MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
1. Golikipa Aishi Manula
Tusifiche na kuwa Wanafiki kwa Siku za karibuni amepoteza Uwezo wake na Kufungika si tu Kirahisi bali Kizembe mno.
Aambiwe awe Mkali awapo Golini hasa kwa Kuwapanga Mabeki wake ila na Yeye ajitahidi mno kupanga vyema Ukuta wake kukitokea Faulo eneo la Jirani.
2. Mabeki wa Pembeni Kapombe na Hussein
Ni Mabeki wazuri mno na wana Vipaji vya hali ya Juu ila kama wakikutana na Mawinga Viberenge na wenye Nguvu huwa na wakati mgumu sana.
Tafadhali waambiwe kuwa kutokana na leo Horoya FC wako Kwao na wanataka Kushinda ni lazima Watashambulia 99% hivyo na Wao wasipande sana na kwa leo wawe too defensive ili kutoleta Madhara.
3. Beki wa Kati Inonga
Nitakuwa ni Ngumbaru ( Mjinga ) nikikataa kuwa huyu siyo Beki mzuri na Bora kwa Sasa nchini Tanzania.
Shida ya Inonga na ambayo Binafsi huwa ananikera kama si Kuniudhi ni tabia yake ya Kujiamini kupita Kiasi hali ambayo kuna muda huwa inamgharimu na hata Kutugharimu Simba SC yetu.
Beki Inonga aambiwe kuwa leo hatutaki Ufaza ( Ubishoo ) wake bali tunataka Kazi Kazi hivyo awe anagusa na kuachia mara moja na akumbuke kuwa Horoya FC siyo Ihefu FC au Coastal Union FC za NBC Premier League yetu hapa Tanzania.
4. Winga Sakho
Akiacha Umachachari wake unaotokana na Utoto mwingi ni Bonge la Mchezaji na Mfungaji mahiri.
Leo nae aambiwe Ukweli kuwa Simba SC yetu inataka zaidi Matokeo na si Mbwembwe zake na Umachachari wake hivyo acheze Kitimu na aache Ubinafsi ( Uchoyo ) ambao Kiasili anaumiliki.
5. Kiungo Mchezeshaji Chama
Ana kila Kitu ila katika Mchezo wa Leo dhidi ya Horoya FC tafadhali aambiwe aongeze Kasi ( Speed ) yake na ajitahidi kuwa anasaidia katika Kukaba ili Kuziba njia na Kuwapunguzia Majukumu Wachezaji wenzake.
6. Mshambuliaji Baleke
Kwa muda mfupi tu aliocheza Simba SC yetu ameshatuonyesha kuwa Yeye ni Mshambuliaji mahiri na ana Kipaji hivyo hata Uongozi wa Simba SC haukukosea Kumsajili kwa Mkopo kutoka huko alikokuwa Kwao DRC.
Hata hivyo Baleke ajitahidi mno kuongeza Umakini leo kwani pamoja na kujua Kwake Kufunga Magoli magumu magumu ila kuna muda anajisahau na Kushindwa Kufunga Magoli mepesi mpaka tunaomuamini tunamshangaa.
Yote kwa yote naitakia Mchezo Mwema Leo Simba SC dhidi ya Horoya FC na Mashabiki pia tusiwe na Matokeo yetu bali tuheshimu kila Matokeo ambayo tutayapata.
Inshaallah na Amen.
Tusifiche na kuwa Wanafiki kwa Siku za karibuni amepoteza Uwezo wake na Kufungika si tu Kirahisi bali Kizembe mno.
Aambiwe awe Mkali awapo Golini hasa kwa Kuwapanga Mabeki wake ila na Yeye ajitahidi mno kupanga vyema Ukuta wake kukitokea Faulo eneo la Jirani.
2. Mabeki wa Pembeni Kapombe na Hussein
Ni Mabeki wazuri mno na wana Vipaji vya hali ya Juu ila kama wakikutana na Mawinga Viberenge na wenye Nguvu huwa na wakati mgumu sana.
Tafadhali waambiwe kuwa kutokana na leo Horoya FC wako Kwao na wanataka Kushinda ni lazima Watashambulia 99% hivyo na Wao wasipande sana na kwa leo wawe too defensive ili kutoleta Madhara.
3. Beki wa Kati Inonga
Nitakuwa ni Ngumbaru ( Mjinga ) nikikataa kuwa huyu siyo Beki mzuri na Bora kwa Sasa nchini Tanzania.
Shida ya Inonga na ambayo Binafsi huwa ananikera kama si Kuniudhi ni tabia yake ya Kujiamini kupita Kiasi hali ambayo kuna muda huwa inamgharimu na hata Kutugharimu Simba SC yetu.
Beki Inonga aambiwe kuwa leo hatutaki Ufaza ( Ubishoo ) wake bali tunataka Kazi Kazi hivyo awe anagusa na kuachia mara moja na akumbuke kuwa Horoya FC siyo Ihefu FC au Coastal Union FC za NBC Premier League yetu hapa Tanzania.
4. Winga Sakho
Akiacha Umachachari wake unaotokana na Utoto mwingi ni Bonge la Mchezaji na Mfungaji mahiri.
Leo nae aambiwe Ukweli kuwa Simba SC yetu inataka zaidi Matokeo na si Mbwembwe zake na Umachachari wake hivyo acheze Kitimu na aache Ubinafsi ( Uchoyo ) ambao Kiasili anaumiliki.
5. Kiungo Mchezeshaji Chama
Ana kila Kitu ila katika Mchezo wa Leo dhidi ya Horoya FC tafadhali aambiwe aongeze Kasi ( Speed ) yake na ajitahidi kuwa anasaidia katika Kukaba ili Kuziba njia na Kuwapunguzia Majukumu Wachezaji wenzake.
6. Mshambuliaji Baleke
Kwa muda mfupi tu aliocheza Simba SC yetu ameshatuonyesha kuwa Yeye ni Mshambuliaji mahiri na ana Kipaji hivyo hata Uongozi wa Simba SC haukukosea Kumsajili kwa Mkopo kutoka huko alikokuwa Kwao DRC.
Hata hivyo Baleke ajitahidi mno kuongeza Umakini leo kwani pamoja na kujua Kwake Kufunga Magoli magumu magumu ila kuna muda anajisahau na Kushindwa Kufunga Magoli mepesi mpaka tunaomuamini tunamshangaa.
Yote kwa yote naitakia Mchezo Mwema Leo Simba SC dhidi ya Horoya FC na Mashabiki pia tusiwe na Matokeo yetu bali tuheshimu kila Matokeo ambayo tutayapata.
Inshaallah na Amen.