Kushindwa kwa sera za CCM ndio chanzo cha umaskini wa Watanzania!

Uzuri wa sera ya ccm kuhusu elimu ya msingi ni nini?

Binafsi hakuana uzuri ukizinagatia wanaomaliza la saba wengi hawajui kusoma na na kuandika, na sasa wamepitisha sera ya mtihani wa la saba utakuwa multiple choice maswali yote.
 
Sijasema kushindwa kwa "utekelezaji" wa sera; bali kushindwa kwa 'sera" zenyewe. Yaani, ni 'substantial failure" ya sera za CCM ndio chanzo hasa cha umaskini wa Watanzania.

Siyo kukosekana kwa raslimali, siyo kukosekana kwa uwezo, fedha, mipango au hata raslimali watu; bali ni uwepo wa sera ambazo zimeshindwa kuyainua maisha ya WAtanzania. Kwamba hakuna sera hata moja ya CCM ambayo imefanikiwa na ikasifiwa kwa kufanya vizuri na kuinua maisha ya watu wetu. NONE.

Siyo Sera ya Elimu
Siyo sera ya Maji
Siyo sera ya Ajira
Siyo sera ya kodi/uchumi
Siyo sera ya uwekezaji
Siyo sera ya ubinafsishaji
Siyo sera ya ulinzi na usalama (kwanza hii haipo technically)
Siyo sera ya utawala bora
Siyo sera ya madini
Siyo sera ya nishati
Siyo sera ya mazingira
Siyo sera ya Utalii
Siyo sera ya "kilimo"
Siyo sera ya afya

Sera zote zimeshindwa.

Sasa sijasema hazijajaribiwa au kwamba hazijawahi kuwa na mafanikio madogomadogo ya hapa na pale la hasha nitakuwa si msema kweli. Shule zimejengwa, vyuo vimejengwa, barabara zimejengwa n.k Lakini ukizichukua sera zote na kuziweka kwenye mizani ya kubadilisha maisha ya mamilioni ya watu wetu utaona kuwa sera hizo zimefeli. Ukishatambua hili ni rahisi kuona kuwa wanaojaribu kufanya CCM waboreshe sera zilizoshindwa wanafanya zoezi litakaloshindwa.

Hutaki?
chanzo cha umaskini wa watanzania sio sera bali ni WATANZANIA wenyewe...period......watu wa TZ na viongozi wao ndio chanzo cha matatizo yao......sera hazijitekelezi zenyewe bali zinatekelezwa na watu.......na pia sera hazijitungi zenyewe bali hutungwa na watu........
 
Ukiongelea sera zipo nzuri kwenye makaratasi lakn hazna watekelezaji wazuri ndio mana hata zinaonekana kupwaya.
 
Mzee Mwanakijiji,
Imani yangu ni kwamba mtu yeyote mpuuzi hufanya mambo yake kipuuzi vile vile na wazungu wanasema Stupid is what stupid does!...Jamani ifike mahala tukubali kwamba sio swala la CCM pekee bali ni letu sote. Sisi bongo zetu sasa hivi zimeganda hivyo kuwa kutoka Wabongo hadi kuwa Wadanganyika. Hata maziwa yakisha ganda hubadilika jina na kuwa mtindi sii maziwa tena.

Tanzania kwa ujumla wetu tupo katikati ya bahari na hatufahamu tunakwenda wapi hivi kusema JK au CCM na sera zao wakati hatuna mahala tunataka kwenda zaidi ya kuutafuta ufukwe ni hadithi mpya ya Christopher Columbus kuitafuta India huku akielekea Magharibi, tena afadhali ya yeye aliweka malengo dhaifu akaibukia na Li -nchi kubwa liitwalo AMERICA..

