Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Ninaendelea na ule ukosoaji wangu wa mchakato wa kufikia katiba mpya; mengi ambayo ninayaandika hapa nilishayaandika nilipokosoa kwa mara ya kwanza mswada wa mchakato huu pale ulipowasilishwa kwa mara ya kwanza. Kwa vile mchakato ndio hivyo unaendelea napenda kuendelea kuonesha kuwa sababu zangu binafsi za kutounga mkono mchakato huu ulivyo sasa bado zipo.
TATIZO LA IBARA YA 34
Ibara ya 34 ya sheria ya kusimamia mchakato huu (haijafanyiwa marekebisho kushughulikia tatizo hili) inasema "Mtu ambaye jina lake limeingizwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililoanzishwa chini ya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi na Sheria ya Uchaguzi Zanzibar ya mwaka 1984, atakuwa na haki ya kupiga kura isipokuwa kama mtu huyo atakuwa amezuiwa kupiga kura na sheria nyingine yoyote"
Kimsingi, hakutakuwa na uandikishaji mpya wa wapiga kura kwa ajili ya kura ya maoni. Hili NI TATIZO. Kama kuna watu hawataki kushiriki katika kura za vyama vya siasa vya wagombea lakini wanataka kushiriki kwenye kura ya maoni wanazuiwa kufanya hivyo. Sasa, katika hali ya kawaida tunaweza kusema kuwa kama wanataka kupiga kura basi wajiandikishe kupiga kura lakini kama tulivyoona hivi karibuni kwamba kule Arumeru mwaka mmoja baadaye wametumia daftari la mwaka 2010!
BILA ya kuweka kwenye sheria lazima (lugha ya "shall") kutaka tume za uchaguzi kufanya maboresho ya daftari la wapiga kura angalau si chini ya miezi mitatu kabla ya kura maoni kuna watu wengi wanaweza kuwekwa nje ya kupigia kura ya maoni na hivyo kuwanyima haki yao ya kutumia ile ambayo nimeita kwenye ile mada nyingine "their sovereignty" kuamua katiba yao. NI LAZIMA kuwepo uandikishaji wa wapiga kuwa kwa ajili ya kura ya maoni; SI SAHIHI hata kidogo kutumia daftari la kawaida la wapiga kura au kutoweka kwenye katiba haja kwa tume za uchaguzi kufanya updating ya daftari hilo
TATIZO LA IBARA YA 36
Mojawapo ya sababu hizo ni hii inayohusiana na Uhalali wa kura ya maoni. Ibara ya 36 nina uhakika haikufanyiwa marekebisho kushughulikia tatizo nitakalolieleza hapa inazungumzia matokeo ya kura ya maoni. Kwamba, kura ya maoni itaitishwa na itakuwa ni ya siri na kuwa uhalali wake utakuwa kukubaliwa kwa katiba na wapiga kura asilimia 50 kutoka bara na asilimia 50 kutoka visiwani. Inasema hivi ibara hiyo kuhusu hili "Matokeo ya kura ya maoni yataamuliwa kwa msingi wa kuungwa mkono kwa asilimia inayozidi hamsini yajumla ya kura zote zilizopigwa kutoka Tanzania Bara na asilimia inayozidi hamsini ya jumla ya kura zote zilizopigwa kutoka Tanzania Zanzibar."
Sasa kwa juu mtu anaweza asione tatizo lakini hili nimedokeza kwenye mada nyingine sitarudia hapa. Tatizo langu kubwa ni kwamba ibara nzima ya 36 haifungi kiasi hicho cha kura na idadi ya watu watakaojitokeza kupiga kura. KIMSINGI asilimia 50 ya watakojitokeza kupiga kura itaamua katiba mpya. Hii ina maana gani?
a. HAIJALISHI ni kiasi gani cha watu kitajitokeza kupiga kura. Kwa mfano, katika chaguzi zetu zote kuu kabla ya 2010 idadi ya wapiga kura (voters turnout) haikuwa chini ya asilimia 70 ya waliojiandikisha kupiga kura isipokuwa mwaka 2010 ambapo kwa mara ya kwanza voters turn out ilikuwa chini ya asilimia 50! Hii ina maana ya kwamba, idadi ya wananchi wachache inaweza kuamua katiba mpya!
