ata mashiko ndo maana nilikuwa ni mesusa kuja Jf bwana ondoa hizi post za huyu form four.
 
Jamani MODS siyo kila post iweinakabalika hapa jamvini!Sasa huyu sijui form four leaver ameandika nini upupu tu.Anaijua tanzania,hajui maana ya sera,uelewa mdogo sana,tatizo shule za kata.Ukiangalia post zake hazina ata mashiko ndo maana nilikuwa ni mesusa kuja Jf bwana ondoa hizi post za huyu form four.

huyu atakuwa degree material from university of ....ni.
 
Nadhani mtaongea weeeeee, lakini haina tofauti na hadithi ya nyani na mpango wa kujenga nyumba.Program zipo nzuri tu, tafiti zimefanywa nyingi tu. Tatizo letu la msingi ni moja tu, UMASIKINI WA AKILI. Tukiweza kujitambua kwamba sisi ni wanadamu kama wao, tuna uwezo wa kufikiri kama wao, tuna uwezo wa kujilisha na kulisha wengine kama wao. Na zaidi ya yote tuna umuhimu mkubwa katika hii dunia zaidi yao. Hapo ndipo ukombozi wa kweli utakapofikiwa. Una taifa lenye ukubwa wa km za mraba 900,000 na ushee, ardhi yenye rutuba, bahari, maziwa yote makuu barani africa, hakuna majanga makubwa ya kidunia kama matetemeko, vimbunga, tsunami n.k. Madini yaliyopo ardhini, mamilioni ya tani. Madini yote yenye dhamani kubwa duniani unayo. Una gesi, mafuta, uranium, coal, joto la ardhi, upepo, jua mwaka mzima, hakuna snow, hakuna jangwa, popote ukilima unapata chakula, above all una hazina ya watu 40 millioni.
Pamoja na kupewa vyote hivyo, kwa akili nyingi sana tulizonazo tunaenda kuomba msaada Sweden nchi ndogo kuliko mkoa wa kilimanjaro, yenye watu 10% ya watu wako - Shame!
VIJANA NDIO TEGEMEO LA MABADILIKO YA KIFIKRA NA KIMAENDELEO, TUSIPOSHIKAMANA NA KUONDOA HAWA VIONGOZI WAZEE WALIOCHOKA KIFIKRA NA CHAMA KILICHOPOTEZA DIRA, TUTAENDELEA NA UMASKINI NA KUITWA MASIKINI WANAOLALIA VITANDA VYA DHAHABU. WAO WAMEWEZA WANA NINI, TUACHANE NA NYIMBO ZA TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE! TUTHUBUTU KWA KUJITEGEMEA KIVITENDO (SI KWA FIKRA ZA JK), TUTAWEZA, NA TUTASONGA MBELE. TUJIKOMBOE WENYEWE KUTOKA KATIKA UTUMWA WA KIAKILI, HAKUNA WA KUTUKOMBOA ILA NI SISI WENYEWE! BY LATE BOB MARLEY.
 