Nchi yetu haina DIRA mkuu, hii ndio sababu kubwa ya kushindwa kwetu sote na sio CCM wala JK wala atakaye kuja.. Tunakwenda tu bila kujua tunapokwenda na kibaya zaidi haijatokea mtu hata mmoja ambaye anaweza kusema tunataka kwenda wapi leo baada ya kuvunjika kwa dira yetu ya kitaifa ilotokana na Azimio la Arusha ama niseme Ujamaa na Kujitegemea. Leo hii CCM wanadai chama chao bado kinatekeleza malengo hayo wakati wanajua kabisa wanakoenda siko na hata wale wanaopingana na Ujamaa pia hawajui tuendako ndiko kweli tunakotaka kwenda au laa!..

Hadithi nzima ni Ubepari, jamani ubepari utawezekana vipi ikiwa nchi yetu bado maamuzi yote yako Centralised yaani kinachoamliwa Ikulu au bungeni ndicho kinapita wakati hatuna AZIMIO letu sote. Wote tunadai tuna Ubepari wakati ujamaa bado umeshika sehemu zote za maamuzi na sio kulinda maslahi ya wananchi bali kulinda uongozi na viongozi...Hivi tunaazimia kujenga taifa gani? mimi sijui pengine wenzangu nisaidieni.. Tazama ndani ya vyama vyetu, hakika chama hakina nguvu tena isipokuwa kuna watu wenye nguvu na bila wao vyama vitasambaratika. Kiongozi anaweza kutishia kuondoka chama akijua akiondoka chama kitapoteza wafuasi wake hatuoni kama hii demokrasia yetu ni UDIKTETA kwa sura tofauti. Hivi kweli Obama anaweza kutishia kuondoka Demokratic na chama kikalalama kuvunjika?. Nani Obama ndani ya chama kaa sii mwanachama tu kama wenigne aliyeomba Urais na akachaguliwa.

Tusiseme sera za CCM zimeshindwa, hazijashindwa kwa sababu wanafanikiwa kujaza kile walichokusudia. Sema wewe na mimi ndio hatuelewi, mimi na wewe ndio hatupendi wajaze pakacha lakini ndio wanalijaza hivyo japokuwa lavuja lakini wanatumaini oengine litajaa au ndio uchumi wa umwagiliaji shambani.. hawakulenga kulijaza pakacha bali vilivyopandwa chini viote..maana walishasema by 2010 watakuwa ma mabillionea 100 sasa Wewe Mtanzania mlalahoi ulitegemea ktk tombola hilo la mabillionea 100 nawe pia ulikuwemo?

Tuyatake mabadiliko kuanzia ngazi ya Ikulu jinsi inavyofanya kazi. serikali, Bunge na mahakama turudishe hata Uzalendo wa kukubali kwamba tumepotea. Tukubali tumepoteza dira na hatuna jinsi isipokuwa kufikiria upya jinsi gani tunataka kujitawala na wapi tunakwenda. Hakuna aibu wala sii ujinga kuweka malengo mapya baada ya miaka 50 tulotoka watupu.
 