b. Kutokana na hilo la "a" hapo juu ni wazi kuwa kama daftari la wapiga kura litakuwa na watu milioni 25 tukasema kuwa ni asilimia 50 tu watajitokeza kupiga kura basi watu milioni 12.5 watapiga kura. Lakini tukisema kuwa katika hawa asilimia 50 tu inahitajika kuhalalisha katiba mpya ina maana watu milioni 6.25 ndio wataamua katiba mpya.
c. Tukikubali kinadharia tu kuwa hilo la "b" ni kweli kwenye taifa la watu karibu milioni 46 (makisio ya chini ya wakati wa kura ya maoni) basi kiasi cha watu watakopiga kura kutupatia katiba mpya itakuwa ni kama asilimia 13.5 tu ya Watanzania?
HII INA MAANA GANI?
1. Ni lazima wananchi wengi zaidi wapewe nafasi ya kujiandikisha kupiga kura kutoa maoni yao
2. Uhalali wa kura ya maoni ufungwe na kiasi cha watu watakaojitokeza kupiga kura - yaani ili kura ya maoni iwe na uhalali basi siyo chini ya asilimia 70 (tunaweza kuweka juu kidogo) ya wapiga kura lazima wajitokeze kupiga kura.
3. Katika wale watakaojitokeza kupiga kura siyo chini ya asilimia 70 wakikubali basi iwe KATIBA MPYA.
Mambo hayo matatu yakikubaliwa japo kwa kiasi cha karibu na hicho, Katiba Mpya - hata kama wakiacha mchakato mwingine kuwa kama ulivyo - itatokana kwa kiasi kikubwa na watu wengi zaidi kuliko mchakato ulivyo sasa unavyopendekeza na kutengeneza. Kwani, kwa mchakato wa sasa haiitajiki watu wengi kushiriki wala kupiga kura na hivyo hailazimishi majadiliano na makubaliano mbalimbali ni kana kwamba mkakati mzima ni kutoruhusu mijadala mikali yenye kutishia kupatikana kwa katiba yenyewe!
TATIZO LA IBARA YA 34
Ibara ya 34 ya sheria ya kusimamia mchakato huu (haijafanyiwa marekebisho kushughulikia tatizo hili) inasema "Mtu ambaye jina lake limeingizwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililoanzishwa chini ya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi na Sheria ya Uchaguzi Zanzibar ya mwaka 1984, atakuwa na haki ya kupiga kura isipokuwa kama mtu huyo atakuwa amezuiwa kupiga kura na sheria nyingine yoyote"
Kimsingi, hakutakuwa na uandikishaji mpya wa wapiga kura kwa ajili ya kura ya maoni. Hili NI TATIZO. Kama kuna watu hawataki kushiriki katika kura za vyama vya siasa vya wagombea lakini wanataka kushiriki kwenye kura ya maoni wanazuiwa kufanya hivyo. Sasa, katika hali ya kawaida tunaweza kusema kuwa kama wanataka kupiga kura basi wajiandikishe kupiga kura lakini kama tulivyoona hivi karibuni kwamba kule Arumeru mwaka mmoja baadaye wametumia daftari la mwaka 2010!