Nadhani mtaongea weeeeee, lakini haina tofauti na hadithi ya nyani na mpango wa kujenga nyumba.Program zipo nzuri tu, tafiti zimefanywa nyingi tu. Tatizo letu la msingi ni moja tu, UMASIKINI WA AKILI. Tukiweza kujitambua kwamba sisi ni wanadamu kama wao, tuna uwezo wa kufikiri kama wao, tuna uwezo wa kujilisha na kulisha wengine kama wao. Na zaidi ya yote tuna umuhimu mkubwa katika hii dunia zaidi yao. Hapo ndipo ukombozi wa kweli utakapofikiwa. Una taifa lenye ukubwa wa km za mraba 900,000 na ushee, ardhi yenye rutuba, bahari, maziwa yote makuu barani africa, hakuna majanga makubwa ya kidunia kama matetemeko, vimbunga, tsunami n.k. Madini yaliyopo ardhini, mamilioni ya tani. Madini yote yenye dhamani kubwa duniani unayo. Una gesi, mafuta, uranium, coal, joto la ardhi, upepo, jua mwaka mzima, hakuna snow, hakuna jangwa, popote ukilima unapata chakula, above all una hazina ya watu 40 millioni.
Pamoja na kupewa vyote hivyo, kwa akili nyingi sana tulizonazo tunaenda kuomba msaada Sweden nchi ndogo kuliko mkoa wa kilimanjaro, yenye watu 10% ya watu wako - Shame!
VIJANA NDIO TEGEMEO LA MABADILIKO YA KIFIKRA NA KIMAENDELEO, TUSIPOSHIKAMANA NA KUONDOA HAWA VIONGOZI WAZEE WALIOCHOKA KIFIKRA NA CHAMA KILICHOPOTEZA DIRA, TUTAENDELEA NA UMASKINI NA KUITWA MASIKINI WANAOLALIA VITANDA VYA DHAHABU. WAO WAMEWEZA WANA NINI, TUACHANE NA NYIMBO ZA TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE! TUTHUBUTU KWA KUJITEGEMEA KIVITENDO (SI KWA FIKRA ZA JK), TUTAWEZA, NA TUTASONGA MBELE. TUJIKOMBOE WENYEWE KUTOKA KATIKA UTUMWA WA KIAKILI, HAKUNA WA KUTUKOMBOA ILA NI SISI WENYEWE! BY LATE BOB MARLEY.

Mkuu umenena lakini bila kuwa na dira makini nawatekelezeji wakweli hivyo vyote haviwezi saidia.Taifa limelala.
 
Jamani MODS siyo kila post iweinakabalika hapa jamvini!Sasa huyu sijui form four leaver ameandika nini upupu tu.Anaijua tanzania,hajui maana ya sera,uelewa mdogo sana,tatizo shule za kata.Ukiangalia post zake hazina ata mashiko ndo maana nilikuwa ni mesusa kuja Jf bwana ondoa hizi post za huyu form four.

Bishweko, nadhani hatutakuwa tunamtendea haki huyu kijana. napingana na mawazo yako. Ni kweli kijana bado mchanga, lakini angalau anafanya efforts za kujua kwanini sisi ni maskini, kwanini tupo hapa na wapi tumekwama. naamini kwenye jamvi hili watu wote tunajifunza, nobody is perfect 100% in each and everything. Through this platform some of us r learning a lot.

unaposema kijana ana uelewa mdogo na tatizo la St. Kata hapo ndio sikuelewi kabisa unataka kutuambia nini? Kijana si kosa lake, hongera wewe uliyesoma International school if that is the case, lakini kumbuka chimbuko la St. Kata ni nini? Tatizo si huyo kijana ni zao la mfumo tulio nao ndio wa kulaumiwa. Siasa zilizopitiliza kuliko vitendo.

Nakushauri, usimkatishe tamaa kijana kwani kwa kumwelewesha ndio anaifahamu historia, labda ambayo kutokana na mfumo tulio nao ktk elimu na sekta nyingine ndio zimemfanya kijana ame-miss some vital information. Iwapo hukufurahishwa na mtoa hoja hukuwa na lazima ya kuchangia kwa sababu unajua sana, asiyejua mwache aulize!
 
Isee haya sijui tutafikaje huko tusikokujua

Hakuna taifa lisilojua wapi linabidi lienda labdo Tanzania ya sasa.Tatizo ni kuwa mnaweza kuwa mnapotaka kwenda papo na mnamaono ya kwenda huko lakini tatizo likawa ni kwamba njia yakwenda huko hamuijui au hamna haja ya kuijua pamoja na kutokuwepo harakati makini na muwafaka za kutumia hiyo njia kusudi mfike mnapopataka.
Sera na fikra ni miongozo muhimu kufikia maendeleo ilimradi ziwe sera na fikra hai siyo zilizo kufa au pitwa na wakati.
 