Mwanakijiji,
Wadau wamechangia mengi yote yaliyosemwa yana ukweli mkubwa sana, wengi wameilaumu serikali, mimi naamini pamoja na serikali sisi wenyewe watanzania tunapaswa kubeba lawama kubwa; wananchi ndiyo wanayoipa changamoto serikali; kama unakumbuka wakati wa utawala wa Mwalimu kulikuwa na sera za maendeleo; kilimo kilipewa kipaumbele ili kuleta ajira na hatimaye maendeleo ya kiuchumi; yote hayo yalipotea baada ya utawala wa Mwalimu; kumbuka kilimo kinaajiri zaidi 60% kwa nchi zilizo kusini ya Sahara (sub Sahara countries); wakati nchi nyingi za sub Sahara zinawekeza kwa makusudi kwenye kilimo ili kuondoa umasikini uliokithiri; Tanzania iliacha matokeo yake ni haya ya umasikini, viwanda hatuna ajira zitatoka wapi? Sisi watanzania tumekuwa vigeugeu na ndiyo sababu tunachezewa na wanasiasa; tatizo sio sera za CCM ni watanzania wenyewe. Hata ikiingia Chadema madarakani kama watanzania hawatabadilika hakuna kitakachofanyika. Umegusia kupoteza dira, tatizo hatujui hata huko tunakoelekea, na hii ndiyo inayofanya tusijue kama tmepoteza dira.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Mwanakijiji,
Wadau wamechangia mengi yote yaliyosemwa yana ukweli mkubwa sana, wengi wameilaumu serikali, mimi naamini pamoja na serikali sisi wenyewe watanzania tunapaswa kubeba lawama kubwa; wananchi ndiyo wanayoipa changamoto serikali; kama unakumbuka wakati wa utawala wa Mwalimu kulikuwa na sera za maendeleo; kilimo kilipewa kipaumbele ili kuleta ajira na hatimaye maendeleo ya kiuchumi; yote hayo yalipotea baada ya utawala wa Mwalimu; kumbuka kilimo kinaajiri zaidi 60% kwa nchi zilizo kusini ya Sahara (sub Sahara countries); wakati nchi nyingi za sub Sahara zinawekeza kwa makusudi kwenye kilimo ili kuondoa umasikini uliokithiri; Tanzania iliacha matokeo yake ni haya ya umasikini, viwanda hatuna ajira zitatoka wapi? Sisi watanzania tumekuwa vigeugeu na ndiyo sababu tunachezewa na wanasiasa; tatizo sio sera za CCM ni watanzania wenyewe. Hata ikiingia Chadema madarakani kama watanzania hawatabadilika hakuna kitakachofanyika. Umegusia kupoteza dira, tatizo hatujui hata huko tunakoelekea, na hii ndiyo inayofanya tusijue kama tmepoteza dira.

Chama
Gongo la Mboto DSM


Chama,

Katika sera alizotoa Mwanakijiji nitajie moja ambayo Mwalimu alifanikiwa katika utawala wake? Mafanikio ni pale unapomkabidhi anayekufuatia kitu kilicho kamili. Na mwalimu hakufanikiwa katika hilo na mwenyewe alikiri.

Umezungumzia kilimo. Ukweli wa mambo, watanzania pamoja na elimu yao ndogo walikuwa wazalishaji wazuri wa chakula cha kujitosheleza wenyewe.

Sera moja iliyoharibu kilimo ilikuwa ni ya vijiji vya ujamaa. Na mwandisi wa sera hiyo ni JKN.
 
Chama,

Katika sera alizotoa Mwanakijiji nitajie moja ambayo Mwalimu alifanikiwa katika utawala wake? Mafanikio ni pale unapomkabidhi anayekufuatia kitu kilicho kamili. Na mwalimu hakufanikiwa katika hilo na mwenyewe alikiri.

Umezungumzia kilimo. Ukweli wa mambo, watanzania pamoja na elimu yao ndogo walikuwa wazalishaji wazuri wa chakula cha kujitosheleza wenyewe.

Sera moja iliyoharibu kilimo ilikuwa ni ya vijiji vya ujamaa. Na mwandisi wa sera hiyo ni JKN.