BILA ya kuweka kwenye sheria lazima (lugha ya "shall") kutaka tume za uchaguzi kufanya maboresho ya daftari la wapiga kura angalau si chini ya miezi mitatu kabla ya kura maoni kuna watu wengi wanaweza kuwekwa nje ya kupigia kura ya maoni na hivyo kuwanyima haki yao ya kutumia ile ambayo nimeita kwenye ile mada nyingine "their sovereignty" kuamua katiba yao. NI LAZIMA kuwepo uandikishaji wa wapiga kuwa kwa ajili ya kura ya maoni; SI SAHIHI hata kidogo kutumia daftari la kawaida la wapiga kura au kutoweka kwenye katiba haja kwa tume za uchaguzi kufanya updating ya daftari hilo
TATIZO LA IBARA YA 36
Mojawapo ya sababu hizo ni hii inayohusiana na Uhalali wa kura ya maoni. Ibara ya 36 nina uhakika haikufanyiwa marekebisho kushughulikia tatizo nitakalolieleza hapa inazungumzia matokeo ya kura ya maoni. Kwamba, kura ya maoni itaitishwa na itakuwa ni ya siri na kuwa uhalali wake utakuwa kukubaliwa kwa katiba na wapiga kura asilimia 50 kutoka bara na asilimia 50 kutoka visiwani. Inasema hivi ibara hiyo kuhusu hili "Matokeo ya kura ya maoni yataamuliwa kwa msingi wa kuungwa mkono kwa asilimia inayozidi hamsini yajumla ya kura zote zilizopigwa kutoka Tanzania Bara na asilimia inayozidi hamsini ya jumla ya kura zote zilizopigwa kutoka Tanzania Zanzibar."
Sasa kwa juu mtu anaweza asione tatizo lakini hili nimedokeza kwenye mada nyingine sitarudia hapa. Tatizo langu kubwa ni kwamba ibara nzima ya 36 haifungi kiasi hicho cha kura na idadi ya watu watakaojitokeza kupiga kura. KIMSINGI asilimia 50 ya watakojitokeza kupiga kura itaamua katiba mpya. Hii ina maana gani?
a. HAIJALISHI ni kiasi gani cha watu kitajitokeza kupiga kura. Kwa mfano, katika chaguzi zetu zote kuu kabla ya 2010 idadi ya wapiga kura (voters turnout) haikuwa chini ya asilimia 70 ya waliojiandikisha kupiga kura isipokuwa mwaka 2010 ambapo kwa mara ya kwanza voters turn out ilikuwa chini ya asilimia 50! Hii ina maana ya kwamba, idadi ya wananchi wachache inaweza kuamua katiba mpya!
b. Kutokana na hilo la "a" hapo juu ni wazi kuwa kama daftari la wapiga kura litakuwa na watu milioni 25 tukasema kuwa ni asilimia 50 tu watajitokeza kupiga kura basi watu milioni 12.5 watapiga kura. Lakini tukisema kuwa katika hawa asilimia 50 tu inahitajika kuhalalisha katiba mpya ina maana watu milioni 6.25 ndio wataamua katiba mpya.
c. Tukikubali kinadharia tu kuwa hilo la "b" ni kweli kwenye taifa la watu karibu milioni 46 (makisio ya chini ya wakati wa kura ya maoni) basi kiasi cha watu watakopiga kura kutupatia katiba mpya itakuwa ni kama asilimia 13.5 tu ya Watanzania?
HII INA MAANA GANI?
1. Ni lazima wananchi wengi zaidi wapewe nafasi ya kujiandikisha kupiga kura kutoa maoni yao
2. Uhalali wa kura ya maoni ufungwe na kiasi cha watu watakaojitokeza kupiga kura - yaani ili kura ya maoni iwe na uhalali basi siyo chini ya asilimia 70 (tunaweza kuweka juu kidogo) ya wapiga kura lazima wajitokeze kupiga kura.
3. Katika wale watakaojitokeza kupiga kura siyo chini ya asilimia 70 wakikubali basi iwe KATIBA MPYA.
Mambo hayo matatu yakikubaliwa japo kwa kiasi cha karibu na hicho, Katiba Mpya - hata kama wakiacha mchakato mwingine kuwa kama ulivyo - itatokana kwa kiasi kikubwa na watu wengi zaidi kuliko mchakato ulivyo sasa unavyopendekeza na kutengeneza. Kwani, kwa mchakato wa sasa haiitajiki watu wengi kushiriki wala kupiga kura na hivyo hailazimishi majadiliano na makubaliano mbalimbali ni kana kwamba mkakati mzima ni kutoruhusu mijadala mikali yenye kutishia kupatikana kwa katiba yenyewe!