Kuzaa Nje ya Ndoa au kuwa na Wake Zaidi ya Mmoja

mujemaso

Senior Member
Apr 26, 2012
112
44
Habari wanajamvi...

Hivi juzi nilikutana na mtwasi mwenzangu na tukawa na stori za hapa na pale kuhusu maisha. Katika mazungumzo tukagusia maendeleo ya watoto shuleni.

Jamaa ana watoto wa kiume wanne na akawa analalamika kuwa watoto hawako vizuri shuleni. Ni wazito sana kuelewa masomo. Akaongeza kitu ambacho kimenifanya niandike hapa jamvini kuwa:

Akili (intelligence) kwa mtoto wa kiume inachangiwa kwa asilimia kubwa na mama yake. Kwa madai kuwa akili (intelligence) hubebwa na kijinasaba (gene) ambayo inakuwa kwenye X chromosome (ikumbukwe kuwa mtoto wa kiume huwa ni XY) hivyo baba ni asilimia ndogo sana huchangia kwenye akili ya mtoto wa kiume kwani X inachangiwa na mama. Akaendelea kusema kuwa baba huchangia kwa mtoto wa kike na akanambia kuwa yuko mbioni kutafuta mtoto wa kike ili angalau amrithishe akili.

Mazungumzo hayakuishia hapo akadai kwamba ndo maana baba zetu walikuwa wanaoa wake wengi ama wanazaa nje ya ndoa ili tu kujaribu kuwa na watoto mchanganyiko na matokeo yake unaweza ukapata mtoto mwenye akili. Akasema jaribu kuangalia familia ambazo baba ana wake wengi utakuta watoto wa mama mmoja ndo wana akili kuliko wengine. Pia watoto wa nje ya ndoa wanavyokuwa tofauti.

Swali ni je, huyu jamaa yuko sahihi? Ni kweli akili ya mtoto wa kiume inachangiwa zaidi na mama?

Nawasilisha.
 
Kweli huyu jamaa yuko sahihi?Hapana...

Kweli akili ya mtoto mama anachangia pakubwa

Ziada...cognitive ina two factors; Mazingira na urithi...!!!
 
Suala la mtoto kuwa na akili mimi nadhani kwanza ni mazingira ya namna mtoto kakulia,na uasili tu wa kati ya mtoto na mtoto,hilo jambo halihusiani na mama wala baba,tajiri au masikini,yeyote anaweza akazaliwa na akili au akazaliwa hana akili...
 
Habari wanajamvi...

Hivi juzi nilikutana na mtwasi mwenzangu na tukawa na stori za hapa na pale kuhusu maisha. Katika mazungumzo tukagusia maendeleo ya watoto shuleni.

Jamaa ana watoto wa kiume wanne na akawa analalamika kuwa watoto hawako vizuri shuleni. Ni wazito sana kuelewa masomo. Akaongeza kitu ambacho kimenifanya niandike hapa jamvini kuwa:

Akili (intelligence) kwa mtoto wa kiume inachangiwa kwa asilimia kubwa na mama yake. Kwa madai kuwa akili (intelligence) hubebwa na kijinasaba (gene) ambayo inakuwa kwenye X chromosome (ikumbukwe kuwa mtoto wa kiume huwa ni XY) hivyo baba ni asilimia ndogo sana huchangia kwenye akili ya mtoto wa kiume kwani X inachangiwa na mama. Akaendelea kusema kuwa baba huchangia kwa mtoto wa kike na akanambia kuwa yuko mbioni kutafuta mtoto wa kike ili angalau amrithishe akili.

Mazungumzo hayakuishia hapo akadai kwamba ndo maana baba zetu walikuwa wanaoa wake wengi ama wanazaa nje ya ndoa ili tu kujaribu kuwa na watoto mchanganyiko na matokeo yake unaweza ukapata mtoto mwenye akili. Akasema jaribu kuangalia familia ambazo baba ana wake wengi utakuta watoto wa mama mmoja ndo wana akili kuliko wengine. Pia watoto wa nje ya ndoa wanavyokuwa tofauti.

Swali ni je, huyu jamaa yuko sahihi? Ni kweli akili ya mtoto wa kiume inachangiwa zaidi na mama?

Nawasilisha.
Hapo nikionacho ni kwamba huyo jamaa anatafuta excuses tuu ila hayupo sahihi hata kidogo. Akili huchangiwa zaid na malezi, kurithi ni kwa kiwango kidogo sana
 
Kisayansi yupo sahihi kwambe chromosome x ndo hubeba genes za characteristics mbalimbali ,ila akiri huchangiwa pia na afya,malezi na mfumo wa maisha kiujumla
 
ukweli in kwamba motto anarithi akili kwa mama
 
Back
Top Bottom