Kwa Tz bado kilimo kiwe uti wa mgango, kwa nini? Nchi nyingi zilizoendelea zilianzia kwenye kilimo na mali ghafi walizokuwanazo kama vile chuma, mkaa wa mawe nk. mali ghafi hizi ndizo zilizowasaidia kuanzisha viwanda vidogovidogo na baadae vikawa vikubwa kutokana na mahitaji ya watumiaji. Najiuliza, tukihamia kwenye viwanda, mali ghafi zitatoka wapi wakati hatujajiandaa? Viwanda vichache tulivyonavyo kwa kiasi kikubwa vinategemea mali ghafi toka nje ambazo zinatumia fedha za kigeni kuziagizia, kwa mfano, viwanda vya Bakharesa vinaingiza nafaka toka nje, TBL inaagiza shairi toka nje, viwanda vya magodoro, hata vya plastic vinaagiza plastic toka nje, vya mafuta ya kula, nk. Wakati ardhi tunayo tele ya ziada. Mie naona tujikite zaidi katika kilimo, kwa jinsi tutakapozalisha mazao kwa wingi kama vile pamba, shairi, alizeti, nafaka, mpira na mengineyo ndivyo ambavyo wawekezaji wataamua kuanzisha viwanda humuhumu nchini kwa kutumia mali ghafi zilizopo kwa vile hata gharama za uzalishaji zitakuwa chini (tuondoe tatizo la umeme na bei pamoja na urasimu ktk uwekezaji). KILIMO KWANZA bora tuwe na malengo ya masoko na kuondoa fikra zilizopitwa na wakati.
 
Kwa Tz bado kilimo kiwe uti wa mgango, kwa nini? Nchi nyingi zilizoendelea zilianzia kwenye kilimo na mali ghafi walizokuwanazo kama vile chuma, mkaa wa mawe nk. mali ghafi hizi ndizo zilizowasaidia kuanzisha viwanda vidogovidogo na baadae vikawa vikubwa kutokana na mahitaji ya watumiaji. Najiuliza, tukihamia kwenye viwanda, mali ghafi zitatoka wapi wakati hatujajiandaa? Viwanda vichache tulivyonavyo kwa kiasi kikubwa vinategemea mali ghafi toka nje ambazo zinatumia fedha za kigeni kuziagizia, kwa mfano, viwanda vya Bakharesa vinaingiza nafaka toka nje, TBL inaagiza shairi toka nje, viwanda vya magodoro, hata vya plastic vinaagiza plastic toka nje, vya mafuta ya kula, nk. Wakati ardhi tunayo tele ya ziada. Mie naona tujikite zaidi katika kilimo, kwa jinsi tutakapozalisha mazao kwa wingi kama vile pamba, shairi, alizeti, nafaka, mpira na mengineyo ndivyo ambavyo wawekezaji wataamua kuanzisha viwanda humuhumu nchini kwa kutumia mali ghafi zilizopo kwa vile hata gharama za uzalishaji zitakuwa chini (tuondoe tatizo la umeme na bei pamoja na urasimu ktk uwekezaji). KILIMO KWANZA bora tuwe na malengo ya masoko na kuondoa fikra zilizopitwa na wakati.

Mkuu hapo ndo ninaposhindwa kuelewa kama na sisi tulipewa uwezo sawa kama binadam wengine.Kasumba ya kusema ata nani walianza na kilimo ndo wamefanikiwa sijui na si amini kuwa inatija.Kwani lazima kila kitu tujifunze kutoka kwao?Kwa nini na wao wasijifunze kutoka kwetu katika mafanikio.
Hii ndo inatufanya tuishi kwenye umaskini kwani tunaowaamini wasipo fauru nasi basi tunaamini kuwa hatutaweza this is dependency at its highest level.
Tukisema leo ni viwanda unadhani kipi kitatokea mkuu kama hiyo sera itakuwa imetekelezwa vizuri kama inavyotekelezwa sera ya kuendeleza umaskini Tanzania!
Tusidanganyane viwanda ni bora kuliko hiyo sera na fikra ya CCM ya kilimo kwanza.VIWANDA KWANZA.
 