Zakumi,
Kwenye kujadili sera za Mwalimu kuna makundi mawili wapo waliokuwa wakati wa Mwalimu na wale wanaohadithiwa hadithi za kusadikika; wale waliokuwa wakati wa Mwalimu na bado wapo ndio pekee wanaoweza kujadili mapungufu na mafanikio ya Mwalimu; si kweli kwamba sera za vijiji vya ujamaa iliharibu kilimo; kimsingi lengo la vijiji vya ujamaa lilikuwa ni kuleta mapinduzi ya kilimo; na kwa kukuthibitishia vijiji vingi vilivyoanzishwa kwa sera za ujamaa bado vipo na wananchi wanaendelea kuishi pamoja, upo ushahidi mkubwa wa mafanikio ya sera zile ndiyo tunayoyaona sasa hivi. Mwalimu hakuwa mfalme yeye alianzisha wengine waendeleze, kutokana na viongozi wetu kukosa ubunifu wa nini kifanyike ili maendeleo yapatikane viongozi wanakimbilia kumlaumu Mwalimu kwasababu hawana cha kuwaeleza wananchi. Mwalimu alishajiendea mbele ya haki tutendelea kulaumu mpaka lini? Ni afadhali yeye alijaribu hawa viongozi tulionao wamejaribu kitu gani mpaka sasa hivi? Hata ukiwauliza wakupe mipango ya maendeleo ya miaka 5 hawana.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Chama,
Katika sera alizotoa Mwanakijiji nitajie moja ambayo Mwalimu alifanikiwa katika utawala wake? Mafanikio ni pale unapomkabidhi anayekufuatia kitu kilicho kamili. Na mwalimu hakufanikiwa katika hilo na mwenyewe alikiri.
Umezungumzia kilimo. Ukweli wa mambo, watanzania pamoja na elimu yao ndogo walikuwa wazalishaji wazuri wa chakula cha kujitosheleza wenyewe.Sera moja iliyoharibu kilimo ilikuwa ni ya vijiji vya ujamaa. Na mwandisi wa sera hiyo ni JKN.
Mzee Mwanakijiji: Re: Mdahalo: Kushindwa kwa sera za CCM ndio chanzo cha umaskini wa Watanzania!
...... Zakumi kinachojadiliwa ni sera za Chama na si mtu.
 
Mwanakijiji,

Ukweli wa mambo. Napiga mabox hapa US na naona kuwa excellence inarithishwa. Utamaduni wa sera za kwenye makaratasi ulianza zamani, na mambo yanayofanyika sasa hivi ni wajukuu.

This is where you are wrong. Nyerere alisema wazi kabisa (rejea hotuba yake ya 1995) kwamba uongozi unatakiwa uendeleze mazuri na "yale ya kipumbavu" unayaacha. Sera mpya ya nishati iliandikwa mwaka 1992 - unajua nani alikuwa Waziri wa Nishati wakati huo? Well, haikuandikwa wakati wa Nyerere! Sera ya kilimo kwanza haikuandikwa wakati wa Nyerere (Nyerere alikuwa na 'siasa ni kilimo'); Sera karibu zote zinazotumika sasa hivi zimeandikwa baada ya Mwalimu kuondoka.

Kila uongozi unapoingia madarakani haupokei tu sera za waliotangulia bila kuzikosoa. Obama alipoingia madarakani alikuja na sera zake huku akiahidi kubadilisha sera za Bush - hakuwa na wajibu wa kuendeleza sera za Bush! Leo hii kina Mitt nao wanataka wakubaliwe kwa sababu wanataka kuondoa "the failed policies of Obama"! na wanapendekeza sera zao.

Sera za Nyerere ziliishia mwaka 1985 alipoachia Urais! Sera za sasa ni kinyume kwa kiasi kikubwa kabisa na sera za Nyerere na wala hazina mfanano wowote; nakupa changamoto ni sera ipi ya CCM leo hii ambayo inafanana na ssera ya wakati wa Nyerere - give me a couple of them it you can:

Sera ya ardhi inafanana na ya Nyerere?
Sera ya Elimu inayozalisha watoto hadi wanafika form four hawajui kusoma na kuandika (SOMA NIPASHE LA J'TANO HII)
Sera ya kilimo - cha mimbono na miwa ya mafuta!?
Sera ya elimu ya juu?
Pick any...
 
Nope! sera pekee zinazofanya kazi nchini ni za chama tawala; vyama vingine vinazo sera zao lakini havitawali na hivyo sera zao hazitekelezwi.

