Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Jamani hali ya hewa ni mbaya sana kwa sisi m hata vijijini. Hivi sasa nipo Kagera kwenye msiba na nipo eneo linaitwa Izibya ni Bukoba vijijini. Hapa ni usiku na tupo watu wengi kulala hapa msibani na umetokea mjadala mkali sana kuhusu hali ya uchaguzi upande wa urais na sisi m wakasema wana hakika watashinda. Hawa ni vibosile wenye pesa yao mzuri na baada ya ubishi mkubwa mwisho ikalazimika kwamba zipigwe kura za siri ili kuthibitisha kama ni kweli sisi m itashinda. Mara ukaandaliwa uchaguzi kwa taratibu ambazo wote tumekubali ulikuwa huru na haki. Jamani kumbe hatuna haja ya REDET kabisa maana umefanyika uchaguzi wa siri kabisa na matokeo yametoka hivi:
Kikwete kura 8;
Dr Slaa kura 48;
Lipumba kura 4;
Wagombea wengine hawakupata kitu.
Hii imenishitua kabisa maana hapa ni mbali sana na mji na wala hakuna mtandao wa internet kama wa JF, lakini watu wanafahamu watampigia nani kura. Kwa wale wakazi na watu waliowahi kutembelea wilaya ya Bukoba wanapafahamu. Jamani, Kikwete afanye packing ya mizigo yake maana after 31.10 hatakuwa rais wetu tena. Nimefurahishwa sana na misimamo ya wanavijiji na nimefuta ile dhana kuwa kura za sisi m zitatoka vijijini.
Habari ndio hiyo. Kwa herini.
Kikwete kura 8;
Dr Slaa kura 48;
Lipumba kura 4;
Wagombea wengine hawakupata kitu.
Hii imenishitua kabisa maana hapa ni mbali sana na mji na wala hakuna mtandao wa internet kama wa JF, lakini watu wanafahamu watampigia nani kura. Kwa wale wakazi na watu waliowahi kutembelea wilaya ya Bukoba wanapafahamu. Jamani, Kikwete afanye packing ya mizigo yake maana after 31.10 hatakuwa rais wetu tena. Nimefurahishwa sana na misimamo ya wanavijiji na nimefuta ile dhana kuwa kura za sisi m zitatoka vijijini.
Habari ndio hiyo. Kwa herini.