hivi karibuni tulisikia Riziki ana malory kadhaa, na zaidi ya hapo tunaona na waziri wa utalii naye yumo kwenye biashara hiyo, sasa tukiwa na watu namna hiyo kweli ipo siku serikali wakapitisha sera ya kweli ya kunyanyua au kukarabati reli ya kati na nyinginezo? au ndio itakuwa ni biashara kama kawaida mpaka ndani ya baraza la mawaziri na wengineo, na kumtupilia mbali mluguru, mgogo, nyamwezi , sukumas, jita, kerewe, haya, nyambo, bazinza nk na matatizo ya reli. na zaidi ya hapo hivi karibuni wakati wa davos ambao raisi alihudhuria na kushriki mdahalo , alimsikia pm aka waziri mkuu wa kenya akisema ili kufufua uchumi ni lazima wajenge/tujenge reli na kupunguza kuziumiza hizi bara bara na mizigo mikubwa matokeo yake barabara kuharibika muda si mrefu baada ya kutengenezwa. ndio maana uchumi wa tanzania upo mifukoni mwa watu, kwani hela inayoingia au kutumiwa inaenda kwao, wakati serikli matumizi trillioni 3, mapato ni 1 trillion. na wachumi wetu? wanaona kwa kuwa hizi trillioni 3 zimeingia miongoni mwao na kujenga mahekalu nk basi uchumiunakuwa kwa kasi saana, wakati serkali haiwezi kujitosheleza hata kwa karatasi za kuandikia nyaraka, kulipa mishahara kwa wakati., kutoa nyongeza za mishahara n.k n.k