Mwanakijiji
Ni kweli zinaotumika ni sera ni za chama tawala kabla hujalaumu hicho chama tawala hebu jiulize je hao watawala waliopewa dhamana wanazifuata? Ndio sababu binafsi ziwezi kulaumu CCM kama chama; naamini kabisa sera za CCM kama zitafuatwa zitaondoa kero nyingi; wakulaumiwa ni watanzania wenyewe; wanachama wa CCM hawafiki hata mil.8 kwa mantiki hiyo serikali hii ilichaguliwa na watanzania, ni sisi tu wananchi wa kawaida ndio wenye uwezo wa kuishinikiza serikali, kama walivyofanya madaktari ipo siku watanzania wataweza.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Ha ha ha,Sasa wapi mmefanikiwa ndugu KIKWETE,Ambapo hakuna any other Changamoto?

nchi hii changamoto haziishi bwana!
alikuwepo mwalimu hakuzimaliza
akaja mzee mwinyi hakuzimaliza
amekuja mkapa hajazimaliza
na mimi ninauhakika sitazimaliza
kwa ujumla hazitaisha!
 
Mwanakijiji
Ni kweli zinaotumika ni sera ni za chama tawala kabla hujalaumu hicho chama tawala hebu jiulize je hao watawala waliopewa dhamana wanazifuata? Ndio sababu binafsi ziwezi kulaumu CCM kama chama; naamini kabisa sera za CCM kama zitafuatwa zitaondoa kero nyingi; wakulaumiwa ni watanzania wenyewe; wanachama wa CCM hawafiki hata mil.8 kwa mantiki hiyo serikali hii ilichaguliwa na watanzania, ni sisi tu wananchi wa kawaida ndio wenye uwezo wa kuishinikiza serikali, kama walivyofanya madaktari ipo siku watanzania wataweza.

Chama
Gongo la Mboto DSM

Kumbuka JK alichaguliwa na watu karibu milioni 5 hivi... yawezekana waliomchagua ni wana CCM watupu!
 
Kwa sasa hata kama zikija sera toka mbinguni chini ya CCM hazitawezekana, labda CCM ikitoka kuwa chama tawala kwa miaka kama 10 hivi, wakirudi tena wanaweza kufanya kitu lakini kwa hali ilivyo kwa sasa haiwezekani. Mzee MM unatimiza wajibu wako kama Mtz, sisi tumeshindwa kuiondoa CCM ila watoto wetu wataitoa iwe kwa hiari au kwa lazima
 
Mwanakijiji,
Kwa muono wangu, tumeathiriwa sana na uamuzi wa wakubwa kuliweka pembeni azimio la Arusha. Kibaya zaidi, sioni hata kwenye vyama vingine kama kuna atakayekuja kutukomboa. Mazungumzo ya Mbowe na watanzania waishio Marekani miezi michache iliyopita yalinivunja moyo. Huwezi kuondokana na umaskini wakati mali na nyenzo nyingine ambazo zingekutoa kwenye umaskini umewapatia wengine kwa kisingizio cha kukosa mtaji kuvuna rasilimali hizo.
 
Mwanakijiji,
Kwa muono wangu, tumeathiriwa sana na uamuzi wa wakubwa kuliweka pembeni azimio la Arusha. Kibaya zaidi, sioni hata kwenye vyama vingine kama kuna atakayekuja kutukomboa. Mazungumzo ya Mbowe na watanzania waishio Marekani miezi michache iliyopita yalinivunja moyo. Huwezi kuondokana na umaskini wakati mali na nyenzo nyingine ambazo zingekutoa kwenye umaskini umewapatia wengine kwa kisingizio cha kukosa mtaji kuvuna rasilimali hizo.

Kinachonisumbua mara nyingi ni kuwa hivi watu wetu wanajua jinsi sera za chama tawala zinavyogusa maisha yao - wapi wanasoma, kitu gani wanasoma, wanaishi wapi, vipi, wanakula vitu gani n.k kwamba maisha yao yanatawaliwa na matokeo ya sera mbalibali.
 
Back
Top Bottom