Kutana na Unju Bin Unuq. Zimwi lililopata kuishi Tanzania 🇹🇿 👇🏾

TAJIRI MKUU WA MATAJIRI

JF-Expert Member
Dec 1, 2010
5,720
10,220
Kutana na unju bin unuq.👇🏾
1684621717873.jpg

Unaambiwa huyu jamaa unju bin unuq alikua ni mkazi wa pwani. Huyu unju alikua na nambo ya ajabu, moja ya mambo ya ajabu ya mtu huyu ni urefu wake, inasadikika unju alikua na urefu mkubwa ulioweza kumfanya atembee baharini na miguu yake kugusa chini.

Pia alikuwa akitembea kutoka nchi hadi nchi kutokana na urefu wake. Inasimuliwa kuwa mmoja kati ya nyayo zake unapatikana kwenye jiwe alilokanyaga huko Tabora, Tanzania, wayo wa mguu wa kushoto wakati wayo wa mguu wa kulia ulionekana kwenye jiwe alilokanyaga huko Kongo.

Inasimuliwa pia akitaka kula alikuwa akichukua samaki baharini kwa mkono na kuchoma katika jua kisha anakula. Kuhusu maisha yake inasimuliwa kuwa Unju bin Unuk hakuoa wala kuolewa kutokana na umbo lake.

Sehemu nyingine ya hadithi yake ni alipokufa Unju , aligawanyika vipandevipande kutokana na urefu wake na inasemekana kidole chake chenye urefu wa kilometa moja kasoro ndicho kilichopatikana na kuzikwa pale Bagamoyo, lakini hakuna simulizi mwili wake uliobaki uliangukia wapi.

1684621768432.jpg
Unju bin Unuq alikuwa na ndugu yake aliyejulikana kama Geofrey bin Unuk, huyu alipatikana maeneo ya Dodoma. Au kwamba Unuq baada ya kupotea kwa muda wa miaka mingi ndugu zake wa mbali sana wameonekana katika mkoa wa Dodoma.

1684621760720.jpg
Hii ni story ya kweli kama wewe ni mtu lazima utakua ushakutana na hii story, au kama ushawahi kwenda makumbusho ya bagamoyo basi utakua ushakutana na hii story.
 
Stori zingine bhana🤣🤣
Eti kidole chenye urefu wa zaidi nusu kilomita, huo mkono utakuwa na urefu gani sasa?😂🤣
Nyayo moja Tabora na ya mguu wa pili Congo, hapo alikuwa anatembea je akiamua kupasha(jogging) si atazunguka mabara yote?🤣🙌
 
Stori zingine bhana🤣🤣
Eti kidole chenye urefu wa zaidi nusu kilomita, huo mkono utakuwa na urefu gani sasa?😂🤣
Nyayo moja Tabora na ya mguu wa pili Congo, hapo alikuwa anatembea je akiamua kupasha(jogging) si atazunguka mabara yote?🤣🙌
Ndiyo maana akaitwa zimwi
 
Kutana na unju bin unuq.👇🏾
View attachment 2629397
Unaambiwa huyu jamaa unju bin unuq alikua ni mkazi wa pwani. Huyu unju alikua na nambo ya ajabu, moja ya mambo ya ajabu ya mtu huyu ni urefu wake, inasadikika unju alikua na urefu mkubwa ulioweza kumfanya atembee baharini na miguu yake kugusa chini.

Pia alikuwa akitembea kutoka nchi hadi nchi kutokana na urefu wake. Inasimuliwa kuwa mmoja kati ya nyayo zake unapatikana kwenye jiwe alilokanyaga huko Tabora, Tanzania, wayo wa mguu wa kushoto wakati wayo wa mguu wa kulia ulionekana kwenye jiwe alilokanyaga huko Kongo.

Inasimuliwa pia akitaka kula alikuwa akichukua samaki baharini kwa mkono na kuchoma katika jua kisha anakula. Kuhusu maisha yake inasimuliwa kuwa Unju bin Unuk hakuoa wala kuolewa kutokana na umbo lake.

Sehemu nyingine ya hadithi yake ni alipokufa Unju , aligawanyika vipandevipande kutokana na urefu wake na inasemekana kidole chake chenye urefu wa kilometa moja kasoro ndicho kilichopatikana na kuzikwa pale Bagamoyo, lakini hakuna simulizi mwili wake uliobaki uliangukia wapi.

View attachment 2629400Unju bin Unuq alikuwa na ndugu yake aliyejulikana kama Geofrey bin Unuk, huyu alipatikana maeneo ya Dodoma. Au kwamba Unuq baada ya kupotea kwa muda wa miaka mingi ndugu zake wa mbali sana wameonekana katika mkoa wa Dodoma.

View attachment 2629401Hii ni story ya kweli kama wewe ni mtu lazima utakua ushakutana na hii story, au kama ushawahi kwenda makumbusho ya bagamoyo basi utakua ushakutana na hii story.
Unyayo wake ulionyesha hapo kwenye jiwe ni mkubwa lakini hauashirii kuwa alikuwa mrefu kiasi cha kukatisha kwenye bahari wala kunyosha mikono juu akachoma samaki kwenye jua. Urefu wake ni sawa tu na mti wa mnazi
 
Back
Top Bottom