Tunahitaji viongozi walio na mtazamo wa kuona mbali na sahihi ili kubadilisha hali ya mkulima wa Tanzania. Hatuhitaji misemo, hatuhitaji majigambo bali vitendo. Hebu fikiri kidogo iwapo kiwanda cha ngozi kitaweza kuzalisha viatu kwa wanafunzi na walimu wao, majeshi yote, mikanda ya suruali, mikoba ya akina mama, mabegi na masanduku. Je, utakuwa umewaondoa watu wangapi katika umaskini? Fikria iwapo tutakuwa na viwanda vya nafaka ikauzwa nadani na nje ya nchi. Fikiria iwapo kilimo chetu kitaacha kutegemea mvua bali umwagiliaji. Fikria viwanda vya nyama kama cha Kawe walichoua. Fikiria viwanda vya nguo, zikavaliwe hapa kwetu. Bila shaka umaskini wa mkulima unalelewa na viongozi tuliowaweka madaraknani. Umefika wakati wa mkulima kusema HAPANA sasa imetosha.Viongozi wetu wanendekeza vitu vya wageni lakini vya hapa hawavitaki. Hebu fikiria samani maofisini wanataka za Ulaya lakini za JKT na Magereza hawazitaki. Tuukomboe uongozi kwanza. Tupate uongozi utakao badili mifumo ya sasa hivi na kuleta mifumo yenye kuliangalia Taifa kwanza. Then Umaskini utafutika.
 
Tunahitaji viongozi walio na mtazamo wa kuona mbali na sahihi ili kubadilisha hali ya mkulima wa Tanzania. Hatuhitaji misemo, hatuhitaji majigambo bali vitendo. Hebu fikiri kidogo iwapo kiwanda cha ngozi kitaweza kuzalisha viatu kwa wanafunzi na walimu wao, majeshi yote, mikanda ya suruali, mikoba ya akina mama, mabegi na masanduku. Je, utakuwa umewaondoa watu wangapi katika umaskini? Fikria iwapo tutakuwa na viwanda vya nafaka ikauzwa nadani na nje ya nchi. Fikiria iwapo kilimo chetu kitaacha kutegemea mvua bali umwagiliaji. Fikria viwanda vya nyama kama cha Kawe walichoua. Fikiria viwanda vya nguo, zikavaliwe hapa kwetu. Bila shaka umaskini wa mkulima unalelewa na viongozi tuliowaweka madaraknani. Umefika wakati wa mkulima kusema HAPANA sasa imetosha.Viongozi wetu wanendekeza vitu vya wageni lakini vya hapa hawavitaki. Hebu fikiria samani maofisini wanataka za Ulaya lakini za JKT na Magereza hawazitaki. Tuukomboe uongozi kwanza. Tupate uongozi utakao badili mifumo ya sasa hivi na kuleta mifumo yenye kuliangalia Taifa kwanza. Then Umaskini utafutika.

Mkuu kwanini unawaza sana kuwapata viongozi wakusimaia mambo wakati nawe pia nikiongozi au unadhani viongozi hao watatoka kuzimu....nadhani wakati umefika kuamua sisi wenyewe na sikusubiri hao viongozi ambao sijui watatoka wapi.
 
Hongera kijana kwa mada yako nzuri! Ingawa umekosa muda wa kutafakari maana ya Kilimo uti wa mgongo, hii ni kweli na kwakua UTI WA MGONGO WA MTANZANIA UMETEGUKA basi usitegemee tutatembea wima na haraka, kwasasa ni mkongojo tu,
 
Back
Top Bottom